Paulo Aenda Yerusalemu

21 Tulipokwisha agana nao tuliondoka tukasafiri moja kwa moja, mpaka Kosi, na siku ya pili yake tukafika Rodo, na kutoka huko tukaenda Patara. Hapo tukapata meli iliyokuwa ikielekea Foinike tukaingia ndani tukasafiri nayo. Tulipokaribia kisiwa cha Kipro, tulikizunguka upande wa kushoto, tukasafiri mpaka Siria, tukatia nanga katika bandari ya Tiro ambapo meli yetu ili kuwa ipakue shehena yake. Tukawatafuta waamini wa huko, tukakaa nao kwa siku saba. Wale waamini wakiwa wameongozwa na Roho walim wambia Paulo asiende Yerusalemu. Muda wa kukaa nao ulipokwisha, tuliendelea na safari yetu na wale ndugu waamini pamoja na wake zao na watoto wao walitusindikiza hadi nje ya mji. Wote tulipiga magoti pale pwani tukaomba, kisha tukaagana.

Ndipo tukaingia ndani ya meli na wale ndugu wakarudi mak wao. Tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai, tukawasalimu waamini wa huko na tukakaa nao kwa siku moja. Kesho yake tuliondoka tukafika Kaisaria. Huko tukaenda nyumbani kwa mwinjilisti mmoja jina lake Filipo ambaye alikuwa kati ya wale watu saba waliochaguliwa kule Yerusalemu, tukakaa kwake. Filipo alikuwa na binti wanne ambao walikuwa bado hawajaolewa nao walikuwa na karama ya unabii. 10 Wakati tulipokuwa huko kwa siku kadhaa, alifika nabii mmoja aitwaye Agabo kutoka Yudea. 11 Alikuja kutuona akachukua mshipi wa Paulo, akautumia kufunga mikono yake mwenyewe na miguu yake akasema, “Roho Mtakatifu anasema: ‘Hivi ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mwe nye mshipi huu na kumkabidhi kwa watu wa mataifa .”’ 12 Tulipo sikia maneno haya sisi na ndugu wengine tulimwomba Paulo asiende Yerusalemu. 13 Lakini Paulo alijibu, “Kwa nini mnanivunja moyo kwa machozi yenu? Mimi niko tayari kufungwa na hata kufa huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.” 14 Na kwa kuwa hatukuweza kumshawishi asiende, tuliacha kumsihi tukamwambia, “Mapenzi ya Bwana na yatendeke.”

15 Baadaye tulijiandaa tukaondoka kwenda Yerusalemu. 16 Baadhi ya waamini kutoka Kaisaria waliongozana nasi, wakat upeleka nyumbani kwa Mnasoni, mtu wa Kipro, mmoja wa waamini wa zamani, tukae kwake.

Taarifa Ya Paulo Kwa Kanisa La Yerusalemu

17 Tulipofika Yerusalemu ndugu wa huko walitukaribisha kwa furaha. 18 Kesho yake Paulo alikwenda nasi kwa Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwepo. 19 Baada ya kuwasalimu, Paulo alitoa taarifa kamili ya mambo yote ambayo Mungu alifanya kati ya watu wa mataifa kwa kumtumia yeye. 20 Baada ya maelezo yake wote walimtukuza Mungu. Ndipo wakamwambia, “Unavyoona ndugu, kuna maelfu ya Wayahudi walioamini; nao wote wanaishika sheria kwa bidii. 21 Lakini wamekuwa wakiambiwa habari zako kuwa wewe umew afundisha Wayahudi wanaoishi na watu wa mataifa waache kushika sheria za Musa; na kuwaambia wasitahiri watoto wao, au kufuata mila za Kiyahudi. 22 Sasa tufanyeje? Kwa maana watasikia kwamba umefika Yerusalemu. 23 Kwa hiyo fanya kama tunavyokushauri. Tunao watu wanne hapa ambao wameweka nadhiri. 24 Wachukue hawa ukajitakase pamoja nao na ulipe gharama zao ili wanyoe nywele zao. Kwa njia hii kila mtu atafahamu ya kuwa mambo waliyosikia si ya kweli na kwamba wewe unashika sheria. 25 Lakini wale watu wa mataifa walioamini tumewapelekea barua tukiwaambia kuwa tumeamua wajitenge na kitu cho chote ambacho kimetolewa kwanza kama sadaka kwa miungu ya sanamu na wasinywe damu au kula nyama ya mnyama aliyeuawa kwa kunyongwa. Tena ni lazima wajitenge na uasherati.” 26 Kwa hiyo Paulo akawachukua wale watu na kesho yake akajita kasa pamoja nao. Akaingia ndani ya Hekalu ili akatoe taarifa ya tarehe ambayo siku zao za utakaso zitamalizika na sadaka kutolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.

