Huruma Ya Mungu Kwa Waisraeli

11 Kwa hiyo nauliza, je, Mungu amewakataa watu wake? La, sivyo. Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, wa uzao wa Ibrahimu na wa kabila la Benjamini. Mungu hajawakataa watu wake ambao aliwajua tokea mwanzo. Hamfahamu Maandiko yanavyosema kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Waisraeli akisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuziharibu madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua? Na Mungu alimjibuje? “Nime bakiza kwa ajili yangu watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.” Ndivyo ilivyo hata sasa; wapo wachache wal iosalia ambao Mungu amewachagua kwa neema yake. Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, haiwezekani tena wakachaguliwa kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa hivyo, neema isingekuwa neema tena.

Tusemeje basi? Waisraeli walishindwa kupata kile ambacho walikitafutakwa bidii. Lakini waliochaguliwa walikipata. Wa liobaki walifanywa wagumu, kama Maandiko yasemavyo, “Mungu ali wapa mioyo mizito, na macho ambayo hayawezi kuona, na masikio ambayo hayawezi kusikia, hata mpaka leo.” Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, na kitu cha kuwakwaza waanguke na kuadhibiwa, 10 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, na migongo yao ipinde kwa taabu daima.”

Kurejeshwa Kwa Waisraeli

11 Nauliza tena, je, Waisraeli walipojikwaa walianguka na kuangamia kabisa? La sivyo! Lakini kwa sababu ya uhalifu wao, wokovu umewafikia watu wa mataifa mengine, ili Waisraeli waone wivu. 12 Ikiwa uhalifu wao umeleta utajiri mkubwa kwa ulimwe ngu, na kama kuanguka kwao kumeleta utajiri kwa watu wasiomjua Mungu, basi Waisraeli wote watakapoongoka itakuwa ni baraka kub wa zaidi.

13 Sasa ninasema nanyi watu wa mataifa mengine. Mimi ni mtume kwa watu wa mataifa na ninajivunia huduma hiyo 14 ili kuwafanya Wayahudi wenzangu waone wivu, na hivyo niwaokoe baadhi yao. 15 Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao kumefanya ulimwengu wote upatanishwe na Mungu, kuokolewa kwao je, si kutakuwa ni uhai kutoka kwa wafu? 16 Na kama sehemu ya kwanza ya unga ulioumuliwa ni wakfu, basi unga wote ni wakfu; na kama shina ni wakfu, matawi nayo yatakuwa wakfu.

17 Lakini kama baadhi ya matawi yamekatwa, na ninyi kama mizeituni mwitu mkapandwa katika shina, mkashiriki pamoja na matawi mengine chakula kutoka katika shina la mzeituni, 18 msi jivune mbele ya hayo matawi. Kama mkijisifu mkumbuke kuwa si ninyi mnaoshikilia shina, bali ni shina linalowashikilia ninyi. 19 Pengine mtasema, “Matawi yalikatwa ili nipate nafasi ya kupandikizwa katika shina.” 20 Hii ni kweli. Lakini kumbuka kuwa matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini; na wewe umesimama imara kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijisifu, bali ujinyenyekeze na kuogopa. 21 Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, hatakuacha wewe, atakuondoa. 22 Tafakari basi kuhusu wema na ukali wa Mungu. Yeye ni mkali kwa wale walio anguka, bali amekuonyesha wewe wema wake, kama utadumu katika wema wake. Vinginevyo, na wewe utakatiliwa mbali. 23 Na hata hao Waisraeli, kama wakiacha kudumu katika kutokuamini kwao, atawar udisha kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwarejesha. 24 Ikiwa ninyi mmekatwa kutoka katika mizeituni mwitu, na ki nyume cha asilia mkapandikizwa kwenye mzeituni uliopandwa, ita kuwa ni rahisi kiasi gani matawi haya ya asili kurejeshwa kwenye shina lake?

Huruma Ya Mungu Ni Kwa Wote

25 Ndugu zangu, napenda mfahamu siri hii, msije mkaanza kujiona. Waisraeli wamekuwa na mioyo migumu kwa kiasi fulani mpaka idadi kamili ya watu wa mataifa mengine watakapoamini. 26 Na ndipo Waisrael wote wataokoka kama ilivyoandikwa, “Mko mbozi atakuja kutoka Sayuni, na kuuondoa uasi wote kutoka katika uzao wa Yakobo. 27 Na hii itakuwa ni agano langu nao, nitakapoondoa dhambi zao.”

