Muhuri Wa Saba

Mwana-Kondoo alipofungua muhuri wa saba, mbinguni palikuwa kimya kwa muda upatao nusu saa hivi. Kisha nikawaona wale mal aika saba wanaosimama mbele za Mungu, nao wakapewa tarumbeta saba.

Malaika mwingine aliyekuwa na chetezo cha dhahabu, alikuja akasimama mbele ya madhabahu. Akapewa ubani mwingi auchanganye pamoja na sala za watu wote wa Mungu, kwenye madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kile kiti cha enzi. Ule moshi wa ubani ukapanda juu mbele za Mungu, pamoja na maombi ya watu wa Mungu , kutoka mkononi mwa huyo malaika. Halafu yule malaika akachukua kile chetezo akakijaza moto kutoka kwenye ile madhabahu akautupa juu ya nchi. Pakatokea radi, ngurumo, umeme na tetemeko la nchi.

Tarumbeta Za Kwanza Nne

Kisha wale malaika saba waliokuwa na tarumbeta saba waka jiandaa kuzipiga. Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake, pakatokea mvua ya mawe na moto uliochanganyika na damu, ikanyesha kwa nguvu juu ya nchi; na theluthi moja ya nchi ikateketea, na theluthi moja ya miti ikateketea na majani yote mabichi yakateke tea.

Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto kikatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikageuka kuwa damu, theluthi moja ya viumbe hai waishio bahar ini wakafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.

10 Malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake, na nyota kubwa iliyokuwa ikiwaka kama taa ilianguka kutoka angani, ikaangukia theluthi moja ya mito na chemchemi za maji. 11 Nyota hiyo inaitwa “Uchungu”. Theluthi moja ya maji yakawa machungu, na watu wengi walikufa kutokana na maji hayo kwa maana yalikuwa machungu.

12 Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta, na theluthi moja ya jua, theluthi moja ya mwezi na theluthi moja ya nyota, zika pigwa. Kwa hiyo theluthi moja ya mwanga wao ukawa giza. Theluthi moja ya mchana ilikuwa haina mwanga na pia theluthi moja ya usiku.

13 Halafu tena nikatazama, nikasikia tai mmoja akipiga kelele kwa sauti kuu wakati akiruka katikati ya mbingu, “Ole wao! Ole wao! Ole wao watu waishio duniani wakati itakaposikika milio ya tarumbeta ambazo karibuni zitapigwa na malaika watatu waliobakia.”

The Seventh Seal and the Golden Censer

When he opened the seventh seal,(A) there was silence in heaven for about half an hour.

And I saw the seven angels(B) who stand before God, and seven trumpets were given to them.(C)

Another angel,(D) who had a golden censer, came and stood at the altar. He was given much incense to offer, with the prayers of all God’s people,(E) on the golden altar(F) in front of the throne. The smoke of the incense, together with the prayers of God’s people, went up before God(G) from the angel’s hand. Then the angel took the censer, filled it with fire from the altar,(H) and hurled it on the earth; and there came peals of thunder,(I) rumblings, flashes of lightning and an earthquake.(J)

The Trumpets

Then the seven angels who had the seven trumpets(K) prepared to sound them.

The first angel(L) sounded his trumpet, and there came hail and fire(M) mixed with blood, and it was hurled down on the earth. A third(N) of the earth was burned up, a third of the trees were burned up, and all the green grass was burned up.(O)

The second angel sounded his trumpet, and something like a huge mountain,(P) all ablaze, was thrown into the sea. A third(Q) of the sea turned into blood,(R) a third(S) of the living creatures in the sea died, and a third of the ships were destroyed.

10 The third angel sounded his trumpet, and a great star, blazing like a torch, fell from the sky(T) on a third of the rivers and on the springs of water(U) 11 the name of the star is Wormwood.[a] A third(V) of the waters turned bitter, and many people died from the waters that had become bitter.(W)

12 The fourth angel sounded his trumpet, and a third of the sun was struck, a third of the moon, and a third of the stars, so that a third(X) of them turned dark.(Y) A third of the day was without light, and also a third of the night.(Z)

13 As I watched, I heard an eagle that was flying in midair(AA) call out in a loud voice: “Woe! Woe! Woe(AB) to the inhabitants of the earth,(AC) because of the trumpet blasts about to be sounded by the other three angels!”

Footnotes

  1. Revelation 8:11 Wormwood is a bitter substance.