Kuwa Na Amani Na Mungu

Basi, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo. Kwa kupitia kwake tumepata njia ya kufikia neema hii ambayo inatuwezesha kusimama imara, tukifurahia tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu. Zaidi ya hayo, pia tunafurahia mateso yetu kwa sababu tunafahamu kuwa mateso huleta subira; na subira huleta uthabiti wa moyo; na uthabiti wa moyo hujenga tumaini. Tukiwa na tumaini hatuwezi kukata tamaa kwa sababu Mungu amekwisha kumimina upendo wake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ni zawadi tuliyopewa na Mungu.

Tulipokuwa tungali wanyonge, wakati aliochagua Mungu, Kristo aliwafia wenye dhambi. Ni vigumu sana kwa mtu kujitolea kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa yawezekana mtu akajitolea kufa kwa ajili ya mtu mwema. Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo ali kufa kwa ajili yetu.

Basi, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa damu yake, bila shaka atatuokoa kutoka katika ghadhabu ya Mungu. 10 Kwa kuwa kama tulipokuwa maadui wa Mungu tulipatanishwa kwa kifo cha Mwanae, bila shaka sasa kwa kuwa tumepatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake. 11 Si hivyo tu, bali pia tunamfurahia Mungu katika Bwana wetu Yesu Kristo ambaye kwa ajili yake tumepokea upatanisho wetu.

Adamu Alileta Kifo, Yesu Ameleta Uzima

12 Kwa hiyo kama vile ambavyo dhambi iliingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na dhambi ikaleta kifo, na kwa njia hiyo kifo kikawajia watu wote kwa kuwa wote walitenda dhambi -

13 kwa maana kabla sheria haijatolewa dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi ambapo hakuna sheria. 14 Hata hivyo tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Musa, kifo kiliwatawala watuwote hata wale ambao dhambi zao hazikuwa kama uasi wa Adamu. Adamu alikuwa mfano wa yule ambaye angalikuja. 15 Lakini zawadi iliyotolewa bure haiwezi kulinganishwa na ule uasi. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya uasi wa mtu mmoja, basi neema ya Mungu na zawadi iliyotolewa kwa ajili ya mtu mmoja, Yesu Kristo, imemiminika kwa wingi zaidi kwa watu wengi. 16 Pia zawadi ya Mungu sio kama matukio ya ile dhambi ya mtu mmoja. Kwa maana hukumu iliyotokana na uasi huo ilileta laana, lakini zawadi iliyopatikana bure baada ya dhambi nyingi, inaleta haki ya Mungu. 17 Na ikiwa kutokana na uasi wa mtu mmoja kifo kilitawala kupitia huyo mtu mmoja, wale wanaopokea wingi wa neema na zawadi ya bure ya kuhesabiwa haki, watatawala zaidi sana katika maisha kwa ajili ya huyo mtu mmoja, Yesu Kristo. 18 Kwa hiyo, kama vile uasi wa mtu mmoja ulivyoleta hukumu kwa watu wote, hali kadhalika, tendo la haki la mtu mmoja linawafanya watu wote waachiliwe huru na kupewa uzima. 19 Na kama vile ambavyo watu wengi walifanywa kuwa wenye dhambi kwa ajili ya kutokutii kwa mtu mmoja, vivyo hivyo wengi watahesabiwa haki na Mungu kwa ajili ya utii wa mtu mmoja.

20 Sheria ililetwa ili dhambi iongezeke. Lakini dhambi ili poongezeka, neema iliongezeka zaidi. 21 Kama vile ambavyo dhambi ilitawala kwa njia ya kifo, vivyo hivyo neema ya Mungu iweze kutawala kwa njia ya haki, ikileta uzima wa milele katika Yesu

Peace and Hope

Therefore, since we have been justified(A) through faith,(B) we[a] have peace(C) with God through our Lord Jesus Christ,(D) through whom we have gained access(E) by faith into this grace in which we now stand.(F) And we[b] boast in the hope(G) of the glory of God. Not only so, but we[c] also glory in our sufferings,(H) because we know that suffering produces perseverance;(I) perseverance, character; and character, hope. And hope(J) does not put us to shame, because God’s love(K) has been poured out into our hearts through the Holy Spirit,(L) who has been given to us.

You see, at just the right time,(M) when we were still powerless,(N) Christ died for the ungodly.(O) Very rarely will anyone die for a righteous person, though for a good person someone might possibly dare to die. But God demonstrates his own love for us in this: While we were still sinners, Christ died for us.(P)

Since we have now been justified(Q) by his blood,(R) how much more shall we be saved from God’s wrath(S) through him! 10 For if, while we were God’s enemies,(T) we were reconciled(U) to him through the death of his Son, how much more, having been reconciled, shall we be saved through his life!(V) 11 Not only is this so, but we also boast in God through our Lord Jesus Christ, through whom we have now received reconciliation.(W)

Death Through Adam, Life Through Christ

12 Therefore, just as sin entered the world through one man,(X) and death through sin,(Y) and in this way death came to all people, because all sinned(Z)

13 To be sure, sin was in the world before the law was given, but sin is not charged against anyone’s account where there is no law.(AA) 14 Nevertheless, death reigned from the time of Adam to the time of Moses, even over those who did not sin by breaking a command, as did Adam,(AB) who is a pattern of the one to come.(AC)

15 But the gift is not like the trespass. For if the many died by the trespass of the one man,(AD) how much more did God’s grace and the gift that came by the grace of the one man, Jesus Christ,(AE) overflow to the many! 16 Nor can the gift of God be compared with the result of one man’s sin: The judgment followed one sin and brought condemnation, but the gift followed many trespasses and brought justification. 17 For if, by the trespass of the one man, death(AF) reigned through that one man, how much more will those who receive God’s abundant provision of grace and of the gift of righteousness reign in life(AG) through the one man, Jesus Christ!

18 Consequently, just as one trespass resulted in condemnation for all people,(AH) so also one righteous act resulted in justification(AI) and life(AJ) for all people. 19 For just as through the disobedience of the one man(AK) the many were made sinners,(AL) so also through the obedience(AM) of the one man the many will be made righteous.

20 The law was brought in so that the trespass might increase.(AN) But where sin increased, grace increased all the more,(AO) 21 so that, just as sin reigned in death,(AP) so also grace(AQ) might reign through righteousness to bring eternal life(AR) through Jesus Christ our Lord.

Footnotes

  1. Romans 5:1 Many manuscripts let us
  2. Romans 5:2 Or let us
  3. Romans 5:3 Or let us