Paulo Akamatwa

27 Zile siku saba zilipokaribia kumalizika, Wayahudi kutoka jimbo la Asia waliokuwa wamemwona Paulo ndani ya hekalu, waka chochea umati mkubwa wa watu wakamkamata Paulo. 28 Wakapiga kelele wakasema, “Ndugu Waisraeli, tusaidieni! Huyu ni yule mtu ambaye anafundisha watu kila mahali wawadharau watu wetu, wazid harau sheria zetu na hata hili Hekalu. Zaidi ya hayo amewaleta Wagiriki katika Hekalu na kuchafua hapa mahali patakatifu!” 29 Walisema hivi kwa sababu walimwona Trofimo, mwenyeji wa Efeso, akiwa mjini na Paulo wakadhani kuwa Paulo alikuwa amemleta Hekaluni . 30 Habari hizi zikawachochea watu wa mji mzima nao wakakimbia pamoja kwa hasira wakamkamata Paulo wakamtoa nje ya Hekalu. Milango ya Hekalu ikafungwa. 31 Walipokuwa wakitaka kum wua, habari zikamfikia Jemadari wa jeshi la askari wa Kirumi kwamba Yerusalemu yote ilikuwa katika hali ya machafuko. 32 Na mara yule jemadari akachukua maofisa wengine wa jeshi pamoja na maaskari wakakimbilia kwenye ile ghasia. Watu walipomwona jema dari na askari wakija, waliacha kumpiga Paulo. 33 Kisha yule jemadari akamkamata Paulo akaamuru afungwe kwa minyororo miwili. Akauliza yeye ni nani na alikuwa amefanya nini. 34 Baadhi ya watu wakapiga kelele wakieleza jambo moja na wengine wakieleza jingine. Yule jemadari alipoona kuwa hawezi kupata ukweli kamili kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo apelekwe katika ngome ya jeshi. 35 Basi walipofika penye ngazi, ilibidi askari wambebe Paulo juu juu kwa sababu ya fujo za ule umati wa watu 36 ambao walikuwa wakiwafuata wakipiga kelele, “Mwueni!”

Paulo Anajitetea

37 Walipokuwa wanakaribia kuingia katika ngome ya jeshi, Paulo alimwuliza yule jemadari, “Je, naweza kusema jambo moja?” Yule jemadari akajibu, “Kumbe unajua Kigiriki? 38 Wewe si yule Mmisri ambaye siku za karibuni alianzisha uasi akaongoza majam bazi elfu nne wenye silaha jangwani?” 39 Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso, jimbo la Kilikia na raia wa mji wenye sifa. Tafadhali niruhusu nizungumze na hawa watu.” 40 Yule jemadari alipomruhusu azungumze, Paulo akasimama penye ngazi akawapungia watu mkono ili wanyamaze. Watu walipokuwa kimya kabisa, Paulo akazungumza nao kwa lugha ya Kiebrania, akasema;

21 And it came to pass, that after we were gotten from them, and had launched, we came with a straight course unto Coos, and the day following unto Rhodes, and from thence unto Patara:

And finding a ship sailing over unto Phenicia, we went aboard, and set forth.

Now when we had discovered Cyprus, we left it on the left hand, and sailed into Syria, and landed at Tyre: for there the ship was to unlade her burden.

And finding disciples, we tarried there seven days: who said to Paul through the Spirit, that he should not go up to Jerusalem.

And when we had accomplished those days, we departed and went our way; and they all brought us on our way, with wives and children, till we were out of the city: and we kneeled down on the shore, and prayed.

