Paulo Amchagua Timotheo

16 Paulo alisafiri mpaka Derbe na Listra ambako mwanafunzi mmoja aitwaye Timotheo aliishi. Mama yake Timotheo alikuwa Myahudi naye alikuwa mwamini; baba yake alikuwa Mgiriki. Timotheo alikuwa mtu mwenye sifa nzuri kwa ndugu wote wa huko Listra na Ikonio. Paulo alitaka amchukue Timotheo awe akisafiri naye, kwa hiyo akamtahiri ili asiwe kikwazo kwa Wayahudi wa eneo hilo ambao walijua ya kuwa baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki. Walipokuwa wakipita katika miji mbali mbali waliwasilisha maamuzi ya baraza la mitume na wazee wa kanisa huko Yerusalemu ili wayazingatie. Kwa hiyo makanisa yakazidi kuimarika katika imani na idadi ya waamini ikawa inaongezeka kila siku.

Paulo Anaongozwa Kwenda Makedonia

Walisafiri kupitia wilaya ya Firigia na Galatia, kwa sababu Roho Mtakatifu aliwazuia wasihubiri neno sehemu za Asia. Wali pofika kwenye mpaka wa Misia walijaribu kuingia wilaya ya Bithi nia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu. Kwa hiyo wakaendelea na safari kupitia Misia, wakafika Troa. Usiku huo Paulo akaona katika ndoto, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Njoo Makedo nia ukatusaidie.” 10 Mara baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kuondoka kwenda Makedonia kwa sababu tuliona kuwa Mungu ametuita kuhubiri Habari Njema kwa watu wa huko. 11 Tuliondoka Troa kwa meli tukaenda moja kwa moja mpaka Samo trake, na kesho yake tukafika Neapoli. 12 Kutoka huko tukaende lea na safari hadi Filipi, mji mkuu wa Makedonia ambao ni koloni la Kirumi. 13 Tulikaa Filipi kwa siku chache na siku ya sabato tukaenda nje ya mji kando ya mto, mahali ambapo tulidhani pange faa kwa maombi. Tukakaa chini tukaongea na baadhi ya wanawake waliokuja pale mtoni. 14 Mmoja wa wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mwenyeji wa mji wa Thiatira na mfanya biashara wa nguo za zambarau. Yeye alimpenda Mungu na Bwana akaufungua moyo wake akapokea mahubiri ya Paulo. 15 Basi alipokwisha kubatizwa yeye na jamaa yake, alitusihi akisema, “Kama mmenipokea kweli kama mwamini, tafadhali njooni mkae nyumbani kwangu.” Akatushaw ishi twende naye.

