Mahubiri ya Injili huko Ikonio

14 Basi huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi. Wakahubiri kwa uwezo mkuu na umati mkubwa wa watu wakaamini, Wayahudi pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini wale Wayahudi ambao hawakupokea neno la Mungu, waliwa chochea watu wa mataifa dhidi ya wale walioamini. Paulo na Bar naba wakakaa huko kwa muda mrefu wakifundisha kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha kuwa mahubiri yao yalikuwa ni neno la neema yake; akawapa uwezo wa kutenda ishara na maajabu. Hata hivyo watu wa mji ule waligawanyika. Wengine wakaungana na wale Wayahudi na wengine wakawa upande wa mitume. Watu wa mataifa na Wayahudi walijiunga na baadhi ya viongozi wakafanya mpango wa kuwasumbua mitume na kisha kuwapiga mawe. Lakini wao walipopata habari hizi walitoroka wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya wilaya ya Likaonia, na sehemu zilizopakana nayo. Huko waliende lea kuhubiri Habari Njema.

Kiwete Aponywa Huko Listra

Katika mji wa Listra, alikuwepo kiwete amekaa, ambaye ali kuwa amelemaa miguu yote miwili tangu alipozaliwa, na hakuwahi kutembea kamwe. Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri, na Paulo alipomtazama aliona kuwa anayo imani ya kuponywa. 10 Kwa hiyo Paulo akasema kwa sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akaruka juu akaanza kutembea! 11 Wale watu walipoona maajabu aliyofanya Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao, wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!” 12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu. 13 Kuhani mkuu wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua aki taka kuwatolea sadaka penye lango la mji pamoja na ule umati wa watu. 14 Lakini Paulo na Barnaba waliposikia na kuona mambo haya waliyotaka kufanya, walirarua nguo zao, wakawakimbilia wale watu, wakisema, 15 ‘ ‘Kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni binadamu tu, kama ninyi! Tumekuja kuwatangazia Habari Njema; mziache hizi ibada zisizo na maana na mumgeukie Mungu aliye hai ambaye aliumba mbingu na nchi na bahari, na vyote vilivyoko. 16 Wakati wa vizazi vilivyopita aliwaachia watu waishi walivyotaka. 17 Hata hivyo hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake. Kwa maana aliwatendea mema akawaletea mvua kutoka mbinguni na mazao kwa majira yake, akawatosheleza kwa vyakula na raha.” 18 Hata pamoja na maneno yote haya haikuwa rahisi kuwazuia wale watu waache kuwatolea sadaka zao.

19 Wakaja watu kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamkokota hadi nje ya mji, wakidhani amekufa. 20 Lakini waamini walipokusanyika kumzunguka, aliamka, akarudi nao mjini. Kesho yake akaondoka na Barnaba wakaenda mpaka Derbe.

Paulo Na Barnaba Warudi Antiokia

21 Walipokwisha hubiri Habari Njema katika mji ule na watu wengi wakaamini wakawa wanafunzi, walirudi Listra na Ikonio na Antiokia. 22 Huko waliwatia nguvu wanafunzi na kuwashauri waendelee kukua katika imani. Wakawaonya wakisema, “Tunalazimika kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika mateso mengi.” 23 Na baada ya kuwachagulia wazee viongozi katika kila kanisa, wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini kwa maombi na kufunga. 24 Basi wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia. 25 Na baada ya kufundisha neno la Mungu huko Perga, walikwenda upande wa kusini hadi Atalia. 26 Kutoka huko wakasafiri kwa mashua mpaka Anti okia, ambako walikuwa wameombewa neema ya Mungu kwa kazi ambayo walikuwa wameikamilisha. 27 Walipowasili Antiokia waliwakusanya waamini pamoja wakawaeleza yale yote ambayo Mungu alikuwa amewa tendea, na jinsi Mungu alivyotoa nafasi ya imani kwa watu wasio Wayahudi. 28 Wakakaa huko na wale wanafunzi kwa muda mrefu.

In Iconium

14 At Iconium(A) Paul and Barnabas went as usual into the Jewish synagogue.(B) There they spoke so effectively that a great number(C) of Jews and Greeks believed. But the Jews who refused to believe stirred up the other Gentiles and poisoned their minds against the brothers.(D) So Paul and Barnabas spent considerable time there, speaking boldly(E) for the Lord, who confirmed the message of his grace by enabling them to perform signs and wonders.(F) The people of the city were divided; some sided with the Jews, others with the apostles.(G) There was a plot afoot among both Gentiles and Jews,(H) together with their leaders, to mistreat them and stone them.(I) But they found out about it and fled(J) to the Lycaonian cities of Lystra and Derbe and to the surrounding country, where they continued to preach(K) the gospel.(L)

In Lystra and Derbe

In Lystra there sat a man who was lame. He had been that way from birth(M) and had never walked. He listened to Paul as he was speaking. Paul looked directly at him, saw that he had faith to be healed(N) 10 and called out, “Stand up on your feet!”(O) At that, the man jumped up and began to walk.(P)

11 When the crowd saw what Paul had done, they shouted in the Lycaonian language, “The gods have come down to us in human form!”(Q) 12 Barnabas they called Zeus, and Paul they called Hermes because he was the chief speaker.(R) 13 The priest of Zeus, whose temple was just outside the city, brought bulls and wreaths to the city gates because he and the crowd wanted to offer sacrifices to them.

14 But when the apostles Barnabas and Paul heard of this, they tore their clothes(S) and rushed out into the crowd, shouting: 15 “Friends, why are you doing this? We too are only human,(T) like you. We are bringing you good news,(U) telling you to turn from these worthless things(V) to the living God,(W) who made the heavens and the earth(X) and the sea and everything in them.(Y) 16 In the past, he let(Z) all nations go their own way.(AA) 17 Yet he has not left himself without testimony:(AB) He has shown kindness by giving you rain from heaven and crops in their seasons;(AC) he provides you with plenty of food and fills your hearts with joy.”(AD) 18 Even with these words, they had difficulty keeping the crowd from sacrificing to them.

19 Then some Jews(AE) came from Antioch and Iconium(AF) and won the crowd over. They stoned Paul(AG) and dragged him outside the city, thinking he was dead. 20 But after the disciples(AH) had gathered around him, he got up and went back into the city. The next day he and Barnabas left for Derbe.

The Return to Antioch in Syria

21 They preached the gospel(AI) in that city and won a large number(AJ) of disciples. Then they returned to Lystra, Iconium(AK) and Antioch, 22 strengthening the disciples and encouraging them to remain true to the faith.(AL) “We must go through many hardships(AM) to enter the kingdom of God,” they said. 23 Paul and Barnabas appointed elders[a](AN) for them in each church and, with prayer and fasting,(AO) committed them to the Lord,(AP) in whom they had put their trust. 24 After going through Pisidia, they came into Pamphylia,(AQ) 25 and when they had preached the word in Perga, they went down to Attalia.

26 From Attalia they sailed back to Antioch,(AR) where they had been committed to the grace of God(AS) for the work they had now completed.(AT) 27 On arriving there, they gathered the church together and reported all that God had done through them(AU) and how he had opened a door(AV) of faith to the Gentiles. 28 And they stayed there a long time with the disciples.(AW)

Footnotes

  1. Acts 14:23 Or Barnabas ordained elders; or Barnabas had elders elected