25 5 Mmoja alimpa talanta tano za fedha, mwingine mbili na mwingine moja; kila mmoja alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha akasa firi. Watano walikuwa wajinga na watano walikuwa na busara. Wale wajinga walichukua taa zao bila akiba ya mafuta; lakini wale wenye busara walichukua taa na mafuta ya akiba. Bwana harusi alipoka wia wale wasichana wote walisinzia, wakalala. Usiku wa manane zikapigwa kelele: ‘Bwana harusi anakuja! Tokeni nje kumlaki!’ Wasichana wote wakaamka, wakazitengeneza taa zao. Wale wajinga wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta kidogo, taa zetu zinazimika.’ Lakini wenye busara wakajibu, ‘Pengine hayatatutosha sisi na ninyi pia, afadhali nendeni kwa wauza mafuta mkajinunulie wenyewe.’ 10 Na walipokuwa wamekwenda kunu nua mafuta, bwana harusi akafika. Wale wasichana waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye kwenye karamu ya harusi na mlango uka fungwa. 11 Baadaye wale wasichana wengine pia wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mlango!’ 12 Bwana harusi akawajibu, ‘Nawaambieni kweli, siwajui.’ 13 Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa”

Watumishi Watatu Walioachiwa Talanta

14 “Pia Ufalme wa mbinguni utafananishwa na mtu aliyekuwa anasafiri, akawaita watumishi wake na kuwakabidhi mali yake.

16 “Yule aliyepewa talanta tano alikwenda mara moja kuzifa nyia biashara akapata talanta tano zaidi. 17 Yule aliyepewa tal anta mbili akafanya hivyo hivyo, akapata mbili zaidi. 18 Lakini yule mtumishi aliyepata talanta moja, alikwenda akachimba shimo akaifukia huko.

19 “Baada ya muda mrefu yule bwana wa hao watumishi alirudi akakagua hesabu za fedha zake alizowaachia. 20 Yule mtumishi aliyepokea talanta tano akaja, akaleta talanta tano zaidi. Akasema, ‘Bwana ulinikabidhi talanta tano, hizi hapa, nimezalisha talanta tano zaidi.’ 21 Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu; umekuwa mwaminifu katika machache; nitakupa mamlaka juu ya vitu vingi zaidi. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.’ 22 Yule mwenye talanta mbili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Nami nimepata faida, hizi hapa talanta mbili zaidi.’ 23 Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu; umekuwa mwaminifu katika machache, nami nitakupa mamlaka juu ya vitu vingi zaidi. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.’

Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.’

24 Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unavuna ambapo hukupanda na kukusanya ambapo hukutawanya mbegu. 25 Kwa hiyo niliogopa, nikaenda nikaificha talanta yako ardhini. Hii hapa mali yako.’

26 Lakini Bwana wake akamjibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna nisipopanda na kukusanya nisipota wanya mbegu? 27 Mbona basi hukuweka fedha zangu benki ili nita kaporudi nizichukue na faida yake? 28 Mnyang’anyeni hiyo talanta mumpatie yule mwenye talanta kumi.’ 29 Kwa maana kila mtu mwenye kitu ataongezewa, naye atakuwa navyo kwa wingi. Lakini kwa yule asiye na kitu, hata kidogo alicho nacho atanyang’anywa. 30 ‘Mtupeni huyo mtumishi asiyefaa nje kwenye giza, huko kuta kuwa na kilio na kusaga meno.’ ”

Kondoo Na Mbuzi

31 “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na malaika wote, ataketi katika kiti chake cha utukufu cha enzi. 32 Watu wa mataifa yote watakusanyika mbele yake, naye atawaten ganisha kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi. 33 Atawaweka kondoo upande wa kulia na mbuzi upande wa kushoto. 34 Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wa kulia, ‘Njooni ninyi mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme mlioandaliwa tangu mwanzo wa dunia. 35 Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula; nilikuwa na kiu mkanipa kitu cha kunywa; nilikuwa mgeni mkanikaribisha; 36 nilikuwa sina nguo, mkanivisha; nilikuwa mgonjwa mkaja kunitazama; na nilikuwa kifungoni mkaja kunitembe lea.’

37 “Kisha wale wenye haki watamjibu, ‘Bwana, ni lini tuli kuona na njaa tukakulisha au ukiwa na kiu tukakupa kitu cha kunywa ? 38 Na ni lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au ukihitaji nguo tukakuvisha? 39 Na ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’

40 “Mfalme atajibu, ‘Ninawaambia kweli, kwa jinsi ambavyo mlivyomfanyia mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlini fanyia mimi.’