Paulo Na Sila Wafungwa Gerezani

16 Siku moja tulipokuwa tukienda mahali pa sala tulikutana na msichana mmoja mtumwa aliyekuwa na pepo wa kutabiri mambo yaj ayo. Alikuwa amewapatia mabwana wake faida kubwa kwa kutumia uwezo wa kutabiria watu mambo yajayo. 17 Basi alimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye Juu kuliko wote. Wao wanatangaza kwenu njia ya wokovu.” 18 Na aliendelea kusema maneno haya kwa siku nyingi. Lakini Paulo aliudhika, akageuka na kumwambia yule pepo, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo akamtoka wakati ule ule. 19 Basi mabwana wa yule msichana mtumwa walipoona kuwa matumaini yao ya kuendelea kujipatia fedha yametoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawapeleka sokoni mbele ya viongozi wa mji. 20 Waka washtaki kwa mahakimu wakisema, “ Hawa watu ni Wayahudi nao wan aleta fujo mjini kwetu. 21 Wanafundisha desturi ambazo si halali kwetu kama raia wa Kirumi kuzikubali au kuzitimiza.” 22 Umati wa watu waliokuwepo wakaunga mkono mashtaka haya, na wale maha kimu wakatoa amri Paulo na Sila wavuliwe nguo wachapwe viboko. 23 Baada ya kuchapwa sana wakatupwa gerezani, na askari jela akaamriwa aweke ulinzi mkali. 24 Yule askari jela alipopokea amri hiyo akawaweka katika chumba cha ndani mle gerezani na kisha akafunga miguu yao kwa mkatale. 25 Ilipokaribia saa sita za usiku, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kum sifu Mungu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. 26 Gha fla pakatokea tetemeko kubwa la nchi, hata msingi wa jengo la gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikawa wazi na mikatale yao ikafunguka. 27 Askari wa gereza alipoona kuwa milango ya gereza ni wazi, alivuta upanga wake ili ajiue, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka. 28 Lakini Paulo akapiga kelele kum zuia, akasema, “Usijidhuru kwa maana hatujatoroka, wote tuko hapa.” 29 Askari akaitisha taa iletwe, akaingia ndani ya chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka miguuni mwa Paulo na Sila. 30 Kisha akawatoa nje akasema, “Ndugu zangu, nifanye nini ili nipate kuokoka?” 31 Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka, wewe pamoja na jamaa yako.” 32 Wakawaambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwa wanaishi nyumbani kwake. 33 Yule askari akawachukua saa ile ile akaosha majeraha yao, naye akabatizwa pamoja na wote waliokuwa nyumbani kwake. 34 Aka wachukua, akawaandalia chakula nyumbani kwake, naye akafurahi pamoja na jamaa yake kwa kuwa alikuwa amemwamini Mungu.

35 Kulipopambazuka wale mahakimu wakamtuma polisi amwambie yule askari jela, “Waachie hao watu waende zao.” 36 Yule askari jela akampasha habari Paulo akisema, “Mahakimu wametuma niwaachilie huru; kwa hiyo tokeni mwende kwa amani.” 37 Lakini Paulo akawaambia, “Wametuchapa viboko hadharani bila kufanya kesi na kutoa hukumu, na sisi ni raia wa Kirumi. Je, sasa wana taka kututoa gerezani kisiri siri? Hii si haki! Waambieni wao waje watutoe humu gerezani wenyewe.” 38 Yule askari akarudi kwa wale mahakimu kuwaeleza maneno haya, nao wakaogopa sana walipofa hamu kuwa Paulo na Sila ni raia wa Kirumi. 39 Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha. Kisha wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke mjini. 40 Paulo na Sila walipotoka gerezani walimtembelea Lidia, wakakutana na ndugu waamini wakawatia moyo; ndipo wakaondoka.

Timothy Joins Paul and Silas

16 Paul came to Derbe and then to Lystra,(A) where a disciple named Timothy(B) lived, whose mother was Jewish and a believer(C) but whose father was a Greek. The believers(D) at Lystra and Iconium(E) spoke well of him. Paul wanted to take him along on the journey, so he circumcised him because of the Jews who lived in that area, for they all knew that his father was a Greek.(F) As they traveled from town to town, they delivered the decisions reached by the apostles and elders(G) in Jerusalem(H) for the people to obey.(I) So the churches were strengthened(J) in the faith and grew daily in numbers.(K)

Paul’s Vision of the Man of Macedonia

Paul and his companions traveled throughout the region of Phrygia(L) and Galatia,(M) having been kept by the Holy Spirit from preaching the word in the province of Asia.(N) When they came to the border of Mysia, they tried to enter Bithynia, but the Spirit of Jesus(O) would not allow them to. So they passed by Mysia and went down to Troas.(P) During the night Paul had a vision(Q) of a man of Macedonia(R) standing and begging him, “Come over to Macedonia and help us.” 10 After Paul had seen the vision, we(S) got ready at once to leave for Macedonia, concluding that God had called us to preach the gospel(T) to them.

