Mnyama Kutoka Baharini

13 Kisha nikaona mnyama akitoka baharini. Alikuwa na pembe kumi na vichwa saba na taji kumi kwenye pembe zake. Na kila kichwa kiliandikwa jina la kufuru. Huyo mnyama alifanana kama chui lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kama cha simba. Lile joka lilimpa mnyama huyo nguvu zake, kiti chake cha enzi na uwezo mkuu. Kichwa kimoja cha huyo mnyama kilione kana kama kilikwisha kuwa na jeraha lisiloweza kupona, lakini jeraha hilo lilikuwa limepona na dunia nzima ilimstaajabia huyo mnyama na kumfuata. Watu waliliabudu lile joka kwa sababu lili kuwa limempa huyo mnyama uwezo wake. Pia walimwabudu huyo mnyama wakisema, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana naye?”

Kisha huyo mnyama akaruhusiwa kusema maneno ya kujisifu na ya kufuru na akapewa haki ya kutawala kwa muda wa miezi arobaini na miwili. Alisema maneno ya kumkufuru Mungu, akilitukana jina lake na mahali aishipo, yaani, aliwatukana wale waishio mbinguni. Pia aliruhusiwa kuwapiga vita watu wa Mungu na kuwashinda. Alipewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, kila ukoo, kila lugha na taifa. Na watu wote waishio duniani watamwabudu, yaani kila mmoja ambaye tangu kabla ya ulimwengu kuumbwa, jina lake haliku andikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.

“Aliye na nia ya kusikia, asikilize kwa makini: 10 Ye yote aliyepangiwa kuchukuliwa mateka atatekwa. Mtu ye yote akiua kwa upanga atauawa kwa upanga. Na hii ndio nafasi ya watu wa

Mnyama Kutoka Ardhini

11 Kisha nikamwona mnyama mwingine akipanda juu kutoka katika ardhi. Alikuwa na pembe mbili kama za mwana kondoo lakini aliongea kama joka. 12 Naye alitumia uwezo wote wa yule mnyama wa kwanza aliyemtangulia. Akalazimisha dunia yote na wote waliomo duniani wamwabudu huyo mnyama wa kwanza aliyekuwa na jeraha la kifo lililokuwa limepona. 13 Huyu mnyama wa pili akafanya miu jiza ya ajabu hata kufanya moto utoke mbinguni na kushuka duniani mbele ya watu. 14 Kwa njia ya miujiza aliyowezeshwa kufanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, aliwadanganya watu waishio duniani. Aliwaamuru watengeneze sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 15 Kisha akawe zeshwa kuipatia pumzi ile sanamu ya mnyama wa kwanza hata ikaweza kuongea na kufanya wale wote ambao hawakuiabudu wauawe. 16 Pia aliwalazimisha watu wote, wakubwa kwa wadogo, matajiri na mas kini, watu huru na watumwa, watiwe alama kwenye mikono yao ya kulia au kwenye vipaji vya nyuso zao. 17 Hakuna mtu ye yote ambaye angeweza kununua au kuuza kitu kama hana alama ile, yaani jina la huyo mnyama au namba ya jina lake.

18 Jambo hili linahitaji hekima. Mwenye akili ya kutambua apige hesabu ya mnyama huyo kwa sababu ni namba ya mtu. Namba yake ni mia sita sitini na sita.

Mnyama kutoka Baharini

13 Kisha niliona mnyama mwenye pembe kumi na vichwa saba akipanda kutoka baharini. Kila pembe yake ilikuwa na taji. Alikuwa na kumkufuru Mungu lililoandikwa kwenye kila kichwa. Mnyama huyu alionekana kama chui, miguu yake ilikuwa kama ya dubu. Mdomo wake ulikuwa kama wa simba. Joka akampa huyo mnyama uweza wake wote, kiti chake cha enzi na mamlaka kuu.

Kichwa kimoja cha mnyama kilionekana kama kimejeruhiwa na kuuawa, lakini kidonda cha mauti kilipona. Watu wote ulimwenguni walishangaa, na wote walimfuata mnyama. Watu waliliabudu joka kwa sababu limempa nguvu mnyama, na pia walimwabudu mnyama. Waliuliza, “Nani ana nguvu kama mnyama? Nani anaweza kufanya vita dhidi yake?”

Mnyama aliruhusiwa kujigamba na kumtukana Mungu na kutumia nguvu zake kwa miezi arobaini na mbili. Mnyama alifungua kinywa chake ili amtukane Mungu, alitukane jina lake, mahali anapoishi, na wale wote wanaoishi mbinguni. Alipewa uwezo wa kufanya vita na watakatifu wa Mungu na kuwashinda. Alipewa uwezo juu ya kila kabila, asili, lugha na taifa. Kila anayeishi duniani angemwabudu mnyama. Hawa ni watu wote ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo tangu mwanzo wa ulimwengu. Mwanakondoo ndiye yule aliyeuawa.

Kila mtu anayesikia mambo haya azingatie hili:

10 Yeyote ambaye ni lazima awe mfungwa,
    atakuwa mfungwa.
Yeyote ambaye ni wa kuuawa kwa upanga,
    atauawa kwa upanga.

Hii inamaanisha kwamba watakatifu wa Mungu lazima wawe na subira na imani.

Mnyama Kutoka Nchi Kavu

11 Pia nikaona mnyama mwingine akija kutoka katika nchi. Alikuwa na pembe mbili kama kondoo, lakini anaongea kama joka. 12 Mnyama huyu alisimama mbele ya mnyama wa kwanza na kutumia nguvu ile ile ya mnyama wa kwanza. Alitumia nguvu hii kumfanya kila mtu aishiye duniani amwabudu mnyama wa kwanza. Mnyama wa kwanza ndiye mwenye jeraha la mauti lililopona. 13 Mnyama wa pili alifanya miujiza[a] mikuu. Alitengeneza hata moto ushuke kutoka mbinguni kuja duniani watu wakiangalia.

14 Mnyama huyu wa pili aliwadanganya watu wanaoishi duniani kwa kutumia miujiza ambayo amepewa uwezo wa kuifanya kwa ajili ya mnyama wa kwanza. Aliwaamuru watu kutengeneza sanamu ili kumheshimu mnyama wa kwanza, aliyejeruhiwa kwa upanga lakini hakufa bali akawa hai tena. 15 Mnyama wa pili alipewa uwezo wa kuipa uzima sanamu ya mnyama wa kwanza. Kisha kinyago kiliweza kuongea na kuamuru watu wote ambao hawakukiabudu wauawe. 16 Pia mnyama wa pili aliwaamuru watu wote, wakubwa na wadogo, matajiri na maskini, walio huru au watumwa, wawekewe alama kwenye mikono yao ya kulia au kwenye vipaji vya nyuso zao. 17 Hakuna ambaye angeweza kununua au kuuza bila ya kuwa na alama hii. (Alama hii ni jina la mnyama au namba ya jina lake.)

18 Kila mwenye uelewa anaweza kujua maana ya namba ya mnyama. Hili linahitaji hekima. Namba hii ni namba ya mtu. Nayo ni 666.

Footnotes

  1. 13:13 miujiza Miujiza bandia, matendo ya kushangaza yanayofanywa kwa nguvu ya mwovu. Pia katika 6:14 na 19:20.