Yesu Ni Mkuu Kuliko Musa

Kwa hiyo, ndugu zangu watakatifu, ambao mmeshiriki wito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na kuhani mkuu wa imani tunay oikiri.

Kwa maana Yesu alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemchagua, kama vile Musa alivyokuwa mwaminifu katika nyumba ya Mungu. Lakini Yesu amehesabiwa kuwa anastahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile mjenzi wa nyumba anavyopewa heshima zaidi kuliko nyumba aliyoijenga. Maana kila nyumba hujengwa na mtu fulani bali aliyejenga vitu vyote ni Mungu. Ni kweli kwamba Musa ali kuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, akishu hudia juu ya yale mambo ambayo Mungu angeyatamka baadaye, lakini Kristo alikuwa mwaminifu katika nyumba ya Mungu kama mwana. Na sisi ni nyumba yake, ikiwa tutashikilia ujasiri wetu na lile tumaini tunalojivunia.

Jihadharini Na Kutokuamini

Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama mlivyofanya wakati wa uasi , siku ile ya majaribio jangwani, ambapo baba zenu walinijaribu wakaona kazi zangu kwa miaka arobaini. 10 Kwa hiyo kizazi kile kilinikasirisha, nikasema, ‘Mioyo ya watu hao imepotoka; hawajapata kujua njia zangu.’ 11 Katika hasira yangu nikaapa, ‘Hawataingia kwenye pumziko langu kamwe.’

12 Angalieni, ndugu zangu, asiwepo miongoni mwenu mtu ye yote mwenye moyo wa dhambi, usioamini, unaomfanya ajitenge na Mungu wa uzima. 13 Bali muonyane kila siku maadamu bado ni ‘ ‘leo” ili asiwepo mtu kati yenu anayefanywa mkaidi na udangany ifu wa dhambi. 14 Kwa maana sisi ni washiriki pamoja na Kristo iwapo tutashikilia tumaini letu la kwanza kwa uaminifu mpaka mwisho. 15 Kama Maandiko yalivyosema: “Leo mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu. Kama mlivyofanya wakati wa uasi.” 16 Ni nani hao waliosikia lakini wakaasi? Si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Musa? 17 Na ni nani waliom kasirisha Mungu kwa miaka arobaini? Si wale waliofanya dhambi wakafa jangwani? 18 Na ni nani ambao Mungu aliapa kuwa hawatain gia kwenye pumziko lake, isipokuwa wale waliokataa kutii? 19 Kwa hiyo tunaona kwamba walishindwa kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao. Pumziko La Sabato

Jesus Greater Than Moses

Therefore, holy brothers and sisters,(A) who share in the heavenly calling,(B) fix your thoughts on Jesus, whom we acknowledge(C) as our apostle and high priest.(D) He was faithful to the one who appointed him, just as Moses was faithful in all God’s house.(E) Jesus has been found worthy of greater honor than Moses,(F) just as the builder of a house has greater honor than the house itself. For every house is built by someone, but God is the builder of everything.(G) “Moses was faithful as a servant(H) in all God’s house,”[a](I) bearing witness to what would be spoken by God in the future. But Christ is faithful as the Son(J) over God’s house. And we are his house,(K) if indeed we hold firmly(L) to our confidence and the hope(M) in which we glory.

Warning Against Unbelief

So, as the Holy Spirit says:(N)

“Today, if you hear his voice,
    do not harden your hearts(O)
as you did in the rebellion,
    during the time of testing in the wilderness,
where your ancestors tested and tried me,
    though for forty years they saw what I did.(P)
10 That is why I was angry with that generation;
    I said, ‘Their hearts are always going astray,
    and they have not known my ways.’
11 So I declared on oath in my anger,(Q)
    ‘They shall never enter my rest.’ (R)[b](S)

12 See to it, brothers and sisters, that none of you has a sinful, unbelieving heart that turns away from the living God.(T) 13 But encourage one another daily,(U) as long as it is called “Today,” so that none of you may be hardened by sin’s deceitfulness.(V) 14 We have come to share in Christ, if indeed we hold(W) our original conviction firmly to the very end.(X) 15 As has just been said:

“Today, if you hear his voice,
    do not harden your hearts
    as you did in the rebellion.”[c](Y)

16 Who were they who heard and rebelled? Were they not all those Moses led out of Egypt?(Z) 17 And with whom was he angry for forty years? Was it not with those who sinned, whose bodies perished in the wilderness?(AA) 18 And to whom did God swear that they would never enter his rest(AB) if not to those who disobeyed?(AC) 19 So we see that they were not able to enter, because of their unbelief.(AD)

Footnotes

  1. Hebrews 3:5 Num. 12:7
  2. Hebrews 3:11 Psalm 95:7-11
  3. Hebrews 3:15 Psalm 95:7,8