Nafasi Ya Pekee Ya Waisraeli

Ninasema kweli katika Kristo na dhamiri yangu inanishuhudia kwa njia ya Roho Mtakatifu kuwa sisemi uongo. Nina huzuni sana na uchungu usiokwisha moyoni mwangu. Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kama kufanya hivyo kungeweza kuwasaidia ndugu zangu tulio wa kabila moja. Nazungumza kuhusu Waisraeli ambao Mungu aliwateua kuwa wana wake, wakapewa utukufu wake, maagano yake, sheria yake, ibada ya kweli, na ahadi zake. Wao ni wa uzao wa mababu wa kwanza, na katika taifa lao Kristo alitoka kama mwanadamu; yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, atukuzwaye milele! Amina.

Lakini hii haina maana kwamba ahadi ya Mungu kwa wana wa Israeli imeshindwa. Kwa maana si wote ambao ni wa uzao wa Israeli ambao ni wa Israeli. Wala si wazaliwa wote wa kizazi cha Abra hamu ambao ni watoto wake. Ahadi ya Mungu kwa Abrahamu ilikuwa: “Watoto wako watatoka katika uzao wa Isaki.” Kwa maneno men gine, si wale watoto waliozaliwa na Ibrahimu kimwili ambao ni wana wa Mungu; bali ni wale watoto wa ahadi ambao wanahesabiwa kuwa kizazi cha Abrahamu. Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitarudi tena wakati kama huu na Sara atapata mtoto wa kiume.”

10 Na si hivyo tu bali pia wakati Rebeka alipozaa watoto na mume mmoja, Isaki, 11 hata kabla watoto wake mapacha hawajazal iwa wala kutenda jema au baya ili mpango wa Mungu wa kuchagua uendelee, si kwa kutegemea matendo mema bali kwa kufuatana na wito wake - 12 Rebeka aliambiwa, “Mkubwa atamhudumia mdogo.” 13 Kama Maandiko yasemavyo: “Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.”

Mungu Hana Upendeleo

14 Tusemeje basi? Kwamba Mungu ana upendeleo? La, sivyo. 15 Kwa maana Mungu alimwambia Musa, “Nitamrehemu nipendaye kumrehemu; na nitamhurumia nipendaye kumhurumia.” 16 Kwa hiyo haitegemei mapenzi ya mtu au jitihada ya mtu, bali hutegemea huruma ya Mungu. 17 Kwa maana katika Maandiko Farao anaambiwa, “Nilikuinua kwa makusudi ya kudhihirisha nguvu zangu kwako na jina langu lipate kutangazwa duniani pote.” 18 Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia mtu ye yote apendaye kumhurumia na huufanya mgumu moyo wa mtu ye yote atakaye.

19 Bila shaka mtaniuliza, “Kama ni hivyo, kwa nini Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kushindana na mapenzi yake? 20 Lakini wewe mwanadamu, una haki gani ya kumhoji Mungu? Je, kilichotengenezwa kinaweza kumwuliza aliyekitengeneza, “Kwa nini umenitengeneza hivi?” 21 Je, mfinyanzi hana haki ya kufa nya apendavyo na udongo wake? Je, si anaweza kabisa kutumia sehemu ya udongo huo kutengeneza chombo kimoja kitumikacho kwa kupamba na kutoka katika udongo huo huo akatengeneza kingine kwa matumizi ya kawaida?

22 Tunajuaje kama Mungu, kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na nguvu yake, amewavumilia kwa uvumilivu mkuu wale waliomkasi risha, ambao wameandaliwa kuangamizwa? 23 Na tunajuaje kama Mungu alifanya hivi ili kuwadhihirishia utajiri wa utukufu wake wale anaowahurumia, ambao aliwaandaa tangu mwanzo kupokea utu kufu? 24 Na sisi ndio hao walioitwa, si kutoka kwa Wayahudi tu bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.

Yote Yalitabiriwa Katika Maandiko

25 Hivi ndivyo Mungu asemavyo katika kitabu cha Hosea, “Wale ambao hawakuwa watu wangu, nitawaita ‘watu wangu,’ na wale ambao hawakuwa wapendwa wangu, nitawaita ‘wapendwa wangu’.” 26 Na pale pale walipoambiwa,“Ninyi si ‘watu wangu,’ ndipo watakapoitwa, ‘Wana wa Mungu aliye hai’.” 27 Na Isaya anasema hivi kuhusu Israeli: “Ijapokuwa wana wa Israeli watakuwa wengi kama mchanga wa bahari, ni wachache tu miongoni mwao watakaooko lewa;

28 kwa maana Mungu ataitekeleza hukumu yakejuu ya ulimwengu mara moja na kuikamilisha.” 29 Na tena kama alivyotabiri Isaya,“Kama Bwana wa majeshi asingetuachia uzao, tungalikuwa kama Sodoma, na kufanywa kama Gomora.”

30 Kwa hiyo tusemeje basi? Watu wa mataifa ambao hawakuta futa kupata haki wamepewa haki kwa njia ya imani. 31 Lakini Waisraeli ambao wametafuta kupata haki kwa msingi wa sheria, hawakuipata kwa maana hawakutimiza sheria. 32 Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa imani bali kwa kutegemea matendo. Wali jikwaa kwenye lile ‘jiwe la kujikwaa.’ 33 Kama ilivyoandikwa kwe nye Maandiko,“Tazama naweka jiwe huko Sayuni ambalo linawafanya watu kujikwaa na mwamba utakaowaangusha, na wale watakaomtegemea hawataaibika kamwe.”

