Kiti Cha Enzi Kilichoko Mbinguni

Baada ya hayo nilitazama, nikaona mlango ulio wazi mbin guni. Na ile sauti niliyokuwa nimeisikia ikisema nami kama tar umbeta ikasema, “Njoo huku juu nami nitakuonyesha yatakayotokea baada ya haya. ” Ghafla nilikuwa katika Roho, na mbele yangu kilikuwapo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa. Aliyeketi kwenye kiti hicho cha enzi alionekana kama jiwe zuri jekundu na akiki, na upinde wa mvua ulizunguka kile kiti cha enzi, ukione kana kama zumaridi. Kiti hicho kilizungukwa na viti vingine ishirini na vinne vya enzi ambavyo juu yake walikaa wazee ishi rini na wanne waliokuwa wamevalia mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani. Na katika kile kiti cha enzi kulitoka umeme, ngurumo na sauti. Taa saba za moto zilikuwa zinawaka mbele ya kile kiti cha enzi, ambazo ni zile roho saba za Mungu. Mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na kitu kinachofanana na bahari ya kioo iking’aa kama jiwe la kioo. Katikati, kuzunguka kile kiti cha enzi, walikuwapo viumbe hai wanne, wenye macho kila mahali, mbele na nyuma.

Kiumbe hai wa kwanza alifanana na simba, wa pili alifanana na ng’ombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, wa nne alifanana na tai arukaye. Na hawa viumbe hai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita na macho kila mahali, hata chini ya mabawa. Usiku na mchana hawakuacha kuimba, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako, aliyeko na atakayekuja.”

Kila mara viumbe hao wanne walipomtukuza na kumheshimu na kumshukuru yeye aliyeketi kwenye kiti cha enzi na aishie milele na milele, 10 wale wazee ishirini na wanne walianguka mbele zake yeye aliyeketi kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Wakaziweka taji zao mbele ya kile kiti cha enzi wakisema, 11 “Bwana wetu na Mungu wetu, wewe umestahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ni wewe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako vitu vyote viliumbwa na vinapata kuwapo.”

The Throne in Heaven

After this I looked, and there before me was a door standing open(A) in heaven. And the voice I had first heard speaking to me like a trumpet(B) said, “Come up here,(C) and I will show you what must take place after this.”(D) At once I was in the Spirit,(E) and there before me was a throne in heaven(F) with someone sitting on it. And the one who sat there had the appearance of jasper(G) and ruby.(H) A rainbow(I) that shone like an emerald(J) encircled the throne. Surrounding the throne were twenty-four other thrones, and seated on them were twenty-four elders.(K) They were dressed in white(L) and had crowns of gold on their heads. From the throne came flashes of lightning, rumblings and peals of thunder.(M) In front of the throne, seven lamps(N) were blazing. These are the seven spirits[a](O) of God. Also in front of the throne there was what looked like a sea of glass,(P) clear as crystal.

In the center, around the throne, were four living creatures,(Q) and they were covered with eyes, in front and in back.(R) The first living creature was like a lion, the second was like an ox, the third had a face like a man, the fourth was like a flying eagle.(S) Each of the four living creatures(T) had six wings(U) and was covered with eyes all around,(V) even under its wings. Day and night(W) they never stop saying:

“‘Holy, holy, holy

is the Lord God Almighty,’[b](X)

who was, and is, and is to come.”(Y)

Whenever the living creatures give glory, honor and thanks to him who sits on the throne(Z) and who lives for ever and ever,(AA) 10 the twenty-four elders(AB) fall down before him(AC) who sits on the throne(AD) and worship him who lives for ever and ever. They lay their crowns before the throne and say:

11 “You are worthy, our Lord and God,
    to receive glory and honor and power,(AE)
for you created all things,
    and by your will they were created
    and have their being.”(AF)

Footnotes

  1. Revelation 4:5 That is, the sevenfold Spirit
  2. Revelation 4:8 Isaiah 6:3