Paulo Na Mitume Wa Uongo

11 Natumaini mtanivumilia hata wakati ninapokuwa mjinga kidogo. Tafadhali nivumilieni! Nawaonea wivu wa kimungu kwa kuwa mimi niliwaposea Kristo, ili niwatoe kama mwanamwali anavy otolewa kwa mume mmoja akiwa hana dosari. Lakini nina hofu kuwa, kama vile Hawa alivyodanganywa na ujanja wa yule nyoka, huenda akili zenu zimepotoshwa, mkaacha upendo wenu safi na wa kweli kwa Kristo. Kwa sababu kama mtu akija akawahubiria Yesu mwingine ambaye si yule tuliyemhubiri, au kama mkipokea roho mwingine ambaye si yule mliyempokea, au kama mkikubali Injili nyingine ambayo si ile mliyoikubali, mnaipokea kwa moyo mmoja! Lakini sidhani ya kuwa mimi ni mdogo sana nikilinganishwa na hao ‘mitume wakuu’. Hata kama mimi si mzungumzaji hodari, lakini ni hodari katika maarifa. Jambo hili ni dhahiri kwenu.

Je, nilitenda dhambi kwa kujishusha mbele yenu na kuwainua ninyi, kwa kuwa niliwahubiria Injili ya Mungu pasipo gharama yo yote kwa upande wenu? Nilipokea msaada kutoka kwa makanisa men gine, niliwanyang’anya wao ili niweze kuwahudumia ninyi. Na nilipokuwa nanyi, nikipungukiwa na cho chote, sikuwa mzigo kwa mtu ye yote, kwa maana ndugu waliotoka Makedonia walitosheleza mahitaji yangu. Kwa hiyo nilijizuia na nitaendelea kujizuia kuwa mzigo kwenu kwa njia yo yote. 10 Na kama ukweli wa Kristo ulivyo ndani yangu, hakuna mtu ye yote katika Akaya nzima atakayenizuia kujivunia jambo hili. 11 Kwa nini? Mnadhani ni kwa kuwa siwa pendi? Mungu anajua ya kuwa nawapenda!

12 Nami nitaendelea kufanya hivi ili kuwazima wale ambao wanatafuta nafasi ya kuhesabiwa kuwa sawa na sisi katika mambo wanayojisifia. 13 Watu kama hao ni manabii wa uongo, ni wafany akazi wadanganyifu ambao wanajifanya kuwa mitume wa Kristo. 14 Na hii si ajabu, kwa sababu hata shetani hujigeuza aonekane kama malaika wa nuru. 15 Kwa hiyo si ajabu kama malaika wake shetani nao wanajigeuza waonekane kama watumishi wa haki. Mwisho wao utakuwa sawa na matendo yao.

Paulo Anajivunia Mateso Yake

16 Nasema tena, mtu ye yote asidhani kwamba mimi ni mjinga. Lakini hata kama mkinidhania hivyo, basi nipokeeni kama mjinga ili nipate kujisifu kidogo. 17 Ninayosema sasa, kwa majivuno, nasema kama mjinga na wala si kwa mamlaka ya Bwana. 18 Kwa sababu wengine wanajivunia mambo ya kidunia, basi na mimi nitaji sifu. 19 Ninyi mnawavumilia wajinga kwa kuwa mna hekima mno! 20 Tena mnavumilia hata kama mtu anawafanya watumwa au anawany onya na kuwadanganya au anajigamba mbele yenu au anawapiga makofi usoni. 21 Naona aibu kukubali kwamba sisi ni wadhaifu kiasi ambacho hatuwezi kufanya mambo kama hayo. Lakini cho chote ambacho mtu anathubutu kujivunia, sasa nasema kama mjinga, mimi pia naweza kuthubutu kujivunia.

22 Je, wao ni Waebrania? Mimi pia ni Mwebrania. Wao ni uzao wa Ibrahimu? Na mimi pia. 23 Wao ni watumishi wa Kristo? Mimi ni mtumishi bora zaidi, nasema kama kichaa. Nimefanya kazi zaidi, nimefungwa gerezani zaidi, nimechapwa viboko visivyo na hesabu, na mara nyingi nilikuwa karibu kufa. 24 Mara tano nimechapwa viboko aro baini kupungua kimoja na Wayahudi. 25 Nimechapwa kwa chuma mara tatu. Nimepigwa mawe mara moja. Mara tatu nimevunjikiwa na meli. Nimeelea baharini usiku kucha na mchana kutwa. 26 Katika safari zangu nyingi, nimekuwa katika hatari za mafuriko, hatari za wany ang’anyi, hatari kutoka kwa Wayahudi wenzangu na hatari kutoka kwa watu wa mataifa mengine; nimekuwa katika hatari mijini, nyikani, baharini na katika hatari kutoka kwa ndugu wa uongo. 27 Nimekuwa katika kazi ngumu na taabu, siku nyingi nimekuwa bila usingizi, nimekuwa na njaa na kiu, mara nyingi nimekuwa bila chakula, katika baridi na bila nguo. 28 Na ukiacha mambo mengine nimelemewa na wasiwasi juu ya makanisa yote. 29 Je, ni nani ana kuwa mdhaifu nisijisikie mdhaifu? Nani anashawishiwa kutenda dhambi nisijisikie nachomwa na uchungu?

30 Nikilazimika kujisifu, basi nitajisifia yale mambo yanay oonyesha udhaifu wangu. 31 Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye amebarikiwa daima, anajua ya kuwa mimi sisemi uongo. 32 Kule Dameski, gavana aliyekuwa chini ya Mfalme Areta aliu linda mji wa Dameski ili wapate kunikamata, 33 lakini nilish ushwa kwa kapu kubwa kupitia katika dirisha ukutani nikaepuka kukamatwa.