Paul’s Anguish Over Israel

I speak the truth in Christ—I am not lying,(A) my conscience confirms(B) it through the Holy Spirit— I have great sorrow and unceasing anguish in my heart. For I could wish that I myself(C) were cursed(D) and cut off from Christ for the sake of my people,(E) those of my own race,(F) the people of Israel.(G) Theirs is the adoption to sonship;(H) theirs the divine glory,(I) the covenants,(J) the receiving of the law,(K) the temple worship(L) and the promises.(M) Theirs are the patriarchs,(N) and from them is traced the human ancestry of the Messiah,(O) who is God over all,(P) forever praised![a](Q) Amen.

God’s Sovereign Choice

It is not as though God’s word(R) had failed. For not all who are descended from Israel are Israel.(S) Nor because they are his descendants are they all Abraham’s children. On the contrary, “It is through Isaac that your offspring will be reckoned.”[b](T) In other words, it is not the children by physical descent who are God’s children,(U) but it is the children of the promise who are regarded as Abraham’s offspring.(V) For this was how the promise was stated: “At the appointed time I will return, and Sarah will have a son.”[c](W)

10 Not only that, but Rebekah’s children were conceived at the same time by our father Isaac.(X) 11 Yet, before the twins were born or had done anything good or bad(Y)—in order that God’s purpose(Z) in election might stand: 12 not by works but by him who calls—she was told, “The older will serve the younger.”[d](AA) 13 Just as it is written: “Jacob I loved, but Esau I hated.”[e](AB)

14 What then shall we say?(AC) Is God unjust? Not at all!(AD) 15 For he says to Moses,

“I will have mercy on whom I have mercy,
    and I will have compassion on whom I have compassion.”[f](AE)

16 It does not, therefore, depend on human desire or effort, but on God’s mercy.(AF) 17 For Scripture says to Pharaoh: “I raised you up for this very purpose, that I might display my power in you and that my name might be proclaimed in all the earth.”[g](AG) 18 Therefore God has mercy on whom he wants to have mercy, and he hardens whom he wants to harden.(AH)

19 One of you will say to me:(AI) “Then why does God still blame us?(AJ) For who is able to resist his will?”(AK) 20 But who are you, a human being, to talk back to God?(AL) “Shall what is formed say to the one who formed it,(AM) ‘Why did you make me like this?’”[h](AN) 21 Does not the potter have the right to make out of the same lump of clay some pottery for special purposes and some for common use?(AO)

22 What if God, although choosing to show his wrath and make his power known, bore with great patience(AP) the objects of his wrath—prepared for destruction?(AQ) 23 What if he did this to make the riches of his glory(AR) known to the objects of his mercy, whom he prepared in advance for glory(AS) 24 even us, whom he also called,(AT) not only from the Jews but also from the Gentiles?(AU) 25 As he says in Hosea:

“I will call them ‘my people’ who are not my people;
    and I will call her ‘my loved one’ who is not my loved one,”[i](AV)

26 and,

“In the very place where it was said to them,
    ‘You are not my people,’
    there they will be called ‘children of the living God.’”[j](AW)

27 Isaiah cries out concerning Israel:

“Though the number of the Israelites be like the sand by the sea,(AX)
    only the remnant will be saved.(AY)
28 For the Lord will carry out
    his sentence on earth with speed and finality.”[k](AZ)

29 It is just as Isaiah said previously:

“Unless the Lord Almighty(BA)
    had left us descendants,
we would have become like Sodom,
    we would have been like Gomorrah.”[l](BB)

Israel’s Unbelief

30 What then shall we say?(BC) That the Gentiles, who did not pursue righteousness, have obtained it, a righteousness that is by faith;(BD) 31 but the people of Israel, who pursued the law as the way of righteousness,(BE) have not attained their goal.(BF) 32 Why not? Because they pursued it not by faith but as if it were by works. They stumbled over the stumbling stone.(BG) 33 As it is written:

“See, I lay in Zion a stone that causes people to stumble
    and a rock that makes them fall,
    and the one who believes in him will never be put to shame.”[m](BH)

Footnotes

  1. Romans 9:5 Or Messiah, who is over all. God be forever praised! Or Messiah. God who is over all be forever praised!
  2. Romans 9:7 Gen. 21:12
  3. Romans 9:9 Gen. 18:10,14
  4. Romans 9:12 Gen. 25:23
  5. Romans 9:13 Mal. 1:2,3
  6. Romans 9:15 Exodus 33:19
  7. Romans 9:17 Exodus 9:16
  8. Romans 9:20 Isaiah 29:16; 45:9
  9. Romans 9:25 Hosea 2:23
  10. Romans 9:26 Hosea 1:10
  11. Romans 9:28 Isaiah 10:22,23 (see Septuagint)
  12. Romans 9:29 Isaiah 1:9
  13. Romans 9:33 Isaiah 8:14; 28:16