Kristo alituweka sisi huru ili tuwe na uhuru. Kwa hiyo simameni imara wala msikubali tena kulemewa na minyororo ya utumwa. Sikilizeni! Mimi Paulo nawaambieni kwamba kama mkiku bali kutahiriwa, basi Kristo hatawafaidia cho chote. Tena, napenda kumshuhudia kila mmoja wenu anayekubali kutahiriwa kwamba inampasa kushika sheria zote. Ninyi mnaotafuta kuhesabiwa haki kwa njia ya sheria fahamuni kwamba mmetengwa na Kristo, mko mbali na neema ya Mungu. Kwa maana, kwa msaada wa Roho wa Mungu, sisi tunangojea kwa matumaini kupata haki kwa njia ya imani. Kwa maana tukiwa ndani ya Kristo, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuleti faida yo yote, bali jambo la msingi ni kuwa na imani inayofanya kazi kwa upendo.

Mlikuwa mkienenda vizuri, sasa ni nani aliyewazuia msiitii kweli? Kushawishiwa huku hakutokani na yule anayewaita. Hamira kidogo sana inaweza kuchachusha donge zima. 10 Nina hakika katika Bwana kwamba mtakubaliana na msimamo wangu. Huyo anayewasumbueni atapata hukumu anayostahili hata akiwa nani. 11 Lakini ndugu zangu, kama mimi ninahubiri kwamba kutahiriwa ni lazima, kwa nini bado nateswa? Ingekuwa hivyo, mahubiri yangu juu ya msalaba wa Kristo yasingekuwa kikwazo tena. 12 Laiti hao wanaowavurugeni wangejikatakata wenyewe!

13 Ndugu zangu, ninyi mliitwa ili muwe watu huru. Hata hivyo msitumie uhuru wenu kuendelea kufuata tamaa za mwili, bali tumi kianeni ninyi kwa ninyi kwa upendo. 14 Kwa maana sheria yote hukamilika katika amri moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” 15 Lakini ikiwa mtaumana na kutafunana, basi jihadhar ini, msije mkaangamizana wenyewe kwa wenyewe.

Maisha Ya Kiroho

16 Kwa hiyo nasema, mruhusuni Roho atawale maisha yenu na msitafute kutimiza tamaa za mwili. 17 Kwa maana tamaa za mwili hushindana na Roho; na Roho hushindana na tamaa za mwili. Roho na mwili hupingana, na kwa sababu hiyo ninyi hamwezi kufanya yale mnayotaka. 18 Lakini kama mkiongozwa na Roho, hamko tena chini ya sheria.

19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri nayo ni haya: uasherati, uchafu, ufisadi, 20 kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, mafarakano, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine yanayofanana na hayo. Nawaonya, kama nilivyokwisha waonya kabla, kwamba watu watendao mambo kama haya, hawataurithi Ufalme wa Mungu. 22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumili vu, wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi. Hakuna sheria inayopinga mambo kama haya.

24 Wote walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na tamaa zake. 25 Kwa kuwa tunaishi kwa kuongozwa na Roho wa Mungu, basi tufuate uongozi wake. 26 Tusiwe watu wenye maji vuno, tusichokozane na wala tusioneane wivu. Kuchukuliana Mizigo

Stand fast therefore in the liberty wherewith Christ hath made us free, and be not entangled again with the yoke of bondage.

Behold, I Paul say unto you, that if ye be circumcised, Christ shall profit you nothing.

For I testify again to every man that is circumcised, that he is a debtor to do the whole law.

Christ is become of no effect unto you, whosoever of you are justified by the law; ye are fallen from grace.

For we through the Spirit wait for the hope of righteousness by faith.

For in Jesus Christ neither circumcision availeth any thing, nor uncircumcision; but faith which worketh by love.

Ye did run well; who did hinder you that ye should not obey the truth?

This persuasion cometh not of him that calleth you.

A little leaven leaveneth the whole lump.

10 I have confidence in you through the Lord, that ye will be none otherwise minded: but he that troubleth you shall bear his judgment, whosoever he be.

11 And I, brethren, if I yet preach circumcision, why do I yet suffer persecution? then is the offence of the cross ceased.

12 I would they were even cut off which trouble you.

13 For, brethren, ye have been called unto liberty; only use not liberty for an occasion to the flesh, but by love serve one another.

14 For all the law is fulfilled in one word, even in this; Thou shalt love thy neighbour as thyself.

15 But if ye bite and devour one another, take heed that ye be not consumed one of another.

16 This I say then, Walk in the Spirit, and ye shall not fulfil the lust of the flesh.

17 For the flesh lusteth against the Spirit, and the Spirit against the flesh: and these are contrary the one to the other: so that ye cannot do the things that ye would.

18 But if ye be led of the Spirit, ye are not under the law.

19 Now the works of the flesh are manifest, which are these; Adultery, fornication, uncleanness, lasciviousness,

20 Idolatry, witchcraft, hatred, variance, emulations, wrath, strife, seditions, heresies,

21 Envyings, murders, drunkenness, revellings, and such like: of the which I tell you before, as I have also told you in time past, that they which do such things shall not inherit the kingdom of God.

22 But the fruit of the Spirit is love, joy, peace, longsuffering, gentleness, goodness, faith,

23 Meekness, temperance: against such there is no law.

24 And they that are Christ's have crucified the flesh with the affections and lusts.

25 If we live in the Spirit, let us also walk in the Spirit.

26 Let us not be desirous of vain glory, provoking one another, envying one another.