Yesu Anaingia Yerusalemu Kwa Shangwe

21 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage katika mlima wa Mizeituni. Ndipo Yesu akawatuma wanafunzi wake wawili, aka waagiza, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu na mkiingia mtamwona punda amefungwa na mwanapunda pamoja naye. Wafungueni mniletee. Kama mtu akiwauliza lo lote, mwambieni, ‘Bwana anawa hitaji Haya yalitokea ili kutimiza utabiri wa nabii aliposema, ‘Mwambieni binti Sayuni, tazama mfalme wako anakuja kwako ni mnyenyekevu, na amepanda punda, mwanapunda, mtoto wa punda.’

Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya kama Yesu alivyowaagiza. Wakamleta yule punda na mwanapunda. Wakatandika mavazi yao juu ya hao punda na Yesu akaketi juu yake. Umati mkubwa wa watu wakatandika nguo zao barabarani, wengine wakakata matawi ya miti wakayatandaza barabarani. Ule umati wa watu waliomtangulia na wale waliomfuata wakapiga kelele wakisema, “Hosana kwa Mwana wa Daudi . Amebarikiwa anayekuja kwa jina la Bwana! Hosana juu mbin guni.”

10 Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote ukajawa na hekaheka, watu wakauliza, “Huyu ni nani?” 11 Ule umati wa watu wakajibu, “Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.”

Yesu Afukuza Wafanya Biashara Hekaluni

12 Yesu aliingia katika eneo la Hekalu akawafukuza wote wali okuwa wakinunua na kuuza vitu Hekaluni. Akazipindua meza za watu waliokuwa wakibadilisha fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa. 13 Akawaambia, “Imeandikwa katika Maandiko, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeigeuza kuwa pango la wanyang’anyi.”

14 Vipofu na vilema wakamwendea, naye akawaponya. 15 Lakini makuhani wakuu na walimu wa sheria waliudhika walipoona mambo ya ajabu aliyoyafanya na kuwasikia watoto wakishangilia Hekaluni wakisema, “Hosana kwa Mwana wa Daudi!” Wakamwuliza Yesu, 16 “Unasikia hawa wanavyosema?” Akawajibu, “Nasikia. Kwani hamjasoma maneno haya, ‘Kutoka katika vinywa vya watoto wadogo na wale wanaonyonya umeleta sifa kamili’? ” 17 Akawaacha akatoka nje ya mji, akaenda hadi Bethania, akalala huko.

18 Asubuhi, Yesu alipokuwa akirudi mjini, aliona njaa. 19 Alipoona mtini kando ya bara bara aliusogelea akakuta hauna tunda lo lote ila majani tu. Akaulaani akisema, “Usizae matunda kamwe!” Wakati huo huo ule mtini ukanyauka. 20 Wanafunzi wake wakashangazwa na tukio hilo wakamwuliza, “Imekuwaje mtini huu ukanyauka ghafla?” 21 Yesu akawajibu, “Nawaambia kweli, kama mna imani na msiwe na mashaka hata kidogo, mtaweza kufanya yaliy ofanyika kwa huu mtini; na hata mkiuambia mlima huu, ‘Ng’oka, nenda kajitupe baharini,’ itafanyika. 22 Na lo lote mtakaloomba katika sala, mtapewa, kama mna imani.”

Yesu Aulizwa Kuhusu Mamlaka Yake

23 Yesu alipoingia tena Hekaluni, makuhani wakuu na wazee walimjia alipokuwa akifundisha, wakamwuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani na ni nani amekupa mamlaka hayo?” 24 Yesu akawajibu, “Na mimi nitawauliza swali na mkinijibu nami nita waambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya. 25 Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi? Mbinguni au kwa watu?” Wakaanza kubishana kati yao wakisema, “Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, ‘Mbona basi hamkumwamini?’ 26 Lakini tukisema ulitoka kwa wanadamu, tunaogopa hawa watu, maana wote wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.” 27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Hatufahamu.” Naye aka waambia, “Nami sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”

