Yesu Azungumzia Tena Juu Ya Kifo Chake

18 Yesu akawachukua wale wanafunzi wake kumi na wawili kando akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na yote yaliy oandikwa na manabii kunihusu mimi Mwana wa Adamu yatatimia. Akawaambia, “Katika mji mmoja alikuwapo hakimu ambaye hakumwogopa Mungu wala kumjali mtu. Na alikuwapo mjane mmoja katika mji huo ambaye alikuwa akija kwake mara kwa mara akimwomba, ‘Tafadhali niamulie haki kati yangu na adui yangu.’ Kwa muda mrefu yule hakimu hakufanya lo lote. Lakini hatimaye akasema moyoni mwake, ‘Simwogopi Mungu wala simjali mtu lakini kwa kuwa huyu mjane ananisumbua na kesi yake, nitamwamulia haki asije akanichosha kwa kuja kwake mara kwa mara.”’ Bwana akasema, “Mnasikia asemavyo huyu hakimu dhalimu. Na Mungu je, hatawatendea haki watu wake wanaomlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwapa msaada? Nina waambieni atahakikisha amewatendea haki upesi. Lakini je, mimi Mwana wa Adamu nitakaporudi duniani nitakuta watu wanadumu katika imani?”

Mfano Wa Farisayo Na Mtoza Ushuru

Yesu alitoa mfano huu kwa ajili ya wale waliojiona kuwa wao ni wenye haki na kuwadharau wengine. 10 Watu wawili walikwenda hekaluni kusali, mmoja wao alikuwa Farisayo na mwingine alikuwa mtoza ushuru. 11 yule Farisayo alisimama akasali kimoyomoyo. ‘Ninakushukuru Mungu kwa sababu mimi si kama watu wengine: wany ang’anyi, wadhalimu, wazinzi, au kama huyu mtoza ushuru. 12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma na kutoa sehemu ya kumi ya mapato yangu.’ 13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali. Hakuthubutu hata kuinua uso wake kutazama mbinguni; bali alijipiga kifuani kwa majuto akasema, ‘Mungu, nihurumie, mimi mwenye dhambi.’

14 Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki mbele za Mungu na wala si yule Farisayo. Kwa maana ye yote ajikwezaye atashushwa na ye yote ajinyenyekezaye, atainuliwa.”

Yesu Awabariki Watoto Wadogo

15 Watu wakamletea Yesu watoto wao wachanga ili awaguse. Wanafunzi walipowaona, wakawakemea. 16 Lakini Yesu akawaita wale watoto waje kwake, akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu walio kama hawa watoto. 17 Nawaambia hakika, ye yote ambaye hataupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”

18 Kiongozi mmoja akamwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

19 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema ila Mungu peke yake. 20 Unazifahamu amri: ‘Usizini, usiue, usiibe, usishuhudie uongo, waheshimu baba yako na mama yako?”’ 21 Akajibu, “Amri zote hizi nimezishika tangu utoto wangu.”

22 Yesu aliposikia haya, akamwambia, “Bado unahitaji kufa nya jambo moja. Nenda ukauze vitu vyote ulivyo navyo, uwagawie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.” 23 Aliposikia hayo alisikitika, kwa maana alikuwa tajiri sana.

24 Yesu alipoona yule kiongozi amesikitika, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu! 25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.” 26 Wale waliosi kia hayo wakauliza, “Kama ni hivyo, ni nani basi awezaye kuoko lewa?” 27 Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu yaweze kana kwa Mungu.” 28 Ndipo Petro akasema, “Sisi je? Tumeacha vyote tulivyokuwanavyo tukakufuata!” 29 Yesu akajibu, “Nawaam bia hakika, hakuna hata mmoja aliyeacha nyumba yake, au mke, ndugu, wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, 30 ambaye hatapewa na Mungu mara nyingi zaidi ya hivyo katika maisha haya na kupata uzima wa milele katika maisha yajayo.” 32 Nitatiwa mikononi mwa watawala wa Kirumi. Watu watanizomea, watanitukana na kunitemea mate. 33 Watanipiga na kuniua, lakini siku ya tatu nitafufuka.”

34 Wanafunzi wake hawakuelewa mambo haya. Maana ya maneno haya ilikuwa imefichika kwao, nao hawakujua Yesu alikuwa anazun gumzia nini.

Yesu Amponya Kipofu

35 Yesu na wafuasi wake walipokaribia Yeriko, walimpita kipofu mmoja aliyekuwa amekaa kando ya njia, akiomba fedha. 36 Kipofu huyo aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?” 37 Wakamwambia, “Yesu Mnazareti anapita.” 38 Akaita kwa sauti kuu, “Yesu, Mwana wa Daudi! Nionee huruma!” 39 Wale waliokuwa wakiongoza msafara wakamkemea wakamwambia akae kimya. Lakini yeye akapiga kelele zaidi, “Mwana wa Daudi! Nionee huruma!”

