Yesu Atembea Juu Ya Maji

16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kuelekea ziwani. 17 Wakaingia katika mashua, wakaanza kuvuka kwenda Kap ernaumu. Wakati huo giza lilikuwa limeanza kuingia na Yesu ali kuwa hajatokea bado.

18 Wakati huo upepo mkali ulikuwa unavuma na bahari ikaanza kuchafuka. 19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo upatao kar ibu kilometa nane, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikari bia mashua! Wakaogopa sana. 20 Lakini Yesu akawaambia, “ Ni mimi; msiogope.” 21 Ndipo wakafurahi, wakamkaribisha kwenye mashua, na mara wakafika walipokuwa wanakwenda.

Read full chapter