Maono Ya Paulo Na Mwiba Aliokuwa Nao

12 Inanibidi nijisifu. Ingawa hakuna faida, nitawaeleza juu ya maono na mafunuo niliyopata kutoka kwa Bwana. Namfahamu mtu aliyekuwa ndani ya Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alijikuta katika mbingu ya tatu. Kama alikuwa katika mwili au katika roho mimi sijui, Mungu anajua. Na ninafahamu ya kuwa huyu mtu alijikuta yuko Paradiso, kama alikuwa katika mwili au katika roho mimi sijui, Mungu anajua. Naye alisikia mambo ambayo hayawezi kusimuliwa, ambayo mtu hawezi kuyatamka. Kwa niaba ya mtu huyu nitajisifu, lakini kwa ajili yangu mwenyewe sitajisifu isipokuwa kuhusu udhaifu wangu. Lakini ningependa kujisifu, sitakuwa mjinga kwa maana nitakuwa nasema kweli. Ila najizuia, ili mtu ye yote asije akaniona mimi kuwa bora zaidi kuliko ninavyoonekana katika yale ninayotenda na kusema.

Na ili nisijione bora kuliko nilivyo, kutokana na mafunuo haya makuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mtumishi wa she tani, ili anitese. Nimemsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu. Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uwezo wangu unakamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu ili uwezo wa Kristo ukae juu yangu. 10 Basi, kwa ajili ya Kristo, naridhika na udhaifu, mat usi, taabu, mateso na maafa; kwa maana ninapokuwa mdhaifu ndipo nina nguvu.

Upendo Wa Paulo Kwa Wakorintho

11 Nimekuwa mjinga, lakini ninyi mmenilazimisha niwe hivyo. Kwa kuwa ninyi ndio ambao mngenisifu. Kwa sababu sikuwa wa chini kuliko hawa “mitume wakuu,” hata ingawa mimi si kitu. 12 Mambo yanayomtambulisha mtume wa kweli, yaani ishara, miujiza na maaj abu, yalifanywa miongoni mwenu kwa uvumilivu wote. 13 Je, kuna kitu ambacho hamkupewa sawa na wengine, isipokuwa mimi sikuwa mzigo kwenu? Nisameheni kwa kosa hili.

14 Na sasa niko tayari kuwatembelea kwa mara ya tatu, nami sitahitaji msaada wenu kwa sababu sitaki mnipe mali yenu, ninaowahitaji ni ninyi. Kwa kuwa si sawa watoto waweke akiba kwa ajili ya wazazi wao bali wazazi waweke akiba kwa ajili ya watoto wao. 15 Nitafurahi kutumia kila nilicho nacho hata mwili wangu pia, kwa ajili yenu. Je kama nawapenda zaidi, mtanipenda kidogo tu kwa sababu hiyo? 16 Hata kama mnakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu, wengine watasema nilikuwa mjanja nikawanasa kwa hila. 17 Je, niliwahi kuwadanganya kupitia mmojawapo wa hao watu nil iowatuma kwenu? 18 Nilimsihi Tito aje kwenu nikamtuma ndugu mwingine waje pamoja. Je, Tito aliwatoza cho chote? Je, sisi sote hatukutenda kwa kuongozwa na Roho mmoja na kufuata njia moja?

19 Pengine mnafikiri wakati wote kwamba sisi tunajaribu kujitetea mbele yenu. Sisi tunajitetea mbele ya Mungu katika Kristo, na yote haya ni kwa nia ya kuwajenga ninyi, wapendwa wetu. 20 Kwa maana nina hofu kwamba nitakapokuja nitawakuta hamko kama ambavyo ningependa muwe, na ninyi mtakuta siko kama ambavyo mngependa niwe. Nina hofu kwamba kati yenu huenda kuna ugomvi, wivu, hasira, ubinafsi, uzushi, usengenyaji, majivuno na machafuko. 21 Nina hofu kuwa nitakapokuja tena Mungu wangu ata ninyenyekeza mbele yenu, na huenda nikaomboleza kuhusu wengi wenu ambao walitenda dhambi na hawajatubu na kuacha hayo matendo machafu, uasherati na ufisadi ambao walikuwa wakitenda.

12 It is not expedient for me doubtless to glory. I will come to visions and revelations of the Lord.

I knew a man in Christ above fourteen years ago, (whether in the body, I cannot tell; or whether out of the body, I cannot tell: God knoweth;) such an one caught up to the third heaven.

And I knew such a man, (whether in the body, or out of the body, I cannot tell: God knoweth;)

How that he was caught up into paradise, and heard unspeakable words, which it is not lawful for a man to utter.

Of such an one will I glory: yet of myself I will not glory, but in mine infirmities.

For though I would desire to glory, I shall not be a fool; for I will say the truth: but now I forbear, lest any man should think of me above that which he seeth me to be, or that he heareth of me.

And lest I should be exalted above measure through the abundance of the revelations, there was given to me a thorn in the flesh, the messenger of Satan to buffet me, lest I should be exalted above measure.

For this thing I besought the Lord thrice, that it might depart from me.

And he said unto me, My grace is sufficient for thee: for my strength is made perfect in weakness. Most gladly therefore will I rather glory in my infirmities, that the power of Christ may rest upon me.

10 Therefore I take pleasure in infirmities, in reproaches, in necessities, in persecutions, in distresses for Christ's sake: for when I am weak, then am I strong.

11 I am become a fool in glorying; ye have compelled me: for I ought to have been commended of you: for in nothing am I behind the very chiefest apostles, though I be nothing.

12 Truly the signs of an apostle were wrought among you in all patience, in signs, and wonders, and mighty deeds.

13 For what is it wherein ye were inferior to other churches, except it be that I myself was not burdensome to you? forgive me this wrong.

14 Behold, the third time I am ready to come to you; and I will not be burdensome to you: for I seek not yours but you: for the children ought not to lay up for the parents, but the parents for the children.

15 And I will very gladly spend and be spent for you; though the more abundantly I love you, the less I be loved.

16 But be it so, I did not burden you: nevertheless, being crafty, I caught you with guile.

17 Did I make a gain of you by any of them whom I sent unto you?

18 I desired Titus, and with him I sent a brother. Did Titus make a gain of you? walked we not in the same spirit? walked we not in the same steps?

19 Again, think ye that we excuse ourselves unto you? we speak before God in Christ: but we do all things, dearly beloved, for your edifying.

20 For I fear, lest, when I come, I shall not find you such as I would, and that I shall be found unto you such as ye would not: lest there be debates, envyings, wraths, strifes, backbitings, whisperings, swellings, tumults:

21 And lest, when I come again, my God will humble me among you, and that I shall bewail many which have sinned already, and have not repented of the uncleanness and fornication and lasciviousness which they have committed.