Paulo Ahubiri Thesalonike

17 Walisafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalo nike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi. Paulo aliingia ndani ya sinagogi kama ilivyokuwa kawaida yake, na kwa muda wa majuma matatu akawa akihojiana na Wayahudi akitumia Maandiko kuwaonyesha wazi kwamba ilikuwa ni lazima Kristo ateswe na afu fuke kutoka kwa wafu, akamalizia kwa kusema, “Huyu Yesu ambaye nawaambia habari zake, ndiye Kristo.” Baadhi yao wakakubaliana nao, wakajiunga na Paulo na Sila. Pia umati mkubwa wa Wagiriki waliomcha Mungu, na baadhi ya wanawake viongozi wakaungana nao. Lakini Wayahudi wengi waliwaonea Paulo na Sila wivu, waka chochea baadhi ya wazururaji waovu waanzishe fujo mji mzima; kisha wakashambulia nyumba ya Yasoni ambamo Paulo na Sila wali kuwa wakikaa, ili wawatoe nje. Walipokuta hawako huko, wakawa kamata Yasoni na baadhi ya ndugu waamini wakawaleta mbele ya viongozi wa mji wakipiga kelele: “Hawa watu ambao wamepindua dunia nzima wamefika huku na huyu Yasoni amewakaribisha. Wao wanavunja sheria ya Kaisari kwa kusema eti kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu.” Mashtaka haya ya Wayahudi yaliwafadhaisha watu wote pamoja na wale viongozi wa mji. Kwa hiyo wakataka dhamana kutoka kwa Yasoni na waamini wenzake kabla ya kuwaachilia waende zao.

10 Giza lilipoingia, wale ndugu waamini waliwatoa Paulo na Sila wakaondoka kwenda Beroya, na walipowasili wakaingia katika Sinagogi la Wayahudi. 11 Watu wa Beroya walikuwa waungwana zaidi kuliko watu wa Thesalonike. Walisikiliza neno la Mungu kwa hamu wakachambua Maandiko kila siku ili waone kama waliyokuwa wakiam biwa na Paulo ni kweli. 12 Wengi wao waliamini, ikiwa ni pamoja na wanawake maarufu wa Kigiriki na wanaume wengi. 13 Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, walikuja wakaanza kuwashawishi watu na kuwa chochea waanzishe vurugu. 14 Na ndugu wa Beroya wakafanya haraka wakamsafirisha Paulo kuelekea bandarini , lakini Sila na Timotheo walibaki Beroya. 15 Wale waliomsindikiza Paulo walienda naye mpaka Athene. Ndipo wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba, Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.

Paulo Ahubiri Huko Athene

16 Paulo alipokuwa akiwangojea wenzake huko Athene alisikit ishwa sana kuona jinsi mji ulivyojaa miungu ya sanamu. 17 Kwa hiyo akawa akienda katika sinagogi kujadiliana na Wayahudi na Wagiriki waliomcha Mungu na katika mahali pa soko ambako aliongea na watu aliokutana nao. 18 Huko sokoni alikutana na vikundi viwili vya wanafalsafa waitwao Waepikureo na Wastoiko. Baadhi yao wakamdhihaki wakisema, “Huyu mpayukaji asiyejua kitu anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Anaelekea kuwa mhubiri wa miungu wageni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na ufufuo. 19 Wakamkamata wakampeleka kwenye baraza la Areopago wakamwambia, “Tungependa kufahamu haya mafundisho mapya unayotangaza. 20 Mambo tunayosikia kuwa unafundisha ni mageni kwetu nasi tungependa kuelewa maana yake.” 21 Waathene na hata wageni walikuwa na tabia ya kutumia wakati wao wote katika mazungumzo ya mambo yo yote ambayo yanaonekana kuwa mageni au mapya.