Mfano Wa Wana Wawili

28 ‘Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na watoto wawili wa kiume. Akamwendea yule wa kwanza akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’ 29 Yule mwanae akasema, ‘Siendi,’ lakini baadaye akabadili mawazo akaenda. 30 Kisha yule baba akamwendea yule mwanae mwingine akamwambia vile vile. Yeye akajibu, ‘Nitakwenda baba,’ lakini asiende. 31 Ni yupi kati yao aliyetimiza alivyotaka baba yake?” Wakamjibu, “Yule wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Nawaambieni kweli, watoza ushuru na makahaba wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa Mungu.

32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, lakini hamkumwamini, ila watoza ushuru na makahaba walimwamini. Nanyi hata mlipoona hayo, baadaye hamkutubu na kum wamini.”

Mfano Wa Wapangaji Waovu

33 “Sikilizeni mfano mwingine: mtu mmoja mwenye shamba alilima shamba akapanda mizabibu. Akalizungushia ua, na ndani yake akachimba kisima cha kusindikia zabibu; na akajenga mnara. Kisha akalikodisha hilo shamba kwa wakulima fulani, akasafiri kwenda nchi nyingine.

34 “Wakati wa mavuno ulipokaribia aliwatuma watumishi wake kwa hao wakulima kupokea mavuno yake. 35 Wale wakulima wakawaka mata wale watumishi; wakampiga mmoja, wakamwua mwingine na kum piga mawe mwingine. 36 Akatuma watumishi wengine, wengi kuliko wale wa mwanzo. Wale wakulima wakawatendea vile vile. 37 Mwish owe akamtuma mwanae kwao akisema, ‘Bila shaka watamheshimu mwa nangu.’ 38 Lakini walipomwona mwanae, waliambiana, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumwue tuchukue urithi wake.’ 39 Basi wakamchu kua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. 40 Sasa, akija yule mwenye shamba, mnadhani atawafanya nini hao waku lima?” 41 Wakamjibu, “Atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na kulipangisha shamba lake kwa wakulima wengine ambao watampatia matunda yake wakati wa mavuno.”

42 Yesu akawaambia, “Hamjapata kusoma katika Maandiko kwamba: ‘Lile jiwe walilokataa wajenzi limekuwa jiwe kuu la pembeni; Bwana ndiye amefanya jambo hili nalo ni zuri ajabu machoni petu’?

43 Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na watapewa watu wawezao kutoa matunda yake.” [ 44 “Na ambaye ataanguka kwenye jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagika sagika.”]

45 Makuhani wakuu na Mafarisayo waliposikia mifano yake, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao. 46 Wakatafuta njia ya kumkamata lakini waliogopa ule umati wa watu kwa kuwa wao walim tambua Yesu kuwa nabii.

21 And when they drew nigh unto Jerusalem, and were come to Bethphage, unto the mount of Olives, then sent Jesus two disciples,

Saying unto them, Go into the village over against you, and straightway ye shall find an ass tied, and a colt with her: loose them, and bring them unto me.

And if any man say ought unto you, ye shall say, The Lord hath need of them; and straightway he will send them.

All this was done, that it might be fulfilled which was spoken by the prophet, saying,

Tell ye the daughter of Sion, Behold, thy King cometh unto thee, meek, and sitting upon an ass, and a colt the foal of an ass.

And the disciples went, and did as Jesus commanded them,

And brought the ass, and the colt, and put on them their clothes, and they set him thereon.

And a very great multitude spread their garments in the way; others cut down branches from the trees, and strawed them in the way.

And the multitudes that went before, and that followed, cried, saying, Hosanna to the son of David: Blessed is he that cometh in the name of the Lord; Hosanna in the highest.

10 And when he was come into Jerusalem, all the city was moved, saying, Who is this?

11 And the multitude said, This is Jesus the prophet of Nazareth of Galilee.

12 And Jesus went into the temple of God, and cast out all them that sold and bought in the temple, and overthrew the tables of the moneychangers, and the seats of them that sold doves,

13 And said unto them, It is written, My house shall be called the house of prayer; but ye have made it a den of thieves.