41 “Kisha atawaambia wale walio kushoto kwake, ‘Ondokeni kwangu ninyi mliolaaniwa, nendeni katika moto wa milele alioan daliwa shetani na malaika zake. 42 Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu na hamkunipa kitu cha kunywa; 43 nilikuwa mgeni wala hamkunikaribisha; nilikuwa uchi hamkuni vika; na nilikuwa mgonjwa na gerezani nanyi hamkuja kunitazama.’

44 “Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au ukihitaji nguo, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’

45 “Naye atawajibu, ‘Nawaambieni kweli, kwa jinsi ambavyo hamkumfanyia mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkuni fanyia mimi.’

46 “Basi hawa wataingia katika adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.”

Wanawali Kumi

25 Nyakati hizo, ufalme wa Mungu utafanana na wanawali kumi waliokwenda kusubiri kuwasili kwa bwana arusi wakiwa na taa zao. Watano kati yao walikuwa na hekima, na watano walikuwa wajinga. Wanawali wajinga walichukua taa zao bila ya kubeba mafuta ya ziada kwa ajili ya taa zao. Wanawali wenye hekima walichukua taa zao pamoja na mafuta ya ziada kwa ajili ya taa zao katika chupa. Bwana arusi alipochelewa sana, walichoka na wote wakasinzia.

Usiku wa manane ulipofika, ikatangazwa, ‘Bwana arusi anakuja! Njooni mumlaki!’

Wasichana wote waliamka. Wakatayarisha taa zao. Lakini wanawali wajinga wakawaambia wanawali wenye hekima, ‘Tupeni mafuta kiasi kwa sababu mafuta katika taa zetu yamekwisha.’

Wanawali wenye hekima wakajibu, ‘Hapana! Mafuta tuliyonayo hayatatutosha sisi sote. Lakini nendeni kwa wauza mafuta mkanunue.’

10 Hivyo wanawali wajinga wakaenda kununua mafuta. Walipoondoka, bwana arusi akafika. Wanawali waliokuwa tayari wakaingia kwenye sherehe ya arusi pamoja na bwana arusi. Kisha mlango ukafungwa.

11 Baadaye wanawali waliokwenda kununua mafuta wakarudi. Wakasema, ‘bwana, bwana! Fungua mlango tuingie.’

12 Lakini bwana arusi akajibu, ‘Kwa hakika hapana! Wala siwajui ninyi.’

13 Hivyo iweni tayari kila wakati. Hamjui siku wala muda ambao Mwana wa Adamu atakuja.

Simulizi Kuhusu Watumishi Watatu

(Lk 19:11-27)

14 Pia, ufalme wa Mungu unafanana na mtu aliyekuwa akiondoka nyumbani kwake kusafiri safari ndefu. Aliwaita watumishi wake na kuwaweka kuwa wasimamizi wa mali zake. 15 Alimgawia kila mtumishi kiasi cha mali atakachosimamia. Alimpa mmoja talanta[a] tano. Alimpa mtumishi mwingine talanta mbili na akampa mtumishi wa tatu talanta moja. Kisha akaondoka. 16 Mtumishi aliyepewa talanta tano alikwenda akazifanyia biashara na talanta zile tano zikazaa talanta tano zingine. 17 Mtumishi aliyepewa talanta mbili alifanya vivyo hivyo. Mtumishi huyo alizifanyia biashara talanta mbili alizopewa na zikazaa talanta mbili zingine. 18 Lakini mtumishi aliyekabidhiwa talanta moja, alikwenda akachimba shimo kisha akaifukia talanta moja aliyopewa na bwana wake.

19 Baada ya muda mrefu kupita bwana wao alirudi. Aliwauliza watumishi wake walizifanyia nini talanta alizowaachia. 20 Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano alimletea bwana wake talanta tano alizomwachia na talanta zingine tano zaidi. Mtumishi akamwambia bwana wake, ‘Bwana, uliniamini ukaniachia talanta tano kuzitunza, hivyo nilizifanyia biashara na kupata talanta tano zaidi.’

21 Bwana wake akajibu, ‘Ulifanya vyema. Wewe ni mtumishi mwema unayeweza kuaminiwa. Ulifanya vizuri kwa kiasi kidogo hicho cha pesa. Hivyo nitakufanya kuwa msimamizi wa mambo makuu. Njoo usherehekee pamoja nami.’

22 Kisha mtumishi aliyepewa talanta mbili akaja kwa bwana wake. Akasema, ‘Bwana ulinipa talanta mbili ili nizitunze. Nilizifanyia biashara talanta hizi mbili na nimepata zingine mbili zaidi.’

23 Bwana wake akajibu, ‘Ulifanya vyema. Wewe ni mtumishi mwema unayeweza kuaminiwa. Ulifanya vizuri kwa kiasi kidogo hicho cha pesa. Hivyo nitakufanya kuwa msimamizi wa mambo makuu. Njoo usherehekee pamoja nami.’