Hotuba Ya Paulo Kwenye Areopago

22 Kwa hiyo Paulo alisimama kati kati ya Areopago akasema, “Ndugu wa Athene! Nimeona katika kila jambo kuwa ninyi ni watu wa dini hasa. 23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini niliona sehemu nyingi za kuabudia. Niliona pia madhabahu moja iliyoan dikwa, ‘Kwa Mungu asiyejulikana.’ Huyo Mungu mnayemwabudu bila kumfahamu, ndiye ninayemtangaza kwenu. 24 Mungu aliyeumba dunia na vitu vyote vilivyomo, ambaye pia ni Bwana wa mbingu na nchi, haishi katika mahekalu yaliyojengwa na wanadamu. 25 Wala hahu dumiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji cho chote; kwa sababu yeye ndiye anayewapa watu wote uhai na pumzi na kila kitu. 26 Yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu waishi juu ya nchi kutokana na mtu mmoja. Pia amepanga muda wa maisha ya watu wote, akaweka na mipaka ya mahali watakapoishi 27 ili wamtafute Mungu na wamfahamu. Lakini Yeye hayuko mbali nasi kwa maana 28 ‘Tunaishi na kuenenda na kuwa na uhai ndani yake,’ na kama mtunga mashairi wenu alivyosema, ‘Sisi ni uzao wa Mungu.’ 29 Kwa kuwa sisi ni wa uzao wa Mungu hatupaswi kudhani kuwa yeye ni kama sanamu ya dhahabu au fedha au jiwe iliyotengenezwa kwa akili na ufundi wa mwanadamu. 30 Mungu alisamehe ujinga huo wa zamani, lakini sasa anaamuru watu wote watubu, waachane na miungu ya sanamu. 31 Kwa kuwa amepanga siku ambayo atahukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua, ambaye amemhakikisha kwa watu wote kwa kumfufua kutoka kwa wafu.” 32 Waathene waliposikia juu ya ufufuo wa wafu, baadhi yao wakamdhihaki; lakini wengine wal isema, “Tutataka kusikia tena juu ya habari hii.” 33 Kwa hiyo Paulo akaondoka. 34 Lakini baadhi ya watu walimfuata Paulo wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago, na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine.

Paulo na Sila Wakiwa Thesalonike

17 Paulo na Sila walisafiri kupitia miji ya Amfipoli na Apolonia. Wakafika katika mji wa Thesalonike, ambako kulikuwa sinagogi la Kiyahudi. Paulo aliingia katika sinagogi kuwaona Wayahudi kama alivyokuwa akifanya. Wiki tatu zilizofuatia, kila siku ya Sabato alijadiliana nao kuhusu Maandiko. Alifafanua Maandiko kuwaonesha kuwa Masihi ilikuwa afe na kufufuka kutoka kwa wafu. Aliwaambia, “Huyu Yesu ninayewaambia habari zake ndiye Masihi.” Baadhi ya Wayahudi pale waliwaamini Paulo na Sila na waliamua kujiunga nao. Idadi kubwa ya Wayunani waliokuwa wanamwabudu Mungu wa kweli na wanawake wengi maarufu walijiunga nao pia.

Lakini Wayahudi ambao hawakuamini wakaingiwa na wivu, hivyo wakawakusanya baadhi ya watu wabaya katikati ya mji ili kufanya vurugu. Wakaunda kundi na wakanzisha vurugu mjini. Walikwenda nyumbani kwa Yasoni kuwatafuta Paulo na Sila. Walitaka kuwaleta mbele ya watu. Walipowakosa wakamkamata na kumburuta Yasoni na baadhi ya waamini wengine na kuwapeleka kwa viongozi wa mji. Watu wakapasa sauti na kusema, “Watu hawa Wamesababisha matatizo mengi kila mahali ulimwenguni, na sasa wamekuja hapa pia! Yasoni amewaweka nyumbani mwake. Wanavunja sheria za Kaisari. Wanasema kuna mfalme mwingine anayeitwa Yesu.”

Viongozi wa mji na watu wengine waliposikia hili waliudhika sana. Wakawalazimisha Yasoni na waamini wengine kuweka dhamana ya fedha kuthibitisha kuwa hakutakuwa vurugu tena. Kisha wakawaruhusu kuondoka.

Paulo na Sila Waenda Berea

10 Usiku ule ule waamini wakawapeleka Paulo na Sila katika mji mwingine ulioitwa Berea. Walipofika pale, walikwenda katika sinagogi la Kiyahudi. 11 Watu wa Berea walikuwa radhi kujifunza kuliko watu wa Thesalonike. Walifurahi waliposikia ujumbe aliowaambia Paulo. Waliyachunguza Maandiko kila siku ili kuhakikisha kuwa waliyoyasikia ni ya kweli. 12 Matokeo yake ni kuwa watu wengi miongoni mwao waliamini, wakiwemo wanawake maarufu Wayunani na wanaume.

13 Lakini Wayahudi wa Thesalonike walipojua kuwa Paulo alikuwa anawahubiri Ujumbe wa Mungu katika mji wa Berea, walikwenda huko pia. Waliwakasirisha watu na kufanya vurugu. 14 Hivyo waamini walimpeleka Paulo sehemu za pwani, lakini Sila na Timotheo walibaki Berea. 15 Wale waliokwenda na Paulo walimpeleka katika mji wa Athene. Waliporudi Berea, waliwapa ujumbe kutoka kwa Paulo Timotheo na Sila kuwa waende kuungana naye haraka kadiri watakavyoweza.

Paulo Akiwa Athene

16 Paulo alipokuwa akiwasubiri Sila na Timotheo katika mji wa Athene, aliudhika kwa sababu aliona mji ulikuwa umejaa sanamu. 17 Alipokuwa katika sinagogi alizungumza na Wayahudi na Wayunani waliokuwa wakimwabudu Mungu wa kweli. Alikwenda pia katika sehemu za wazi za umma za mikutano na kuzungumza na kila aliyekutana naye. 18 Baadhi ya wanafalsafa Waepikureo[a] na baadhi ya wanafalsafa Wastoiko[b] walibishana naye.

