Kuhusu Ufunuo Huu

Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili apate kuwaonyesha watumishi wake mambo yatakayotokea karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe mtumishi wake Yohana, ambaye ameandika yale yote aliyoyaona, yaani ujumbe wa neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo. Amebarikiwa anayesoma maneno ya unabii huu na wale wanaosikiliza na kuzingatia yale yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia.

Salamu Kwa Makanisa Saba

Kutoka kwa Yohana. Kwa Makanisa saba yaliyoko Asia: Ninawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu aliyeko, ambaye alikuwako na atakayekuja; na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;

na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka kwa wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake;

akatufanya sisi kuwa wafalme na makuhani, tum tumikie Mungu Baba yake. Utukufu na uwezo ni wake milele na milele! Amina.

Tazama! Anakuja katika mawingu! Na kila jicho litamwona. Hata na wale waliomchoma mkuki na makabila yote ulimwenguni wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina. “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Aliyeko na aliyekuwako na ata kayekuja, Mwenyezi.”

Yohana Alivyopata Ufunuo

Mimi ni Yohana, ndugu yenu na mwenzenu katika mateso, na katika ufalme na subira kwa ajili ya Yesu Kristo. Niliwekwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya kutangaza neno la Mungu na kumshuhudia Yesu. 10 Basi, siku ya Bwana nilikuwa katika Roho, nikasikia sauti kubwa kama ya tarumbeta nyuma yangu 11 ikasema, “Andika haya yote unayoyaona kwenye kitabu, kisha ukipeleke kwe nye makanisa saba yafuatayo: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”

Sardi, Filadelfia na Laodikia.”

12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Na nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu. 13 Katikati ya vile vinara, nikaona mtu kama mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu na mkanda wa dhahabu kifuani. 14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji; na macho yake yalikuwa kama moto uwakao. 15 Miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama vile imesafishwa katika tanuru ya moto; na sauti yake ilikuwa kama sauti ya mapo romoko ya maji. 16 Katika mkono wake wa kulia alishika nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling’aa kama jua kali.

17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama mfu. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu akasema, “Usiogope. Mimi ni wa kwanza na wa mwisho. 18 Mimi ni Yeye aliye hai; nili kufa na tazama, mimi ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. 19 Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yatakayotokea baadaye. 20 Maana ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia na vile vinara saba vya taa vya dha habu ni hii: zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni hayo makanisa saba.”

Prologue

The revelation from Jesus Christ, which God gave(A) him to show his servants what must soon take place.(B) He made it known by sending his angel(C) to his servant John,(D) who testifies to everything he saw—that is, the word of God(E) and the testimony of Jesus Christ.(F) Blessed is the one who reads aloud the words of this prophecy, and blessed are those who hear it and take to heart what is written in it,(G) because the time is near.(H)

Greetings and Doxology

John,

To the seven churches(I) in the province of Asia:

Grace and peace to you(J) from him who is, and who was, and who is to come,(K) and from the seven spirits[a](L) before his throne, and from Jesus Christ, who is the faithful witness,(M) the firstborn from the dead,(N) and the ruler of the kings of the earth.(O)

To him who loves us(P) and has freed us from our sins by his blood,(Q) and has made us to be a kingdom and priests(R) to serve his God and Father(S)—to him be glory and power for ever and ever! Amen.(T)

“Look, he is coming with the clouds,”[b](U)
    and “every eye will see him,
even those who pierced him”;(V)
    and all peoples on earth “will mourn(W) because of him.”[c]
So shall it be! Amen.

“I am the Alpha and the Omega,”(X) says the Lord God, “who is, and who was, and who is to come,(Y) the Almighty.”(Z)

John’s Vision of Christ

I, John,(AA) your brother and companion in the suffering(AB) and kingdom(AC) and patient endurance(AD) that are ours in Jesus, was on the island of Patmos because of the word of God(AE) and the testimony of Jesus.(AF) 10 On the Lord’s Day(AG) I was in the Spirit,(AH) and I heard behind me a loud voice like a trumpet,(AI) 11 which said: “Write on a scroll what you see(AJ) and send it to the seven churches:(AK) to Ephesus,(AL) Smyrna,(AM) Pergamum,(AN) Thyatira,(AO) Sardis,(AP) Philadelphia(AQ) and Laodicea.”(AR)

12 I turned around to see the voice that was speaking to me. And when I turned I saw seven golden lampstands,(AS) 13 and among the lampstands(AT) was someone like a son of man,[d](AU) dressed in a robe reaching down to his feet(AV) and with a golden sash around his chest.(AW) 14 The hair on his head was white like wool, as white as snow, and his eyes were like blazing fire.(AX) 15 His feet were like bronze glowing in a furnace,(AY) and his voice was like the sound of rushing waters.(AZ) 16 In his right hand he held seven stars,(BA) and coming out of his mouth was a sharp, double-edged sword.(BB) His face was like the sun(BC) shining in all its brilliance.

17 When I saw him, I fell at his feet(BD) as though dead. Then he placed his right hand on me(BE) and said: “Do not be afraid.(BF) I am the First and the Last.(BG) 18 I am the Living One; I was dead,(BH) and now look, I am alive for ever and ever!(BI) And I hold the keys of death and Hades.(BJ)

19 “Write, therefore, what you have seen,(BK) what is now and what will take place later. 20 The mystery of the seven stars that you saw in my right hand(BL) and of the seven golden lampstands(BM) is this: The seven stars are the angels[e] of the seven churches,(BN) and the seven lampstands are the seven churches.(BO)

Footnotes

  1. Revelation 1:4 That is, the sevenfold Spirit
  2. Revelation 1:7 Daniel 7:13
  3. Revelation 1:7 Zech. 12:10
  4. Revelation 1:13 See Daniel 7:13.
  5. Revelation 1:20 Or messengers