Paulo Amchagua Timotheo

16 Paulo alisafiri mpaka Derbe na Listra ambako mwanafunzi mmoja aitwaye Timotheo aliishi. Mama yake Timotheo alikuwa Myahudi naye alikuwa mwamini; baba yake alikuwa Mgiriki. Timotheo alikuwa mtu mwenye sifa nzuri kwa ndugu wote wa huko Listra na Ikonio. Paulo alitaka amchukue Timotheo awe akisafiri naye, kwa hiyo akamtahiri ili asiwe kikwazo kwa Wayahudi wa eneo hilo ambao walijua ya kuwa baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki. Walipokuwa wakipita katika miji mbali mbali waliwasilisha maamuzi ya baraza la mitume na wazee wa kanisa huko Yerusalemu ili wayazingatie. Kwa hiyo makanisa yakazidi kuimarika katika imani na idadi ya waamini ikawa inaongezeka kila siku.

Paulo Anaongozwa Kwenda Makedonia

Walisafiri kupitia wilaya ya Firigia na Galatia, kwa sababu Roho Mtakatifu aliwazuia wasihubiri neno sehemu za Asia. Wali pofika kwenye mpaka wa Misia walijaribu kuingia wilaya ya Bithi nia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu. Kwa hiyo wakaendelea na safari kupitia Misia, wakafika Troa. Usiku huo Paulo akaona katika ndoto, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Njoo Makedo nia ukatusaidie.” 10 Mara baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kuondoka kwenda Makedonia kwa sababu tuliona kuwa Mungu ametuita kuhubiri Habari Njema kwa watu wa huko. 11 Tuliondoka Troa kwa meli tukaenda moja kwa moja mpaka Samo trake, na kesho yake tukafika Neapoli. 12 Kutoka huko tukaende lea na safari hadi Filipi, mji mkuu wa Makedonia ambao ni koloni la Kirumi. 13 Tulikaa Filipi kwa siku chache na siku ya sabato tukaenda nje ya mji kando ya mto, mahali ambapo tulidhani pange faa kwa maombi. Tukakaa chini tukaongea na baadhi ya wanawake waliokuja pale mtoni. 14 Mmoja wa wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mwenyeji wa mji wa Thiatira na mfanya biashara wa nguo za zambarau. Yeye alimpenda Mungu na Bwana akaufungua moyo wake akapokea mahubiri ya Paulo. 15 Basi alipokwisha kubatizwa yeye na jamaa yake, alitusihi akisema, “Kama mmenipokea kweli kama mwamini, tafadhali njooni mkae nyumbani kwangu.” Akatushaw ishi twende naye.

Paulo Na Sila Wafungwa Gerezani

16 Siku moja tulipokuwa tukienda mahali pa sala tulikutana na msichana mmoja mtumwa aliyekuwa na pepo wa kutabiri mambo yaj ayo. Alikuwa amewapatia mabwana wake faida kubwa kwa kutumia uwezo wa kutabiria watu mambo yajayo. 17 Basi alimfuata Paulo na sisi akipiga kelele, “Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye Juu kuliko wote. Wao wanatangaza kwenu njia ya wokovu.” 18 Na aliendelea kusema maneno haya kwa siku nyingi. Lakini Paulo aliudhika, akageuka na kumwambia yule pepo, “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo, umtoke!” Yule pepo akamtoka wakati ule ule. 19 Basi mabwana wa yule msichana mtumwa walipoona kuwa matumaini yao ya kuendelea kujipatia fedha yametoweka, wakawakamata Paulo na Sila wakawapeleka sokoni mbele ya viongozi wa mji. 20 Waka washtaki kwa mahakimu wakisema, “ Hawa watu ni Wayahudi nao wan aleta fujo mjini kwetu. 21 Wanafundisha desturi ambazo si halali kwetu kama raia wa Kirumi kuzikubali au kuzitimiza.” 22 Umati wa watu waliokuwepo wakaunga mkono mashtaka haya, na wale maha kimu wakatoa amri Paulo na Sila wavuliwe nguo wachapwe viboko. 23 Baada ya kuchapwa sana wakatupwa gerezani, na askari jela akaamriwa aweke ulinzi mkali. 24 Yule askari jela alipopokea amri hiyo akawaweka katika chumba cha ndani mle gerezani na kisha akafunga miguu yao kwa mkatale. 25 Ilipokaribia saa sita za usiku, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kum sifu Mungu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. 26 Gha fla pakatokea tetemeko kubwa la nchi, hata msingi wa jengo la gereza ukatikisika. Mara milango ya gereza ikawa wazi na mikatale yao ikafunguka. 27 Askari wa gereza alipoona kuwa milango ya gereza ni wazi, alivuta upanga wake ili ajiue, akidhani ya kuwa wafungwa wote wametoroka. 28 Lakini Paulo akapiga kelele kum zuia, akasema, “Usijidhuru kwa maana hatujatoroka, wote tuko hapa.” 29 Askari akaitisha taa iletwe, akaingia ndani ya chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka miguuni mwa Paulo na Sila. 30 Kisha akawatoa nje akasema, “Ndugu zangu, nifanye nini ili nipate kuokoka?” 31 Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka, wewe pamoja na jamaa yako.” 32 Wakawaambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwa wanaishi nyumbani kwake. 33 Yule askari akawachukua saa ile ile akaosha majeraha yao, naye akabatizwa pamoja na wote waliokuwa nyumbani kwake. 34 Aka wachukua, akawaandalia chakula nyumbani kwake, naye akafurahi pamoja na jamaa yake kwa kuwa alikuwa amemwamini Mungu.

