Yesu Amponya Mtu Aliyezaliwa Kipofu

Yesu alipokuwa akipita, alimwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa. Wanafunzi wake wakamwuliza, “Bwana, ni nani aliyet enda dhambi ya kusababisha mtu huyu azaliwe kipofu, ni yeye au wazazi wake?”

Yesu akawajibu, “Huyu hakuzaliwa kipofu kwa sababu yeye au wazazi wake walitenda dhambi. Jambo hili lilitokea ili nguvu za Mungu zionekane zikifanya kazi katika maisha yake. Yatupasa tutende kazi yake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana kwa maana usiku unakuja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi. Wakati nipo ulimwenguni, Mimi ni nuru ya ulimwengu.”

Baada ya kusema haya, akatema mate kwenye udongo aka tengeneza tope kwa mate yake akampaka yule kipofu machoni. Kisha akamwambia, “Nenda kanawe uso katika kijito cha Siloamu.” Neno ‘Siloamu’ maana yake ni ‘aliyetumwa.’ Yule kipofu akaenda akanawa na akarudi akiwa anaona!

Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona akiomba omba wakauliza, “Huyu si yule kipofu aliyekuwa akiketi hapa akiomba msaada?” Baadhi wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawahakikishia kuwa yeye ndiye yule kipofu ambaye sasa anaona.

10 Wakamwuliza, “Macho yako yalifumbuliwaje?” 11 Akawaam bia, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope akanipaka machoni akaniambia niende nikaoshe uso katika kijito cha Siloamu. Nikaenda na mara baada ya kuosha uso nikaweza kuona!” 12 Wakam wuliza, “Huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”

Mafarisayo Wachunguza Kuponywa Kwa Kipofu

13 Wakampeleka yule mtu aliyeponywa upofu kwa Mafarisayo. 14 Siku hiyo Yesu aliyomponya ilikuwa siku ya sabato. 15 Mafar isayo nao wakamwambia awaeleze jinsi alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho, nikanawa uso na sasa naona.” 16 Baadhi ya Mafarisayo wakamwambia, “Huyu mtu ali yekuponya hawezi kuwa ametoka kwa Mungu kwa sababu hatimizi she ria ya kutokufanya kazi siku ya sabato.” Lakini wengine wakab isha, wakiuliza, “Anawezaje mtu mwenye dhambi kufanya maajabu ya jinsi hii?” Pakawepo na kutokuelewana kati yao . 17 Kwa hiyo wakamgeukia tena yule aliyeponywa wakamwuliza, “Wewe unamwonaje huyu mtu ambaye amekufanya ukaweza kuona?” Yeye akawajibu, “Mimi nadhani yeye ni nabii.”

18 Wale viongozi wa Wayahudi hawakuamini ya kuwa yule mtu aliwahi kuwa kipofu, mpaka walipoamuru wazazi wake waletwe; 19 wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu ambaye alizaliwa kipofu? Ikiwa ndiye, imekuwaje sasa anaweza kuona?” 20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu ambaye ali zaliwa kipofu. 21 Lakini hatujui jinsi alivyoponywa akaweza kuona, wala hatujui ni nani aliyemwezesha kuona. Mwulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.” 22 Walisema hivi kwa tahadhari kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wamekubal iana kuwa mtu ye yote atakayetamka kuwa Yesu ndiye Kristo atafu kuzwa kutoka katika ushirika wa sinagogi. 23 Ndio maana wakasema “Mwulizeni, yeye ni mtu mzima.”

24 Kwa hiyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu wakamwambia, “Tuambie kweli mbele ya Mungu. Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu ni mwenye dhambi.” 25 Akawajibu, “Kama yeye ni mwenye dhambi au sio, mimi sijui. Lakini nina hakika na jambo moja: nil ikuwa kipofu na sasa naona.”

26 Wakamwuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?” 27 Akawajibu, “Nimekwisha waambia aliyonifanyia lakini hamtaki kusikia. Mbona mnataka niwaeleze tena? Au na ninyi mna taka kuwa wafuasi wake?” 28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ni mfuasi wake. Sisi ni wafuasi wa Musa. 29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Musa. Lakini huyu mtu hatujui anakotoka.” 30 Akawa jibu, “Hii kweli ni ajabu! Hamjui anakotoka naye ameniponya upofu wangu! 31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomwabudu na kumtii. 32 Haijawahi kutokea tangu ulimwengu kuumbwa kwamba mtu amemponya kipofu wa kuzaliwa. 33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufa nya lo lote.” 34 Wao wakamjibu, Wewe ulizaliwa katika dhambi! Utawezaje kutufundisha?” Wakamfukuzia nje.

