Nanyi aliwafanya muwe hai, mlipokuwa mmekufa kiroho kwa ajili ya makosa na dhambi zenu. Hapo zamani mliishi maisha ya jinsi hiyo, mkimtii mfalme wa nguvu za anga, ambaye ndiye ile roho inayowatawala wote wanaomwasi Mungu. Sisi sote pia tuliishi miongoni mwao hapo zamani, tukiridhisha na kutawaliwa na tamaa mbaya za mwili na mawazo. Kwa hiyo sisi pia tulikuwa kwa asili tunastahili ghadhabu ya Mungu kama binadamu wengine wote. Lakini Mungu, ambaye ana huruma nyingi, kutokana na upendo wake mkuu ambao alitupenda nao, japokuwa tulikuwa bado tumekufa kiroho kwa sababu ya makosa yetu, alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo Yesu. Mmeokolewa kwa neema. Mungu alitufufua pamoja na Kristo, akatufanya tukae pamoja naye katika makao ya mbinguni tukiwa ndani yake Kristo; ili katika vizazi vijavyo aonyeshe wingi wa neema yake isiyo na mfano, ambayo imedhihirishwa kwa wema wake kwetu sisi tunaoishi ndani ya Kristo Yesu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; na si kwa sababu ya matendo yenu mema. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu mwenyewe. Na kwa sababu hamkuifanyia kazi, mtu ye yote asije akajisifu juu ya wokovu wake. 10 Kwa maana sisi ni matokeo ya kazi ya Mungu tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tuwe na matendo mema ambayo Mungu alikwisha andaa, tuishi katika hayo. 11 Kwa hiyo kumbukeni kwamba ninyi ambao kwa asili ni watu wa mataifa mengine, mnaoitwa ‘wasiotahiriwa’ na wale ‘waliotahi riwa’ kwa kanuni za binadamu; 12 kumbukeni kwamba wakati ule ninyi mlikuwa mmetengwa na Kristo, mkiwa mmefarakana na jumuia ya Israeli na mkiwa wageni kuhusu yale maagano ya ahadi. Mlikuwa hamna matumaini wala Mungu duniani. 13 Lakini kwa kuwa mmeungana na Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali zamani, sasa mmeletwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo. 14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu; yeye aliyetufanya tuwe jamii moja, akavunjavunja ule ukuta wa uadui uliotutenga 15 kwa kuifuta ile sheria na amri zake na kan uni zake alipoutoa mwili wake. Alifanya hivyo ili aumbe taifa jipya kutokana na jamii mbili: Wayahudi na watu wa mataifa, na hivyo alete amani. 16 Kwa kutoa mwili wake pale msalabani, ali patanisha jamii zote mbili na Mungu; na kwa njia hiyo akaua ule uadui uliokuwepo kati yao. 17 Alikuja akahubiri amani kwenu ninyi watu wa mataifa ambao mlikuwa mbali na Mungu, na pia kwa wale waliokuwa karibu na Mungu. 18 Kwa maana, kwa kupitia kwake, sisi sote, Wayahudi na watu wa mataifa, tunaweza kumkaribia Baba katika Roho mmoja. 19 Kwa hiyo, ninyi sasa siyo wageni tena wala wapita njia, bali mmekuwa raia halisi pamoja na watu wa Mungu na familia ya Mungu. 20 Ninyi mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, na Kristo Yesu mwenyewe ndiye jiwe kuu la pembeni. 21 Ndani yake yeye, jengo lote limeunganishwa pamoja na kusimam ishwa kuwa Hekalu takatifu la Mungu. 22 Katika yeye ninyi pia mnajengwa pamoja ili mpate kuwa makao ambamo Mungu anaishi kwa njia ya Roho wake. Paulo, Mhudumu Kwa Watu Wa Mataifa

And you hath he quickened, who were dead in trespasses and sins;

Wherein in time past ye walked according to the course of this world, according to the prince of the power of the air, the spirit that now worketh in the children of disobedience:

Among whom also we all had our conversation in times past in the lusts of our flesh, fulfilling the desires of the flesh and of the mind; and were by nature the children of wrath, even as others.

But God, who is rich in mercy, for his great love wherewith he loved us,

Even when we were dead in sins, hath quickened us together with Christ, (by grace ye are saved;)

And hath raised us up together, and made us sit together in heavenly places in Christ Jesus:

That in the ages to come he might shew the exceeding riches of his grace in his kindness toward us through Christ Jesus.

For by grace are ye saved through faith; and that not of yourselves: it is the gift of God:

Not of works, lest any man should boast.

10 For we are his workmanship, created in Christ Jesus unto good works, which God hath before ordained that we should walk in them.

11 Wherefore remember, that ye being in time past Gentiles in the flesh, who are called Uncircumcision by that which is called the Circumcision in the flesh made by hands;

12 That at that time ye were without Christ, being aliens from the commonwealth of Israel, and strangers from the covenants of promise, having no hope, and without God in the world:

13 But now in Christ Jesus ye who sometimes were far off are made nigh by the blood of Christ.

14 For he is our peace, who hath made both one, and hath broken down the middle wall of partition between us;

15 Having abolished in his flesh the enmity, even the law of commandments contained in ordinances; for to make in himself of twain one new man, so making peace;

16 And that he might reconcile both unto God in one body by the cross, having slain the enmity thereby:

17 And came and preached peace to you which were afar off, and to them that were nigh.

18 For through him we both have access by one Spirit unto the Father.

19 Now therefore ye are no more strangers and foreigners, but fellowcitizens with the saints, and of the household of God;

20 And are built upon the foundation of the apostles and prophets, Jesus Christ himself being the chief corner stone;

21 In whom all the building fitly framed together groweth unto an holy temple in the Lord:

22 In whom ye also are builded together for an habitation of God through the Spirit.