Kutoka kwa Paulo, Silvano na Timotheo. Kwa kanisa la Wathes alonike mlio wa Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo. Tuna watakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo.

Sala Na Shukrani

Hatuna budi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu wapendwa; na ndivyo inavyostahili kwa sababu imani yenu inaongezeka zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu kwa mwen zake unazidi kuongezeka. Ndio maana sisi tunajivuna kwa ajili yenu miongoni mwa makanisa ya Mungu. Tunajivuna juu ya uvumilivu wenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazopata.

Haya yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki na kwa sababu hiyo ninyi mtastahili kupata Ufalme wa Mungu ambao mnateswa kwa ajili yake. Mungu ni wa haki: atawalipa kwa mateso wale wanaowatesa ninyi na kuwapeni ninyi mnaoteseka nafuu pamoja na sisi pia. Haya yatatokea wakati Bwana Yesu atakapodhi hirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu. Atawahukumu wale wasiomjua Mungu, wasioitii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu. Wataadhibiwa kwa kuangamizwa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake, 10 siku ile atakapokuja kutukuzwa kwa ajili ya watakatifu wake na kustaajabiwa na watu wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa mion goni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.

11 Kwa sababu hii tunawaombeeni bila kukoma, kwamba Mungu awahesabu kuwa mnastahili maisha aliyowaitia na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila nia njema mliyo nayo na kila tendo linalotokana na imani yenu. 12 Tunaomba hivi ili jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe kwa ajili yenu nanyi mtukuzwe kwa ajili yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.

Salamu kutoka kwa Paulo, Sila na Timotheo.

Kwa kanisa la Thesalonike lililo mali ya Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.

Neema na amani viwe kwenu kutoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo.

Kaka na dada zetu, tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu. Na hivyo ndivyo tunavyopaswa kufanya, kwani mnatupa sababu ya kushukuru na imani yenu inakua zaidi na zaidi. Pamoja na hilo upendo ambao kila mmoja wenu anao kwa mwenzake nao unakua. Hivyo tunayaeleza makanisa mengine ya Mungu namna tunavyojivuna kuhusu ninyi. Tunawaeleza jinsi mlivyoendelea kwa subira kuwa imara na waaminifu, ingawa mnateswa na kusumbuliwa na matatizo mengi.

Mungu Atafanya Mambo Kuwa Sawa

Huu ni uthibitisho kwamba Mungu ni wa haki katika hukumu zake. Hutaka kuwastahilisha katika ufalme wake. Kuteswa kwenu ni kwa ajili ya ufalme huo. Ni haki kwa Mungu kuwaadhibu wale wanaowaletea matatizo. Atawaletea unafuu wanaoteseka. Atawaletea ninyi nasi unafuu huo atakapokuja Bwana Yesu kutoka mbinguni ili wote wamwone, pamoja na malaika wake wenye nguvu zilizotukuka. Atakuja na moto unaoteketeza kuwaadhibu wasiomjua Mungu na wanaokataa kuitii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu. Wataadhibiwa na maangamizi yasio na mwisho. Hawataruhusiwa kuwa na Bwana lakini watatengwa mbali na nguvu zake za utukufu. 10 Hii itatokea siku ambapo Bwana Yesu atakuja na kupokea heshima miongoni mwa watu wake watakatifu. Na wote wanaomwamini watamstaajabu. Na hii inawajumuisha ninyi kwa sababu mliamini yale tuliyowaambia.

11 Hii ndiyo sababu daima tunawaombea. Tunamwomba Mungu wetu awasaidie kuishi katika njia njema aliyoitaka alipowachagua. Wema mlionao unawafanya mtake kufanya mema. Na imani mliyonayo inafanya mfanye kazi. Tunaomba kwamba kupitia nguvu zake Mungu atayakamilisha yote mema mliyokusudia kufanya pamoja na kazi zote zinazotokana na imani yenu. 12 Kisha jina la Bwana wetu Yesu litaheshimiwa kwa sababu yenu, nanyi mtaheshimiwa kwa sababu yake, na mtaheshimiwa kwa sababu yake. Hii inaweza kutokea tu kwa neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.

Paul, Silas[a](A) and Timothy,(B)

To the church of the Thessalonians(C) in God our Father and the Lord Jesus Christ:

Grace and peace to you from God the Father and the Lord Jesus Christ.(D)

Thanksgiving and Prayer

We ought always to thank God for you,(E) brothers and sisters,[b] and rightly so, because your faith is growing more and more, and the love all of you have for one another is increasing.(F) Therefore, among God’s churches we boast(G) about your perseverance and faith(H) in all the persecutions and trials you are enduring.(I)

All this is evidence(J) that God’s judgment is right, and as a result you will be counted worthy(K) of the kingdom of God, for which you are suffering. God is just:(L) He will pay back trouble to those who trouble you(M) and give relief to you who are troubled, and to us as well. This will happen when the Lord Jesus is revealed from heaven(N) in blazing fire(O) with his powerful angels.(P) He will punish(Q) those who do not know God(R) and do not obey the gospel of our Lord Jesus.(S) They will be punished with everlasting destruction(T) and shut out from the presence of the Lord(U) and from the glory of his might(V) 10 on the day(W) he comes to be glorified(X) in his holy people and to be marveled at among all those who have believed. This includes you, because you believed our testimony to you.(Y)

11 With this in mind, we constantly pray for you,(Z) that our God may make you worthy(AA) of his calling,(AB) and that by his power he may bring to fruition your every desire for goodness(AC) and your every deed prompted by faith.(AD) 12 We pray this so that the name of our Lord Jesus may be glorified in you,(AE) and you in him, according to the grace of our God and the Lord Jesus Christ.[c]

Footnotes

  1. 2 Thessalonians 1:1 Greek Silvanus, a variant of Silas
  2. 2 Thessalonians 1:3 The Greek word for brothers and sisters (adelphoi) refers here to believers, both men and women, as part of God’s family; also in 2:1, 13, 15; 3:1, 6, 13.
  3. 2 Thessalonians 1:12 Or God and Lord, Jesus Christ