Vipofu Wa Kiroho

35 Yesu alipopata habari kuwa yule mtu aliyemfumbua macho amefukuzwa kutoka katika sinagogi, alimtafuta akamwuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?” 36 Yule mtu akamjibu, “Tafadhali nifahamishe yeye ni nani ili nipate kumwamini.” 37 Yesu akam jibu “Umekwisha mwona naye ni mimi ninayezungumza nawe.” 38 Yule mtu akamjibu huku akipiga magoti, “Bwana, naamini.”

39 Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni kutoa hukumu; ili wale walio vipofu wapate kuona; na wale wanaodhani wanaona, waonekane kuwa vipofu.”

40 Baadhi ya Mafarisayo waliomsikia akisema hivi wakauliza, “Je, unataka kusema kuwa sisi pia ni vipofu?” 41 Yesu akawa jibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, hamngekuwa na hatia. Lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi bado mna hatia.”

Yesu Amponya Aliyezaliwa Pasipo Kuwa na Uwezo wa Kuona

Yesu alipokuwa anatembea, alimwona mtu asiyeona tangu alipozaliwa. Wafuasi wake wakamwuliza, “Mwalimu, kwa nini mtu huyu alizaliwa asiyeona? Dhambi ya nani ilifanya hili litokee? Ilikuwa ni dhambi yake mwenyewe au ya wazazi wake?” Yesu akajibu, “Si dhambi yoyote ya huyo mtu wala ya wazazi wake iliyosababisha awe asiyeona. Alizaliwa asiyeona ili aweze kutumiwa kuonesha mambo makuu ambayo Mungu anaweza kufanya. Kukiwa bado ni mchana, tunapaswa kuendelea kuzifanya kazi zake Yeye aliyenituma. Usiku unakuja, na hakuna mtu atakayeweza kufanya kazi wakati wa usiku. Nikiwa bado nipo ulimwenguni, mimi ndiye nuru ya ulimwengu.”

Yesu aliposema haya, akatema mate chini kwenye udongo, akatengeneza tope na kumpaka yule asiyeona katika macho yake. Yesu akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu” (Siloamu maana yake ni “Aliyetumwa”.) Hivyo mtu yule akaenda katika bwawa lile, akanawa na kurudi akiwa mwenye kuona.

Majirani zake na wengine waliomwona akiomba omba wakasema, “Angalieni! Hivi huyu ndiye mtu yule aliyekaa siku zote na kuomba omba?”

Wengine wakasema, “Ndiyo! Yeye ndiye.” Lakini wengine wakasema, “Hapana, hawezi kuwa yeye. Huyo anafanana naye tu.”

Kisha yule mtu akasema, “Mimi ndiye mtu huyo.”

10 Wakamwuliza, “Kulitokea nini? Uliwezaje kupata kuona?”

11 Akawajibu, “Mtu yule wanayemwita Yesu alitengeneza tope akayapaka macho yangu. Kisha akaniambia ‘Nenda kanawe kwenye bwawa la Siloamu.’ Hivyo nikaenda kule na kunawa, na ndipo nikaweza kuona.”

12 Wakamwuliza, “Yuko wapi mtu huyo?”

Akajibu, “Mimi sijui aliko.”

Baadhi ya Mafarisayo Wana Maswali

13 Kisha watu wakampeleka huyo mtu kwa Mafarisayo. 14 Siku Yesu alipotengeneza yale matope na kuyaponya macho ya mtu huyo ilikuwa ni Sabato. 15 Hivyo Mafarisayo wakamwuliza huyo mtu, “Uliwezaje kuona?”

Akawajibu, “Alipaka matope katika macho yangu. Nikaenda kunawa, na sasa naweza kuona.”

16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyo mtu hatii sheria inayohusu siku ya Sabato. Kwa hiyo hatoki kwa Mungu.”