24 Ndipo mtumishi aliyeachiwa talanta moja akaja kwa bwana wake. Akasema, ‘Bwana, nilijua wewe ni mkorofi sana. Unavuna usichopanda. Unakusanya mazao mahali ambapo hukupanda mbegu yoyote. 25 Hivyo niliogopa. Nilienda nikaificha talanta yako ardhini. Hii hapa ni ile talanta moja ya fedha uliyonipa.’

26 Bwana wao akamjibu, ‘Wewe ni mtumishi mbaya na mvivu! Unasema kwamba ulijua ninavuna nisichopanda na ninakusanya mazao ambayo sikupanda mbegu yo yote. 27 Hivyo ungeweka pesa yangu benki. Kisha, wakati nitakaporudi ningepata talanta yangu pamoja na faida ambayo ingezalishwa na talanta yangu.’

28 Hivyo bwana wao akawaambia watumishi wake wengine, ‘Mnyang'anyeni talanta moja mtumishi huyo na kumpa mtumishi mwenye talanta kumi. 29 Kila aliyezalisha faida atapata zaidi. Atakuwa na vingi kuzidi mahitaji yake. Lakini wale wasiotumia walivyonavyo kuleta faida watanyang'anywa kila kitu.’ 30 Kisha bwana wao akasema, ‘Mtupeni nje, gizani mtumishi huyo asiyefaa, ambako watu watalia na kusaga meno kwa maumivu.’

Yesu, Mwana wa Adamu Atawahukumu Watu Wote

31 Mwana wa Adamu atakuja akiwa katika utukufu wake, pamoja na malaika wote. Ataketi kwenye kiti chake cha enzi akiwa mfalme. 32 Watu wote wa ulimwenguni watakusanywa mbele zake, kisha atawagawa katika makundi mawili. Itakuwa kama mchungaji anavyowatenga kondoo kutoka katika kundi la mbuzi. 33 Atawaweka kondoo upande wake wa kuume na mbuzi upande wa kushoto.

34 Kisha mfalme atawaambia walio upande wake wa kuume, ‘Njooni, baba yangu ana baraka kuu kwa ajili yenu. Ufalme alioahidi ni wenu sasa. Uliandaliwa kwa ajili yenu tangu dunia ilipoumbwa. 35 Ni wenu kwa sababu nilipokuwa na njaa, mlinipa chakula. Nilipokuwa na kiu, mlinipa maji ya kunywa. Nilipokosa mahali pa kukaa, mlinikaribisha katika nyumba zenu. 36 Nilipokosa nguo, mlinipa mavazi ya kuvaa. Nilipokuwa mgonjwa, mlinijali. Nilipofungwa gerezani, mlikuja kunitembelea.’

37 Kisha wenye haki watajibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakupa chakula? Lini tulikuona una kiu tukakupa maji ya kunywa? 38 Lini tulikuona huna mahali pa kukaa tukakukaribisha katika nyumba zetu? Lini tulikuona huna nguo za kuvaa na tukakuvisha? 39 Lini tulikuona unaumwa au uko gerezani tukaja kukuona?’

40 Kisha mfalme atajibu, ‘Ukweli ni kuwa, kila mlichowafanyia mmojawapo wa watu wangu hapa, hata wale walioonekana kuwa si watu wa thamani, mlinifanyia mimi pia.’

41 Kisha mfalme atawaambia walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu. Mungu amekwisha amua kuwa mtaadhibiwa. Nendeni katika moto uwakao milele, moto ulioandaliwa kwa ajili ya yule Mwovu na malaika zake. 42 Ondokeni kwa sababu nilipokuwa na njaa, hamkunipa chakula nile. Nilipokuwa na kiu, hamkunipa maji ya kunywa. 43 Nilipokosa mahali pa kukaa, hamkunikaribisha katika nyumba zenu. Nilipokosa nguo za kuvaa, hamkunipa nguo za kuvaa. Nilipokuwa mgonjwa au mfungwa gerezani hamkunijali.’

44 Ndipo watu hao watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu? Lini tulikuona huna mahali pa kukaa? Au ni lini tulikuona huna nguo au mgonjwa au ukiwa gerezani? Tuliona haya yote lini na hatukukusaidia?’

45 Mfalme atajibu, ‘Ukweli ni kuwa, chochote mlichokataa kumfanyia mmojawapo wa watu wangu hapa, hata wale walioonekana kuwa si wa muhimu, mlikataa kunifanyia mimi.’

46 Ndipo watu hawa watakapondolewa ili kuadhibiwa milele. Lakini wenye haki watakwenda kuyafurahia maisha ya milele.”

Footnotes

  1. 25:15 talanta Moja ilikuwa kati ya kilo 27-36 za sarafu za dhahabu, fedha au shaba. Pia katika mstari wa 20,22,24 na 28.