Lydia’s Conversion in Philippi

11 From Troas(U) we put out to sea and sailed straight for Samothrace, and the next day we went on to Neapolis. 12 From there we traveled to Philippi,(V) a Roman colony and the leading city of that district[a] of Macedonia.(W) And we stayed there several days.

13 On the Sabbath(X) we went outside the city gate to the river, where we expected to find a place of prayer. We sat down and began to speak to the women who had gathered there. 14 One of those listening was a woman from the city of Thyatira(Y) named Lydia, a dealer in purple cloth. She was a worshiper of God. The Lord opened her heart(Z) to respond to Paul’s message. 15 When she and the members of her household(AA) were baptized,(AB) she invited us to her home. “If you consider me a believer in the Lord,” she said, “come and stay at my house.” And she persuaded us.

Paul and Silas in Prison

16 Once when we were going to the place of prayer,(AC) we were met by a female slave who had a spirit(AD) by which she predicted the future. She earned a great deal of money for her owners by fortune-telling. 17 She followed Paul and the rest of us, shouting, “These men are servants of the Most High God,(AE) who are telling you the way to be saved.” 18 She kept this up for many days. Finally Paul became so annoyed that he turned around and said to the spirit, “In the name of Jesus Christ I command you to come out of her!” At that moment the spirit left her.(AF)

19 When her owners realized that their hope of making money(AG) was gone, they seized Paul and Silas(AH) and dragged(AI) them into the marketplace to face the authorities. 20 They brought them before the magistrates and said, “These men are Jews, and are throwing our city into an uproar(AJ) 21 by advocating customs unlawful for us Romans(AK) to accept or practice.”(AL)

22 The crowd joined in the attack against Paul and Silas, and the magistrates ordered them to be stripped and beaten with rods.(AM) 23 After they had been severely flogged, they were thrown into prison, and the jailer(AN) was commanded to guard them carefully. 24 When he received these orders, he put them in the inner cell and fastened their feet in the stocks.(AO)

25 About midnight(AP) Paul and Silas(AQ) were praying and singing hymns(AR) to God, and the other prisoners were listening to them. 26 Suddenly there was such a violent earthquake that the foundations of the prison were shaken.(AS) At once all the prison doors flew open,(AT) and everyone’s chains came loose.(AU) 27 The jailer woke up, and when he saw the prison doors open, he drew his sword and was about to kill himself because he thought the prisoners had escaped.(AV) 28 But Paul shouted, “Don’t harm yourself! We are all here!”

29 The jailer called for lights, rushed in and fell trembling before Paul and Silas.(AW) 30 He then brought them out and asked, “Sirs, what must I do to be saved?”(AX)

31 They replied, “Believe(AY) in the Lord Jesus, and you will be saved(AZ)—you and your household.”(BA) 32 Then they spoke the word of the Lord to him and to all the others in his house. 33 At that hour of the night(BB) the jailer took them and washed their wounds; then immediately he and all his household were baptized.(BC) 34 The jailer brought them into his house and set a meal before them; he(BD) was filled with joy because he had come to believe in God—he and his whole household.

35 When it was daylight, the magistrates sent their officers to the jailer with the order: “Release those men.” 36 The jailer(BE) told Paul, “The magistrates have ordered that you and Silas be released. Now you can leave. Go in peace.”(BF)

37 But Paul said to the officers: “They beat us publicly without a trial, even though we are Roman citizens,(BG) and threw us into prison. And now do they want to get rid of us quietly? No! Let them come themselves and escort us out.”

38 The officers reported this to the magistrates, and when they heard that Paul and Silas were Roman citizens, they were alarmed.(BH) 39 They came to appease them and escorted them from the prison, requesting them to leave the city.(BI) 40 After Paul and Silas came out of the prison, they went to Lydia’s house,(BJ) where they met with the brothers and sisters(BK) and encouraged them. Then they left.

Footnotes

  1. Acts 16:12 The text and meaning of the Greek for the leading city of that district are uncertain.