Add parallel Print Page Options

Yesu Awalisha Watu Zaidi ya 5,000

(Mt 14:13-21; Mk 6:30-44; Lk 9:10-17)

Baadaye, Yesu akavuka Ziwa Galilaya (ambalo pia linaitwa Ziwa Tiberia). Umati mkubwa wa watu ukamfuata kwa sababu waliona ishara za miujiza alizofanya kwa kuponya wagonjwa. Yesu akapanda mlimani na kukaa pale pamoja na wafuasi wake. Siku hizo sherehe ya Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.

Yesu akainua macho yake na kuuona umati wa watu ukija kwake. Akamwambia Filipo, “Tunaweza kununua wapi mikate ya kuwatosha watu hawa wote?” Alimwuliza Filipo swali hili ili kumjaribu. Yesu alikwishajua kile alichopanga kufanya.

Filipo akajibu, “Wote tunapaswa kufanya kazi kwa mwezi mmoja ili kununua mikate ya kutosha na kumpa kila mmoja aliyepo angalau kipande kidogo.”

Mfuasi mwingine aliyekuwepo alikuwa Andrea, ndugu yake Simoni Petro. Andrea akasema, “Yupo hapa kijana mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wadogo wawili. Lakini hiyo haitoshi kwa umati huu wa watu.”

10 Yesu akasema, “Mwambieni kila mtu akae chini.” Sehemu hiyo ilikuwa yenye nyasi nyingi, na wanaume wapatao 5,000 walikaa hapo. 11 Yesu akaichukua ile mikate akamshukuru Mungu kwa ajili ya hiyo. Kisha akawapa watu waliokuwa wakisubiri kula. Alifanya vivyo hivyo kwa samaki. Akawapa watu kadiri walivyohitaji.

12 Wote hao wakawa na chakula cha kutosha. Walipomaliza kula, Yesu akawaambia wafuasi wake, “Kusanyeni vipande vya samaki vilivyobaki na mikate ambayo haikuliwa. Msipoteze chochote.” 13 Hivyo wakakusanya vipande vilivyobaki wakajaza vikapu 12 vikubwa vya mikate ya ngano iliyowabakia wale waliokula. Watu walikuwa wameanza kula wakiwa na vipande vitano tu vya mikate ya ngano.

14 Watu waliiona ishara hii aliyoifanya Yesu na kusema, “Huyu atakuwa ndiye yule Nabii[a] anayekuja ulimwenguni!”

Read full chapter

Footnotes

  1. 6:14 Nabii Huenda walikuwa na maana nabii ambaye Mungu, alimwambia Musa ya kwamba atamtuma. Tazama Kum 18:15-19.

Yesu Alisha Watu Elfu Tano

Baadaye, Yesu alivuka hadi ng’ambo ya pili ya ziwa la Gali laya, ambalo pia huitwa bahari ya Tiberia. Watu wengi walikuwa wakimfuata kwa sababu walikuwa wamemwona akiponya wagonjwa kwa njia za ajabu. Yesu alikwenda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.

Yesu alipotazama aliona umati mkubwa wa watu wanamfuata. Akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ya kuwalisha watu hawa?” Alisema hivi kumjaribu Filipo maana yeye mwenyewe ali jua atakalofanya.

Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili, hazitoshi kununua mikate ya kuwapatia watu hawa japo kila mtu apate kipande kidogo.”

Mmoja wa wanafunzi wake, aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akasema, “Kuna mvulana mmoja ana mikate mitano na samaki wawili. Lakini hivi vitafaa nini kwa umati wote huu?”

10 Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Zilikuwapo nyasi nyingi mahali hapo, kwa hiyo watu wapatao elfu tano wal iweza kukaa chini. 11 Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia wale watu waliokuwa wamekaa. Akawagawia pia na hao samaki wawili, kila mtu kiasi alichotaka. 12 Watu wote wali pokwisha kula kiasi cha kutosha, aliwaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vipande vilivyobaki, kisipotee kipande cho chote.” 13 Basi wakakusanya vipande vya ile mikate mitano, wakajaza vikapu kumi na viwili.

14 Watu walipoona muujiza huu alioufanya Yesu, wakasema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii tuliyekuwa tukimtazamia!”

Read full chapter