Yesu Afufuka Kutoka Kwa Wafu

16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena na Mariamu mama yake Yakobo na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu. Asubuhi na mapema, siku ya Jumapili, walikwenda kaburini jua likiwa linaanza kuchomoza. Njiani wakawa wanaulizana, “Ni nani atatuondolea lile jiwe kwenye mlango wa kaburi?” Lakini walipotazama, wakaona jiwe lile, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha ondolewa.

Walipoingia kaburini, walimwona kijana amekaa upande wa kulia akiwa amevaa vazi jeupe. Wakashtuka. Yule mtu akawaambia, “Msishtuke. Mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa! Tazameni mahali alipokuwa amelazwa.

Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, kwamba anatangulia kwenda Galilaya na huko mtamwona, kama alivyowaam bia.” Wale wanawake wakiwa wanashangaa na kutetemeka kwa hofu, wakatoka pale kaburini mbio! Hawakumweleza mtu ye yote jambo lo lote kwa maana walikuwa wanaogopa.

Yesu Anamtokea Mariamu Magdalena

Baada ya Yesu kufufuka, alimtokea kwanza Mariamu Mag dalena, yule aliyemtoa pepo saba. 10 Mariamu akaenda akawaambia wale waliokuwa wakifuatana na Yesu. Wakati huo walikuwa bado wanalia na kuomboleza. 11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Mariamu alikuwa amemwona, hawakuamini.

Yesu Awatokea Wanafunzi Wawili

12 Baadaye Yesu aliwatokea kwa namna nyingine wanafunzi wawili walipokuwa wakienda shamba. 13 Nao pia walirudi wakawaam bia wenzao. Lakini pia hawakuamini.

Yesu Anawatokea Wale Wanafunzi Kumi Na Mmoja

14 Mwishowe, Yesu aliwatokea wale wanafunzi kumi na mmoja, wakiwa wanakula chakula. Akawakemea kwa kutokuamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao uliowafanya wakatae kuwasadiki wale waliomwona baada ya kufufuka.

15 Akawaambia, “Nendeni ulimwenguni kote, mkawahubirie watu wote Habari Njema. 16 Ye yote atakayeamini na kubatizwa ataoko lewa. Lakini ye yote ambaye atakataa kuamini, atahukumiwa.

17 “Na hizi ndizo ishara zitakazoandamana na wale wata kaoamini: Kwa kutumia jina langu watafukuza pepo; watasema kwa lugha mpya; 18 wataweza hata kuwakamata nyoka na kunywa sumu lakini wasidhurike; watawawekea wagonjwa mikono, nao watapona.”

Yesu Apaa Kwenda Mbinguni

19 Yesu alipokwisha kuwaambia maneno haya, alichukuliwa juu mbinguni, akaketi upande wa kulia wa Mungu.

16 And when the sabbath was past, Mary Magdalene, and Mary the mother of James, and Salome, had bought sweet spices, that they might come and anoint him.

And very early in the morning the first day of the week, they came unto the sepulchre at the rising of the sun.

And they said among themselves, Who shall roll us away the stone from the door of the sepulchre?

And when they looked, they saw that the stone was rolled away: for it was very great.

And entering into the sepulchre, they saw a young man sitting on the right side, clothed in a long white garment; and they were affrighted.

And he saith unto them, Be not affrighted: Ye seek Jesus of Nazareth, which was crucified: he is risen; he is not here: behold the place where they laid him.

But go your way, tell his disciples and Peter that he goeth before you into Galilee: there shall ye see him, as he said unto you.

And they went out quickly, and fled from the sepulchre; for they trembled and were amazed: neither said they any thing to any man; for they were afraid.

Now when Jesus was risen early the first day of the week, he appeared first to Mary Magdalene, out of whom he had cast seven devils.

10 And she went and told them that had been with him, as they mourned and wept.

11 And they, when they had heard that he was alive, and had been seen of her, believed not.

12 After that he appeared in another form unto two of them, as they walked, and went into the country.

13 And they went and told it unto the residue: neither believed they them.

14 Afterward he appeared unto the eleven as they sat at meat, and upbraided them with their unbelief and hardness of heart, because they believed not them which had seen him after he was risen.

15 And he said unto them, Go ye into all the world, and preach the gospel to every creature.

16 He that believeth and is baptized shall be saved; but he that believeth not shall be damned.

17 And these signs shall follow them that believe; In my name shall they cast out devils; they shall speak with new tongues;

18 They shall take up serpents; and if they drink any deadly thing, it shall not hurt them; they shall lay hands on the sick, and they shall recover.

19 So then after the Lord had spoken unto them, he was received up into heaven, and sat on the right hand of God.

20 And they went forth, and preached every where, the Lord working with them, and confirming the word with signs following. Amen.