14 And the blind and the lame came to him in the temple; and he healed them.

15 And when the chief priests and scribes saw the wonderful things that he did, and the children crying in the temple, and saying, Hosanna to the son of David; they were sore displeased,

16 And said unto him, Hearest thou what these say? And Jesus saith unto them, Yea; have ye never read, Out of the mouth of babes and sucklings thou hast perfected praise?

17 And he left them, and went out of the city into Bethany; and he lodged there.

18 Now in the morning as he returned into the city, he hungered.

19 And when he saw a fig tree in the way, he came to it, and found nothing thereon, but leaves only, and said unto it, Let no fruit grow on thee henceforward for ever. And presently the fig tree withered away.

20 And when the disciples saw it, they marvelled, saying, How soon is the fig tree withered away!

21 Jesus answered and said unto them, Verily I say unto you, If ye have faith, and doubt not, ye shall not only do this which is done to the fig tree, but also if ye shall say unto this mountain, Be thou removed, and be thou cast into the sea; it shall be done.

22 And all things, whatsoever ye shall ask in prayer, believing, ye shall receive.

23 And when he was come into the temple, the chief priests and the elders of the people came unto him as he was teaching, and said, By what authority doest thou these things? and who gave thee this authority?

24 And Jesus answered and said unto them, I also will ask you one thing, which if ye tell me, I in like wise will tell you by what authority I do these things.

25 The baptism of John, whence was it? from heaven, or of men? And they reasoned with themselves, saying, If we shall say, From heaven; he will say unto us, Why did ye not then believe him?

26 But if we shall say, Of men; we fear the people; for all hold John as a prophet.

27 And they answered Jesus, and said, We cannot tell. And he said unto them, Neither tell I you by what authority I do these things.

28 But what think ye? A certain man had two sons; and he came to the first, and said, Son, go work to day in my vineyard.

29 He answered and said, I will not: but afterward he repented, and went.

30 And he came to the second, and said likewise. And he answered and said, I go, sir: and went not.

31 Whether of them twain did the will of his father? They say unto him, The first. Jesus saith unto them, Verily I say unto you, That the publicans and the harlots go into the kingdom of God before you.

32 For John came unto you in the way of righteousness, and ye believed him not: but the publicans and the harlots believed him: and ye, when ye had seen it, repented not afterward, that ye might believe him.

33 Hear another parable: There was a certain householder, which planted a vineyard, and hedged it round about, and digged a winepress in it, and built a tower, and let it out to husbandmen, and went into a far country:

34 And when the time of the fruit drew near, he sent his servants to the husbandmen, that they might receive the fruits of it.

35 And the husbandmen took his servants, and beat one, and killed another, and stoned another.

36 Again, he sent other servants more than the first: and they did unto them likewise.

37 But last of all he sent unto them his son, saying, They will reverence my son.

38 But when the husbandmen saw the son, they said among themselves, This is the heir; come, let us kill him, and let us seize on his inheritance.

39 And they caught him, and cast him out of the vineyard, and slew him.

40 When the lord therefore of the vineyard cometh, what will he do unto those husbandmen?

41 They say unto him, He will miserably destroy those wicked men, and will let out his vineyard unto other husbandmen, which shall render him the fruits in their seasons.

42 Jesus saith unto them, Did ye never read in the scriptures, The stone which the builders rejected, the same is become the head of the corner: this is the Lord's doing, and it is marvellous in our eyes?

43 Therefore say I unto you, The kingdom of God shall be taken from you, and given to a nation bringing forth the fruits thereof.

44 And whosoever shall fall on this stone shall be broken: but on whomsoever it shall fall, it will grind him to powder.

45 And when the chief priests and Pharisees had heard his parables, they perceived that he spake of them.

46 But when they sought to lay hands on him, they feared the multitude, because they took him for a prophet.