Add parallel Print Page Options

Yesu Atembea Juu ya Maji

(Mt 14:22-27; Mk 6:45-52)

16 Jioni ile wafuasi wake wakashuka kwenda ziwani. 17 Ilikuwa giza sasa, wakati huo Yesu hakuwa pamoja na wafuasi wake. Wakapanda kwenye mashua na kuanza safari kuvuka ziwa kwenda Kapernaumu. 18 Upepo ulikuwa unavuma kwa nguvu sana. Mawimbi ziwani yakawa makubwa. 19 Wakaiendesha mashua kiasi cha kilomita tano au sita. Kisha wakamwona Yesu. Yeye alikuwa anatembea juu ya maji, akiifuata mashua. Nao wakaogopa. 20 Lakini Yesu akawaambia, “Msiogope. Ni mimi.” 21 Baada ya kusema hivyo, wakamkaribisha kwenye mashua. Kisha mashua ikafika ufukweni katika sehemu waliyotaka kwenda.

Read full chapter

Yesu Atembea Juu Ya Maji

16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kuelekea ziwani. 17 Wakaingia katika mashua, wakaanza kuvuka kwenda Kap ernaumu. Wakati huo giza lilikuwa limeanza kuingia na Yesu ali kuwa hajatokea bado.

18 Wakati huo upepo mkali ulikuwa unavuma na bahari ikaanza kuchafuka. 19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo upatao kar ibu kilometa nane, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikari bia mashua! Wakaogopa sana. 20 Lakini Yesu akawaambia, “ Ni mimi; msiogope.” 21 Ndipo wakafurahi, wakamkaribisha kwenye mashua, na mara wakafika walipokuwa wanakwenda.

Read full chapter