Add parallel Print Page Options

Gavana Pilato Amhoji Yesu

(Mt 27:1-2,11-14; Mk 15:1-5; Yh 18:28-38)

23 Kisha kundi lote likasimama, wakampeleka Yesu kwa Pilato. Wakaanza kumshitaki Yesu na kumwambia Pilato, “Tumemkamata mtu huyu akijaribu kuwapotosha watu wetu. Anasema tusilipe kodi kwa Kaisari. Anajiita Masihi, mfalme.”

Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni mfalme wa Wayahudi?”

Yesu akajibu, “Ndiyo, unaweza kusema hivyo.”

Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na watu, “Sioni kosa lolote kwa mtu huyu.”

Lakini waliendelea kusema, “Mafundisho yake yanasababisha matatizo katika Uyahudi yote. Alianzia Galilaya na sasa yupo hapa!”

Read full chapter