28 Basi Waisraeli ni maadui wa Mungu kwa sababu ya Injili. Hii ni kwa faida yenu. Lakini kuhusu uchaguzi, Waisraeli bado ni wapendwa wa Mungu kwa sababu ya ahadi yake kwa Abrahmu, Isaki na Yakobo. 29 Kwa maana karama za Mungu na wito wake hazifutiki. 30 Kama ninyi zamani mlivyokuwa mmemwasi Mungu na sasa mmepokea rehema kwa sababu ya kutokutii kwao, 31 hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi kwa ajili ya rehema mliyopata kutoka kwa Mungu, ili wao pia wapate rehema. 32 Kwa maana Mungu amewaachia wana damu wote wawe katika uasi, ili aweze kuwahurumia wote.

Wimbo Wa Shukrani

33 Jinsi utajiri wa Mungu ulivyo mkuu! Hekima yake na maarifa yake hayana mwisho. Njia zake na maamuzi yake hayachu nguziki! 34 Kwa maana ni nani amepata kufahamu mawazo ya Mungu au kuwa mshauri wake? 35 Au ni nani amewahi kumpa cho chote ili arudishiwe? 36 Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake na vipo kwa ajili yake na vyote vinadumu kwake. Utukufu ni wake milele. Amina.

Mungu Hajawakataa Watu wake

11 Hivyo ninauliza, “Je, Mungu aliwakataa watu wake?” Hapana! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, wa ukoo wa Ibrahimu, katika kabila la Benjamini. Mungu aliwachagua Waisraeli wawe watu wake kabla hawajazaliwa. Na hajawakataa. Hakika mnajua Maandiko yanavyosema kuhusu Eliya anapomwomba Mungu dhidi ya watu wa Israeli. Anasema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuharibu madhabahu zako. Mimi ndiye nabii pekee niliyebaki hai, na sasa wanajaribu kuniua mimi pia.”(A) Lakini ni jibu gani Mungu alilompa Eliya? Mungu alisema, “Nimejihifadhia watu elfu saba wasiomwabudu Baali.”(B)

Ndivyo ilivyo sasa. Mungu amewachagua watu wachache kwa neema yake. Na kama aliwachagua kwa neema yake, hivyo si kwa sababu ya matendo yao yaliyowafanya wawe watu wake. Kama wangefanywa kuwa watu wake kutokana na matendo yao, zawadi yake ya neema isingekuwa zawadi halisi.

Hivyo hivi ndivyo ilivyotokea: Watu wa Israeli wanazitaka sana baraka za Mungu, lakini si wote waliozipata. Watu aliowachagua walipata baraka zake, lakini wengine wakawa wagumu na wakakataa kumsikiliza. Kama Maandiko yanavyosema,

“Mungu aliwafanya watu walale usingizi.”(C)
“Mungu aliyafumba macho yao ili wasione,
    na aliyaziba masikio yao ili wasisikie.
Hili linaendelea hata sasa.”(D)

Na Daudi anasema,

“Watu hawa na wakamatwe na kunaswa
    katika tafrija wanazofurahia.
Nyakati hizo nzuri ziwasababishe waanguke
    ili wapate adhabu wanayoistahili.
10 Yapofushe macho yao ili wasiweze kuona.
    Ipindishe migongo yao kwa mzigo wa matatizo.”(E)

11 Hivyo nauliza: Pale watu wa Mungu walipojikwaa na kuanguka, Je, hawakuweza kuinuka tena? Hakika hapana! Lakini kujikwaa kwao katika mwendo kulileta wokovu kwa wale wasio Wayahudi. Kusudi la hili lilikuwa kuwafanya Wayahudi wapate wivu. 12 Kosa lao na hasara yao vilileta baraka za utajiri kwa ulimwengu kwa wasio Wayahudi. Hivyo fikirini ni kwa kiasi gani baraka hizi zitakuwa kubwa kwa ulimwengu pale idadi ya kutosha ya Wayahudi watakapokuwa watu wa aina ile anayoitaka Mungu.

13 Nasema na ninyi watu msio Wayahudi. Kwa vile mimi ndiye ambaye Mungu ameniteua niwe mtume kwa wale wasio Wayahudi, nitafanya kwa bidii yote kuiheshimu huduma hii. 14 Natarajia kuwafanya watu wangu wawe na wivu. Kwa njia hiyo, labda naweza kuwasaidia baadhi yao waweze kuokolewa. 15 Mungu aliwaacha kwa muda. Hilo lilipotokea, akawa rafiki wa watu wengine ulimwenguni. Hivyo anapowakubali Wayahudi, ni sawa na kuwafufua watu baada ya kifo. 16 Kama sehemu ya kwanza ya mkate inatolewa kwa Mungu, basi mkate mzima unakuwa umetakaswa. Kama mizizi ya mti ni mitakatifu, matawi ya mti huo pia ni matakatifu.