And when we had taken our leave one of another, we took ship; and they returned home again.

And when we had finished our course from Tyre, we came to Ptolemais, and saluted the brethren, and abode with them one day.

And the next day we that were of Paul's company departed, and came unto Caesarea: and we entered into the house of Philip the evangelist, which was one of the seven; and abode with him.

And the same man had four daughters, virgins, which did prophesy.

10 And as we tarried there many days, there came down from Judaea a certain prophet, named Agabus.

11 And when he was come unto us, he took Paul's girdle, and bound his own hands and feet, and said, Thus saith the Holy Ghost, So shall the Jews at Jerusalem bind the man that owneth this girdle, and shall deliver him into the hands of the Gentiles.

12 And when we heard these things, both we, and they of that place, besought him not to go up to Jerusalem.

13 Then Paul answered, What mean ye to weep and to break mine heart? for I am ready not to be bound only, but also to die at Jerusalem for the name of the Lord Jesus.

14 And when he would not be persuaded, we ceased, saying, The will of the Lord be done.

15 And after those days we took up our carriages, and went up to Jerusalem.

16 There went with us also certain of the disciples of Caesarea, and brought with them one Mnason of Cyprus, an old disciple, with whom we should lodge.

17 And when we were come to Jerusalem, the brethren received us gladly.

18 And the day following Paul went in with us unto James; and all the elders were present.

19 And when he had saluted them, he declared particularly what things God had wrought among the Gentiles by his ministry.

20 And when they heard it, they glorified the Lord, and said unto him, Thou seest, brother, how many thousands of Jews there are which believe; and they are all zealous of the law:

21 And they are informed of thee, that thou teachest all the Jews which are among the Gentiles to forsake Moses, saying that they ought not to circumcise their children, neither to walk after the customs.

22 What is it therefore? the multitude must needs come together: for they will hear that thou art come.

23 Do therefore this that we say to thee: We have four men which have a vow on them;

24 Them take, and purify thyself with them, and be at charges with them, that they may shave their heads: and all may know that those things, whereof they were informed concerning thee, are nothing; but that thou thyself also walkest orderly, and keepest the law.

25 As touching the Gentiles which believe, we have written and concluded that they observe no such thing, save only that they keep themselves from things offered to idols, and from blood, and from strangled, and from fornication.

26 Then Paul took the men, and the next day purifying himself with them entered into the temple, to signify the accomplishment of the days of purification, until that an offering should be offered for every one of them.

27 And when the seven days were almost ended, the Jews which were of Asia, when they saw him in the temple, stirred up all the people, and laid hands on him,

28 Crying out, Men of Israel, help: This is the man, that teacheth all men every where against the people, and the law, and this place: and further brought Greeks also into the temple, and hath polluted this holy place.

29 (For they had seen before with him in the city Trophimus an Ephesian, whom they supposed that Paul had brought into the temple.)

30 And all the city was moved, and the people ran together: and they took Paul, and drew him out of the temple: and forthwith the doors were shut.

31 And as they went about to kill him, tidings came unto the chief captain of the band, that all Jerusalem was in an uproar.

32 Who immediately took soldiers and centurions, and ran down unto them: and when they saw the chief captain and the soldiers, they left beating of Paul.

33 Then the chief captain came near, and took him, and commanded him to be bound with two chains; and demanded who he was, and what he had done.

34 And some cried one thing, some another, among the multitude: and when he could not know the certainty for the tumult, he commanded him to be carried into the castle.

35 And when he came upon the stairs, so it was, that he was borne of the soldiers for the violence of the people.

36 For the multitude of the people followed after, crying, Away with him.

37 And as Paul was to be led into the castle, he said unto the chief captain, May I speak unto thee? Who said, Canst thou speak Greek?

38 Art not thou that Egyptian, which before these days madest an uproar, and leddest out into the wilderness four thousand men that were murderers?

39 But Paul said, I am a man which am a Jew of Tarsus, a city in Cilicia, a citizen of no mean city: and, I beseech thee, suffer me to speak unto the people.

40 And when he had given him licence, Paul stood on the stairs, and beckoned with the hand unto the people. And when there was made a great silence, he spake unto them in the Hebrew tongue, saying,