Wengine wakasema, “Lakini mtu aliye mtenda dhambi hawezi kufanya ishara kama hizi?” Hivyo hawakuelewana wao kwa wao. 17 Wakamuuliza tena huyo mtu, “Kwa vile aliponya macho yako, unasemaje juu ya mtu huyo?”

Akajibu, “Yeye ni nabii.” 18 Viongozi wa Kiyahudi walikuwa bado hawaamini kwamba haya yalimtokea mtu huyo; kwamba alikuwa haoni na sasa ameponywa. Lakini baadaye wakawaita wazazi wake. 19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mwana wenu? Mnasema alizaliwa akiwa haoni. Sasa amewezaje kuona?”

20 Wazazi wake wakajibu, “Tunafahamu kwamba mtu huyu ni mwana wetu. Na tunajua kuwa alizaliwa akiwa asiyeona. 21 Lakini hatujui kwa nini sasa anaweza kuona. Hatumjui aliyeyaponya macho yake. Muulizeni mwenyewe. Yeye ni mtu mzima anaweza kujibu mwenyewe.” 22 Walisema hivi kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Kiyahudi. Viongozi walikwisha azimia kwamba, wangemwadhibu mtu yeyote ambaye angesema Yesu alikuwa Masihi. Wangewazuia hao wasije tena kwenye sinagogi. 23 Ndiyo maana wazazi wake walisema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni yeye!”

24 Hivyo viongozi wa Kiyahudi wakamwita yule aliyekuwa haoni. Wakamwambia aingie ndani tena. Wakasema, “Unapaswa kumheshimu Mungu na kutuambia ukweli. Tunamjua mtu huyu kuwa ni mtenda dhambi.”

25 Yule mtu akajibu, “Mimi sielewi kama yeye ni mtenda dhambi. Lakini nafahamu hili: Nilikuwa sioni, na sasa naweza kuona!”

26 Wakawuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyaponyaje macho yako?”

27 Akajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia hayo. Lakini hamkutaka kunisikiliza. Kwa nini mnataka kusikia tena? Mnataka kuwa wafuasi wake pia?”

28 Kwa hili wakampigia makelele na kumtukana wakisema, “Wewe ni mfuasi wake, siyo sisi! Sisi ni wafuasi wa Musa. 29 Tunafahamu kwamba Mungu alisema na Musa. Lakini wala hatujui huyu mtu anatoka wapi!”

30 Yule mtu akajibu, “Hili linashangaza kweli! Hamjui anakotoka, lakini aliyaponya macho yangu. 31 Wote tunajua kuwa Mungu hawasikilizi watenda dhambi, bali atamsikiliza yeyote anayemwabudu na kumtii. 32 Hii ni mara ya kwanza kuwahi kusikia kwamba mtu ameponya macho ya mtu aliyezaliwa asiyeona. 33 Hivyo lazima anatoka kwa Mungu. Kama asingetoka kwa Mungu, asingefanya jambo lolote kama hili.”

34 Viongozi wa Kiyahudi wakajibu, “Ulizaliwa ukiwa umejaa dhambi. Unataka kutufundisha sisi?” Kisha wakamwambia atoke ndani ya sinagogi na kukaa nje.

Kutoona Kiroho

35 Yesu aliposikia kuwa walimlazimisha huyo mtu kuondoka, alikutana naye na kumuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”

36 Yule mtu akajibu, “Niambie ni nani huyo, bwana, ili nimwamini.” 37 Yesu akamwambia, “Umekwisha kumwona tayari. Mwana wa Adamu ndiye anayesema nawe sasa.”

38 Yule mtu akajibu, “Ndiyo, ninaamini, Bwana!” Kisha akainama na kumwabudu Yesu.

39 Yesu akasema, “Nilikuja ulimwenguni ili ulimwengu uweze kuhukumiwa. Nilikuja ili wale wasiyeona waweze kuona. Kisha nilikuja ili wale wanaofikiri wanaona waweze kuwa wasiyeona.”

40 Baadhi ya Mafarisayo walikuwa karibu na Yesu. Wakamsikia akisema haya. Wakamwuliza, “Nini? Unasema sisi pia ni wale wasiyeona?”

41 Yesu akasema, “Kama mngekuwa wasiyeona hakika, msingekuwa na hatia ya dhambi. Lakini kwa kuwa mnasema mnaona, basi bado mngali na hatia.”