17 Ni kama vile baadhi ya matawi ya mzeituni yamevunjwa, na tawi la mzeituni mwitu limeunganishwa katika ule mti wa kwanza. Ikiwa wewe si Myahudi, uko sawa na tawi la mzeituni mwitu, na sasa unashiriki nguvu na uhai wa mti wa kwanza. 18 Lakini msienende kama mlio bora kuliko matawi yale yaliyovunjwa. Hamna sababu ya kujivuna, kwa sababu hamleti uhai katika mzizi. Mzizi ndiyo huleta uhai kwenu. 19 Mnaweza kusema, “Matawi yalivunjwa ili niweze kuunganishwa katika mti wake.” 20 Hiyo ni kweli. Lakini matawi hayo yalivunjwa kwa sababu hayakuamini. Na mnaendelea kuwa sehemu ya mti kwa sababu tu mnaamini. Msijivune, bali muwe na hofu. 21 Ikiwa Mungu hakuyaacha matawi ya asili ya mti huo yawepo, hataweza kuwaacha ninyi muwepo mtakapoacha kuamini.

22 Hivyo mnaona kwamba Mungu yu mwema, lakini anaweza pia kuwa mkali. Huwaadhibu wale wanaoacha kumfuata. Lakini ni mwema kwenu ikiwa mtaendelea kumwamini katika wema wake. Kama hamtaendelea kumtegemea yeye, mtakatwa kutoka katika mti. 23 Na kama Wayahudi watamwamini Mungu tena, yeye atawapokea tena. Ana uwezo wa kuwarudisha pale walipokuwa. 24 Kwa asili, tawi la mzabibu mwitu haliwezi kuwa sehemu ya mti mzuri. Lakini ninyi msio Wayahudi ni kama tawi lililovunjwa kutoka katika mzeituni pori. Na mliunganishwa na mti wa mzeituni ulio mzuri. Lakini Wayahudi ni kama matawi yaliyostawi kutokana na mti mzuri. Hivyo kwa hakika yanaweza kuunganishwa pamoja katika mti wao tena.

25 Ndugu zangu, ieleweni siri hii ya ukweli. Kweli hii itawasaidia ninyi mjue kuwa hamfahamu kila kitu. Kweli ni hii: Sehemu ya Israeli wamefanywa kuwa wakaidi, lakini hiyo itabadilika wasio Wayahudi, wengi, watakapokuja kwa Mungu. 26 Na hivyo ndivyo Israeli wote watakavyookolewa. Kama Maandiko yanavyosema,

“Mwokozi atakuja kutoka Sayuni;
    atauondoa uovu kutoka kwa wazaliwa wa Yakobo.
27 Nami nitalifanya patano hili na watu wale
    nitakapoziondoa dhambi zao.”(F)

28 Kwa sasa, Wayahudi wanaokataa kuzipokea Habari Njema wamekuwa adui wa Habari Njema. Hili limetokea kwa manufaa yenu ninyi msio Wayahudi. Lakini bado Wayahudi ni wateule wa Mungu, na anawapenda kwa sababu ya ahadi alizozifanya kwa baba zao. 29 Mungu habadili mawazo yake kuhusu watu anaowaita. Kamwe haamui kuzirudisha baraka alizokwisha kuwapa. 30 Wakati mmoja ninyi pia mlikataa kumtii Mungu. Lakini sasa mmeipokea rehema, kwa sababu Wayahudi walikataa kutii. 31 Na sasa wao ndiyo wanaokataa kutii, kwa sababu Mungu aliwaonesha ninyi rehema zake. Lakini hili limetokea ili nao pia waweze kupokea rehema kutoka kwake. 32 Mungu amemfungia kila mmoja katika gereza la kutokutii. Lakini amefanya hivi ili aweze kuonesha rehema yake kwa wote.

Sifa kwa Mungu

33 Ndiyo, utajiri wa Mungu ni mkuu sana! Hekima yake na ufahamu wake havina mwisho! Hakuna awezaye kuelezea yale Mungu anayoyaamua. Hayupo awezaye kuzielewa njia zake. 34 Kama Maandiko yanavyosema,

“Nani anaweza kuyajua yaliyo katika mawazo ya Bwana?
    Nani anaweza kumshauri?”(G)
35 “Nani amewahi kumpa Mungu kitu chochote?
    Mungu hadaiwi kitu chochote na mtu yeyote.”(H)

36 Ndiyo, Mungu ameviumba vitu vyote. Na kila kitu kinaendelea kuwepo kwa njia na kwa ajili yake. Utukufu uwe kwa Mungu milele yote! Amina.