Kuhusu Kuutawala Ulimi

Ndugu zangu, wengi wenu msiwe walimu, kwa maana mnafahamu kwamba sisi tufundishao tutahukumiwa vikali zaidi. Sisi sote hufanya makosa mengi. Ikiwa kuna mtu asiyekosea kwa usemi wake, huyo ni mkamilifu, naye anaweza kuutawala mwili wake wote.

Tunapowawekea farasi lijamu vinywani mwao ili watutii, tunatawala miili yao yote. Kadhalika meli, ingawa ni kubwa sana na huendeshwa na upepo mkali, lakini huongozwa na usukani mdogo sana, ikaenda ko kote anakotaka nahodha. Ulimi nao ni kiungo kidogo sana lakini hujivunia mambo makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa! Ulimi pia ni kama moto. Ulimi ni ulimwengu wa uovu kati ya viungo vyetu. Humchafua mtu nafsi nzima na kuwasha moto maisha yake yote, nao ulimi huwashwa moto wa kuzimu. Wanyama wa kila aina, ndege, nyoka na viumbe vya baharini wanafugwa na wamekwisha kufugwa na binadamu. Lakini hakuna mtu awezaye kuufuga ulimi. Ni uovu unaohangaika huku na kule, uliojaa sumu inayoua.

Kwa kutumia ulimi tunamsifu Bwana na Baba yetu na kwa ulimi huo huo tunawalaani watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu. 10 Katika kinywa hicho hicho hutoka sifa na laana. Ndugu zangu, haipaswi kuwa hivyo. 11 Je, chemchemi yaweza kutoa kutoka katika tundu moja maji matamu na maji machungu? 12 Je, ndugu zangu, mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu waweza kuzaa tini? Pia haiwezekani chemchemi ya chumvi kutoa maji matamu.

Aina Mbili Za Hekima

13 Ni nani miongoni mwenu aliye na hekima na ufahamu? Basi aonyeshe hayo kwa maisha yake mazuri na kwa matendo yake anayot enda kwa unyenyekevu utokanao na hekima. 14 Lakini ikiwa mna wivu wenye chuki na kufikiria mno maslahi yenu binafsi, msiji sifie hayo wala kuikataa kweli. 15 Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni bali ni ya kidunia; si hekima ya kiroho bali ni ya shetani. 16 Kwa maana penye wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na kila tendo ovu.

17 Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha ni yenye kupenda amani, yenye kufikiria wengine, yenye unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, na ya kweli. 18 Wapenda-amani wapandao katika amani huvuna mavuno ya haki.

Taming the Tongue

Not many of you should become teachers,(A) my fellow believers, because you know that we who teach will be judged(B) more strictly.(C) We all stumble(D) in many ways. Anyone who is never at fault in what they say(E) is perfect,(F) able to keep their whole body in check.(G)

When we put bits into the mouths of horses to make them obey us, we can turn the whole animal.(H) Or take ships as an example. Although they are so large and are driven by strong winds, they are steered by a very small rudder wherever the pilot wants to go. Likewise, the tongue is a small part of the body, but it makes great boasts.(I) Consider what a great forest is set on fire by a small spark. The tongue also is a fire,(J) a world of evil among the parts of the body. It corrupts the whole body,(K) sets the whole course of one’s life on fire, and is itself set on fire by hell.(L)

All kinds of animals, birds, reptiles and sea creatures are being tamed and have been tamed by mankind, but no human being can tame the tongue. It is a restless evil, full of deadly poison.(M)

With the tongue we praise our Lord and Father, and with it we curse human beings, who have been made in God’s likeness.(N) 10 Out of the same mouth come praise and cursing. My brothers and sisters, this should not be. 11 Can both fresh water and salt water flow from the same spring? 12 My brothers and sisters, can a fig tree bear olives, or a grapevine bear figs?(O) Neither can a salt spring produce fresh water.

Two Kinds of Wisdom

13 Who is wise and understanding among you? Let them show it(P) by their good life, by deeds(Q) done in the humility that comes from wisdom. 14 But if you harbor bitter envy and selfish ambition(R) in your hearts, do not boast about it or deny the truth.(S) 15 Such “wisdom” does not come down from heaven(T) but is earthly, unspiritual, demonic.(U) 16 For where you have envy and selfish ambition,(V) there you find disorder and every evil practice.

17 But the wisdom that comes from heaven(W) is first of all pure; then peace-loving,(X) considerate, submissive, full of mercy(Y) and good fruit, impartial and sincere.(Z) 18 Peacemakers(AA) who sow in peace reap a harvest of righteousness.(AB)