35 Kulipopambazuka wale mahakimu wakamtuma polisi amwambie yule askari jela, “Waachie hao watu waende zao.” 36 Yule askari jela akampasha habari Paulo akisema, “Mahakimu wametuma niwaachilie huru; kwa hiyo tokeni mwende kwa amani.” 37 Lakini Paulo akawaambia, “Wametuchapa viboko hadharani bila kufanya kesi na kutoa hukumu, na sisi ni raia wa Kirumi. Je, sasa wana taka kututoa gerezani kisiri siri? Hii si haki! Waambieni wao waje watutoe humu gerezani wenyewe.” 38 Yule askari akarudi kwa wale mahakimu kuwaeleza maneno haya, nao wakaogopa sana walipofa hamu kuwa Paulo na Sila ni raia wa Kirumi. 39 Kwa hiyo wakaja wakawaomba msamaha. Kisha wakawatoa gerezani, wakawaomba waondoke mjini. 40 Paulo na Sila walipotoka gerezani walimtembelea Lidia, wakakutana na ndugu waamini wakawatia moyo; ndipo wakaondoka.

16 Then came he to Derbe and Lystra: and, behold, a certain disciple was there, named Timotheus, the son of a certain woman, which was a Jewess, and believed; but his father was a Greek:

Which was well reported of by the brethren that were at Lystra and Iconium.

Him would Paul have to go forth with him; and took and circumcised him because of the Jews which were in those quarters: for they knew all that his father was a Greek.

And as they went through the cities, they delivered them the decrees for to keep, that were ordained of the apostles and elders which were at Jerusalem.

And so were the churches established in the faith, and increased in number daily.

Now when they had gone throughout Phrygia and the region of Galatia, and were forbidden of the Holy Ghost to preach the word in Asia,

After they were come to Mysia, they assayed to go into Bithynia: but the Spirit suffered them not.

And they passing by Mysia came down to Troas.

And a vision appeared to Paul in the night; There stood a man of Macedonia, and prayed him, saying, Come over into Macedonia, and help us.

10 And after he had seen the vision, immediately we endeavoured to go into Macedonia, assuredly gathering that the Lord had called us for to preach the gospel unto them.

11 Therefore loosing from Troas, we came with a straight course to Samothracia, and the next day to Neapolis;

12 And from thence to Philippi, which is the chief city of that part of Macedonia, and a colony: and we were in that city abiding certain days.

13 And on the sabbath we went out of the city by a river side, where prayer was wont to be made; and we sat down, and spake unto the women which resorted thither.

14 And a certain woman named Lydia, a seller of purple, of the city of Thyatira, which worshipped God, heard us: whose heart the Lord opened, that she attended unto the things which were spoken of Paul.

15 And when she was baptized, and her household, she besought us, saying, If ye have judged me to be faithful to the Lord, come into my house, and abide there. And she constrained us.

16 And it came to pass, as we went to prayer, a certain damsel possessed with a spirit of divination met us, which brought her masters much gain by soothsaying:

17 The same followed Paul and us, and cried, saying, These men are the servants of the most high God, which shew unto us the way of salvation.

18 And this did she many days. But Paul, being grieved, turned and said to the spirit, I command thee in the name of Jesus Christ to come out of her. And he came out the same hour.

19 And when her masters saw that the hope of their gains was gone, they caught Paul and Silas, and drew them into the marketplace unto the rulers,

20 And brought them to the magistrates, saying, These men, being Jews, do exceedingly trouble our city,

21 And teach customs, which are not lawful for us to receive, neither to observe, being Romans.

22 And the multitude rose up together against them: and the magistrates rent off their clothes, and commanded to beat them.

23 And when they had laid many stripes upon them, they cast them into prison, charging the jailor to keep them safely:

24 Who, having received such a charge, thrust them into the inner prison, and made their feet fast in the stocks.

25 And at midnight Paul and Silas prayed, and sang praises unto God: and the prisoners heard them.

26 And suddenly there was a great earthquake, so that the foundations of the prison were shaken: and immediately all the doors were opened, and every one's bands were loosed.

27 And the keeper of the prison awaking out of his sleep, and seeing the prison doors open, he drew out his sword, and would have killed himself, supposing that the prisoners had been fled.

28 But Paul cried with a loud voice, saying, Do thyself no harm: for we are all here.

29 Then he called for a light, and sprang in, and came trembling, and fell down before Paul and Silas,

30 And brought them out, and said, Sirs, what must I do to be saved?

31 And they said, Believe on the Lord Jesus Christ, and thou shalt be saved, and thy house.

32 And they spake unto him the word of the Lord, and to all that were in his house.

33 And he took them the same hour of the night, and washed their stripes; and was baptized, he and all his, straightway.

34 And when he had brought them into his house, he set meat before them, and rejoiced, believing in God with all his house.

35 And when it was day, the magistrates sent the serjeants, saying, Let those men go.

36 And the keeper of the prison told this saying to Paul, The magistrates have sent to let you go: now therefore depart, and go in peace.

37 But Paul said unto them, They have beaten us openly uncondemned, being Romans, and have cast us into prison; and now do they thrust us out privily? nay verily; but let them come themselves and fetch us out.

38 And the serjeants told these words unto the magistrates: and they feared, when they heard that they were Romans.

39 And they came and besought them, and brought them out, and desired them to depart out of the city.

40 And they went out of the prison, and entered into the house of Lydia: and when they had seen the brethren, they comforted them, and departed.