40 Yesu akasimama, akaagiza huyo mtu aletwe kwake. Alipo karibia, Yesu akamwuliza, 41 “Unataka nikufanyie nini?” Aka jibu, “Bwana, nataka kuona.”

42 Yesu akamwambia, “Basi upate kuona; imani yako imekupo nya.” 43 Akaweza kuona mara hiyo hiyo akamfuata Yesu, huku akimsifu Mungu. Watu wote walioshuhudia mambo hayo, nao wakamsifu Mungu.

18 And he spake a parable unto them to this end, that men ought always to pray, and not to faint;

Saying, There was in a city a judge, which feared not God, neither regarded man:

And there was a widow in that city; and she came unto him, saying, Avenge me of mine adversary.

And he would not for a while: but afterward he said within himself, Though I fear not God, nor regard man;

Yet because this widow troubleth me, I will avenge her, lest by her continual coming she weary me.

And the Lord said, Hear what the unjust judge saith.

And shall not God avenge his own elect, which cry day and night unto him, though he bear long with them?

I tell you that he will avenge them speedily. Nevertheless when the Son of man cometh, shall he find faith on the earth?

And he spake this parable unto certain which trusted in themselves that they were righteous, and despised others:

10 Two men went up into the temple to pray; the one a Pharisee, and the other a publican.

11 The Pharisee stood and prayed thus with himself, God, I thank thee, that I am not as other men are, extortioners, unjust, adulterers, or even as this publican.

12 I fast twice in the week, I give tithes of all that I possess.

13 And the publican, standing afar off, would not lift up so much as his eyes unto heaven, but smote upon his breast, saying, God be merciful to me a sinner.

14 I tell you, this man went down to his house justified rather than the other: for every one that exalteth himself shall be abased; and he that humbleth himself shall be exalted.

15 And they brought unto him also infants, that he would touch them: but when his disciples saw it, they rebuked them.

16 But Jesus called them unto him, and said, Suffer little children to come unto me, and forbid them not: for of such is the kingdom of God.

17 Verily I say unto you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child shall in no wise enter therein.

18 And a certain ruler asked him, saying, Good Master, what shall I do to inherit eternal life?

19 And Jesus said unto him, Why callest thou me good? none is good, save one, that is, God.

20 Thou knowest the commandments, Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Honour thy father and thy mother.

21 And he said, All these have I kept from my youth up.

22 Now when Jesus heard these things, he said unto him, Yet lackest thou one thing: sell all that thou hast, and distribute unto the poor, and thou shalt have treasure in heaven: and come, follow me.

23 And when he heard this, he was very sorrowful: for he was very rich.

24 And when Jesus saw that he was very sorrowful, he said, How hardly shall they that have riches enter into the kingdom of God!

25 For it is easier for a camel to go through a needle's eye, than for a rich man to enter into the kingdom of God.

26 And they that heard it said, Who then can be saved?

27 And he said, The things which are impossible with men are possible with God.

28 Then Peter said, Lo, we have left all, and followed thee.

29 And he said unto them, Verily I say unto you, There is no man that hath left house, or parents, or brethren, or wife, or children, for the kingdom of God's sake,

30 Who shall not receive manifold more in this present time, and in the world to come life everlasting.

31 Then he took unto him the twelve, and said unto them, Behold, we go up to Jerusalem, and all things that are written by the prophets concerning the Son of man shall be accomplished.

32 For he shall be delivered unto the Gentiles, and shall be mocked, and spitefully entreated, and spitted on:

33 And they shall scourge him, and put him to death: and the third day he shall rise again.

34 And they understood none of these things: and this saying was hid from them, neither knew they the things which were spoken.

35 And it came to pass, that as he was come nigh unto Jericho, a certain blind man sat by the way side begging:

36 And hearing the multitude pass by, he asked what it meant.

37 And they told him, that Jesus of Nazareth passeth by.

38 And he cried, saying, Jesus, thou son of David, have mercy on me.

39 And they which went before rebuked him, that he should hold his peace: but he cried so much the more, Thou son of David, have mercy on me.

40 And Jesus stood, and commanded him to be brought unto him: and when he was come near, he asked him,

41 Saying, What wilt thou that I shall do unto thee? And he said, Lord, that I may receive my sight.

42 And Jesus said unto him, Receive thy sight: thy faith hath saved thee.

43 And immediately he received his sight, and followed him, glorifying God: and all the people, when they saw it, gave praise unto God.