Malaika Mwenye Hati Ndogo

10 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevaa wingu, na upinde wa mvua kich wani. Uso wake uling’aa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto. Mkononi mwake alikuwa ameshika hati ndogo iliyokuwa imefunguliwa. Mguu wake wa kulia aliuweka juu ya bahari na mguu wake wa kushoto aliuweka juu ya nchi kavu. Naye akaita kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo. Na zile ngurumo saba zilipokwisha kuitikia, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Funga hayo yaliyosemwa na ngurumo hizo saba, ni siri; usiyaandike.”

Kisha yule malaika aliyekuwa amesimama juu ya bahari na nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni, akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivy omo, akasema, “Wakati wa kungoja umekwisha. Lakini katika siku ambazo yule malaika wa saba atakaribia kupiga tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa kama alivyowatangazia watumishi wake manabii.”

Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia pale mwanzoni ikasema nami tena, “Nenda, kachukue ile hati iliyoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na nchi kavu.”

Basi nikaenda, nikamwomba yule malaika anipe ile hati ndogo. Akaniambia, “Ichukue uile. Itakuwa chungu tumboni mwako, lakini mdomoni mwako itakuwa tamu kama asali.” 10 Basi nikaichukua ile hati ndogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikaila. Ilikuwa tamu kama asali mdomoni mwangu lakini nili poimeza, ikawa chungu tumboni mwangu. 11 Kisha nikaambiwa, “Inakubidi kutoa unabii tena kuhusu watu wengi, na mataifa, lugha na wafalme.”

Malaika Na Kitabu kidogo

10 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni akiwa amevikwa wingu na upinde wa mvua ulizunguka kichwa chake. Uso wake ulikuwa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto. Malaika alikuwa ameshika kitabu kidogo kilichofunguliwa. Akaweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wa kushoto nchi kavu. Alipaza sauti yake kama simba anavyounguruma na sauti za radi saba zikasikika.

Radi saba ziliongea, na nikaanza kuandika. Lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Usiandike ambacho radi saba zinasema. Yaache mambo hayo yawe siri.”

Kisha nikamwona malaika aliyesimama juu ya bahari na nchi kavu akinyoosha mkono wake kuelekea mbinguni. Malaika akaapa kwa nguvu ya yule aishiye milele na milele. Ndiye aliyeziumba mbingu na vyote vilivyomo ndani yake. Aliumba dunia na vyote vilivyomo ndani yake, na aliumba bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Malaika alisema, “Hakutakuwa kusubiri tena! Katika siku ambazo malaika wa saba atakuwa tayari kupuliza tarumbeta yake, mpango wa siri wa Mungu utakamilika, nao ni Habari Njema ambayo Mungu aliwaambia watumishi wake, manabii.”

Kisha nikasikia tena sauti ile ile kutoka mbinguni. Ikaniambia, “Nenda ukachukue kitabu kilicho wazi mkononi mwa malaika, aliyesimama juu ya bahari na nchi kavu.”

Hivyo nilimwendea malaika nikamwomba anipe kitabu kidogo. Naye aliniambia, “Chukua kitabu na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako lakini kitakuwa kitamu kama asali mdomoni mwako.” 10 Hivyo nilichukua kitabu kidogo kutoka mkononi mwa malaika na kukila. Mdomoni mwangu kilikuwa na ladha tamu kama asali, lakini baada ya kukila, kilikuwa kichungu tumboni mwangu. 11 Kisha nikaambiwa, “Ni lazima uwatabirie tena watu wa asili tofauti, mataifa, lugha na watawala.”