Baadhi yao walisema, “Mtu huyu hakika hajui anachokisema. Anajaribu kusema nini?” Paulo alikuwa anawaambia Habari Njema kuhusu Yesu na ufufuo. Hivyo walisema, “Anaonekana anatueleza kuhusu baadhi ya miungu wa kigeni.”

19 Walimchukua Paulo kwenye mkutano wa baraza la Areopago. Wakasema, “Tafadhali tufafanunile hili wazo jipya ambalo umekuwa ukifundisha. 20 Mambo unayosema ni mapya kwetu. Hatujawahi kusikia mafundisho haya, na tunataka kufahamu yana maana gani.” 21 (Watu wa Athene na wageni walioishi pale walitumia muda wao bila kufanya kazi yoyote isipokuwa kusikiliza na kuzungumza kuhusu mawazo mapya.)

22 Ndipo Paulo alisimama mbele ya mkutano wa baraza la Areopago na kusema, “Watu wa Athene, kila kitu ninachokiona hapa kinanionyesha kuwa ninyi ni watu wa dini sana. 23 Nilikuwa natembea katika mji wenu na nimeona mambo mnayoyaabudu. Niliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya juu yake: ‘Kwa Mungu Asiyejulikana.’ Mnamwabudu mungu msiyemjua. Huyu ni Mungu ninayetaka kuwaambia habari zake.

24 Ni Mungu aliyeumba ulimwengu na kila kitu ndani yake. Ni Bwana wa mbingu na nchi. Haishi katika mahekalu yaliyojengwa kwa mikono ya kibinadamu. 25 Ndiye anayewapa watu uzima, pumzi na kila kitu wanachohitaji. Hahitaji msaada wowote kutoka kwao. Ana kila kitu anachohitaji. 26 Mungu alianza kwa kumwumba mtu mmoja, na kutoka kwake aliumba mataifa yote mbalimbali, na akawaweka kila mahali ulimwenguni. Na aliamua ni wakati gani na wapi ambapo angewaweka ili waishi.

27 Mungu alitaka watu wamtafute yeye, na pengine kwa kumtafuta kila mahali, wangempata. Lakini hayuko mbali na kila mmoja wetu. 28 Ni kupitia Yeye tunaweza kuishi, kufanya yale tunayofanya na kuwa kama tulivyo. Kama baadhi ya methali zenu zilivyokwisha sema, ‘Sote tunatokana naye.’

29 Huo ndio ukweli. Sote tunatokana na Mungu. Hivyo ni lazima msifikiri kuwa Yeye ni kama kitu ambacho watu hukidhania au kukitengeneza. Hivyo ni lazima tusifikiri kuwa ametengenezwa kwa dhahabu, fedha au jiwe. 30 Hapo zamani watu hawakumwelewa Mungu, naye Mungu hakulijali hili. Lakini sasa anawaagiza wanadamu kila mahali kubadilika na kumgeukia Yeye. 31 Amekwisha chagua siku ambayo atawahukumu watu wote ulimwenguni katika namna isiyo na upendeleo. Atafanya hili kwa kumtumia mtu aliyemchagua zamani zilizopita. Na alithibitisha kwa kila mtu kwamba huyu ndiye mtu atakayefanya. Alilithibitisha kwa kumfufua kutoka kwa wafu!”

32 Watu waliposikia kuhusu mtu kufufuliwa kutoka kwa kifo, baadhi yao walicheka. Lakini wengine walisema, “Tutasikiliza mengi kuhusu hili kutoka kwako baadaye.” 33 Hivyo Paulo akaondoka kwenye mkutano wa baraza. 34 Lakini baadhi ya watu waliungana na Paulo na kuwa waamini. Miongoni mwao walikuwa Dionisi, ambaye alikuwa mjumbe wa baraza la Areopago, na mwanamke aliyeitwa Damari na baadhi ya wengine.

Footnotes

  1. 17:18 Waepikureo Falsafa ya Waepikureo ilianzishwa na Epikureo katika mji wa Athene kama mwaka 300 Kabla ya Kristo. Waepikureo walitafuta starehe katika maisha kwa kuepuka maumivu na walijulikana kwa kutoamini katika miungu na desturi za kidini.
  2. 17:18 Wastoiko Falsafa ya Wastoiko ilianzishwa na Zeno katika mji wa Athene kati ya mwaka 342-270 Kabla ya Kristo. Wastoiko walijitahidi kuishi maisha safi kwa unyenyekevu na kwa asili, kutegemea na rasilimali alizokuwa nazo mtu na ukomo wa hamu yake.