Add parallel Print Page Options

Nani ni Mkuu Zaidi?

(Mk 9:33-37; Lk 9:46-48)

18 Wakati huo huo wanafunzi wake wakamjia Yesu na kuuliza, “Nani ni mkuu zaidi katika ufalme wa Mungu?”

Yesu akamwita mtoto mdogo, akamsimamisha mbele yao. Kisha akasema, “Ukweli ni huu, ni lazima mbadilike katika namna mnavyofikiri na muwe kama mtoto mdogo. Msipofanya hivi hamtaingia katika ufalme wa Mungu. Aliye mkuu zaidi katika ufalme wa Mungu ni yule anayejinyenyekeza kama mtoto huyu.

Unapomkubali mtoto mdogo kama huyu kama aliye wangu, unanikubali mimi.

Read full chapter