Paulo na Mitume wa Uongo

11 Natamani mngekuwa na subira nami hata pale ninapokuwa mjinga kidogo. Tafadhali muwe na subira nami. Nina wivu unaotoka kwa Mungu kwa ajili yenu. Niliahidi kuwatoa ninyi kama bibi harusi kwa mume mmoja. Niliahidi kuwatoa ninyi kwa Kristo muwe bibi harusi[a] wake aliye safi. Ila nina hofu kuwa nia zenu zitapotoshwa muache kujitoa kwa dhati na kumfuata Yesu Kristo kwa moyo safi. Hili laweza kutokea kama vile Hawa alivyodanganywa na nyoka kwa akili zake za ujanja wenye udanganyifu. Mnaonekana kuwa na subira na mtu yeyote anayekuja kwenu na kuwaeleza habari za Yesu aliye tofauti na Yesu yule ambaye sisi tuliwaambia habari zake. Mnaonekana kuwa radhi kuipokea roho au ujumbe ulio tofauti na roho na ujumbe ambao mlioupokea kutoka kwetu.

Sidhani kuwa hao “mitume wakuu” ni bora kuliko mimi nilivyo. Ni kweli kuwa mimi siye mtu nilyefunzwa kwa mzungumzaji, lakini nina ufahamu wa mambo. Tumeliweka hili wazi kwenu kwa njia zote na kwa mazingira yote.

Nilifanya kazi ya kutangaza Habari Njema za Mungu kwenu bila malipo. Nilijinyenyekeza ili kuwafanya ninyi kuwa wa muhimu. Je! Mwadhani nilikosea katika hilo? Nilipokea malipo toka makanisa mengine. Ilikuwa kana kwamba nimechukua fedha toka kwao ili niweze kuwatumikia ninyi. Kama nilihitaji chochote nilipokuwa nanyi, sikumsumbua yeyote kati yenu. Kina kaka waliofika kutoka Makedonia walinipa yote niliyohitaji. Sikutaka kuwa mzigo kwenu kwa namna yeyote ile. Na kamwe sitakuwa mzigo kwenu. 10 Hakuna mtu yeyote katika jimbo lote la Akaya anayeweza kunizuia kujivuna juu ya hilo. Nasema hili katika kweli ya Kristo iliyo ndani yangu. 11 Kwa nini siwalemei? Je! Mnadhani ni kwa sababu siwapendi? Mungu anajua ya kwamba ninawapenda.

12 Na nitaendelea kufanya kile ninachokifanya sasa, kwa sababu nataka kuwazuia watu hao wasiwe na sababu ya kujivunia. Wangependa kusema kuwa kazi ile wanayojivunia ni sawa na kazi yetu. 13 Wao ni mitume wa uongo, watenda kazi walio wadanganyifu. Wao hujifanya kuwa ni mitume wa Kristo. 14 Hilo halitushangazi sisi, kwa sababu hata Shetani mwenyewe hujigeuza na kujifanya kuwa malaika wa nuru.[b] 15 Hivyo, hiyo haitufanyi sisi kustaajabu ikiwa watumishi wa shetani watajigeuza na kujifanya kuwa watumishi wanaofanya yaliyo ya haki. Lakini mwishowe watapokea hukumu wanayostahili.

Paulo aelezea juu ya Mateso yake

16 Ninawaambia tena: Asiwepo yeyote wa kudhani kuwa mimi ni mjinga. Lakini kama mnadhani kuwa mimi ni mjinga, basi nipokeeni kama vile ambavyo mngempokea mjinga. Kisha nami naweza kujivuna angalau kidogo zaidi pia. 17 Lakini mimi sizungumzi kwa namna ambavyo Bwana angelizungumza. Mimi ninajivuna kama vile mjinga. 18 Wengi wengine wanajivuna jinsi ambavyo watu wa dunia hii wanafanya. Hivyo, nami nitajivuna kwa namna hiyo. 19 Mna busara, hivyo mtamvumilia kwa furaha mjinga! 20 Nasema haya kwa sababu mnamvumilia hata mtu yule anayewatumia vibaya. Mnawavumilia wale wanaowarubuni akili na kudhani kuwa wao ni bora kuliko ninyi, au wanaowapiga usoni! 21 Ninaona aibu kusema haya, lakini tulikuwa “dhaifu sana” kuyafanya mambo kama hayo kwenu.

Lakini kama kuna mtu aliye jasiri vya kutosha kujivuna, nami nitajivuna pia. (Ninaongea hivi kama mjinga.) 22 Je, watu hao ni Wayahudi? Mimi pia. Je, ni Waebrania? Mimi pia. Je, wanatoka katika familia ya Ibrahimu? Mimi pia. 23 Je, wanamtumikia Kristo? Mimi ninamtumikia zaidi sana. (Je, mimi ni mwendawazimu kuongea kwa jinsi hii?) Nimefanya kazi kwa juhudi kuliko wao. Nimekuwa gerezani mara nyingi. Nimepigwa vibaya sana. Nimekuwa katika hali za hatari ya kufa mara nyingi.

24 Mara tano Wayahudi wamenipa adhabu ya viboko 39. 25 Mara tatu katika nyakati tofauti nimepigwa kwa fimbo. Mara moja nilikuwa karibu kuuawa kwa kupigwa kwa mawe. Mara tatu nimevunjikiwa na merikebu, na mara moja katika hizo nilikesha usiku na kushinda kutwa nzima tukielea baharini. 26 Katika safari zangu za mara kwa mara nimekuwa katika hatari za kwenye mito, majambazi, watu wangu wenyewe, na toka kwa watu wasio Wayahudi. Nimekuwa katika hatari mijini, katika maeneo wasioishi watu, na katika bahari. Na nimekuwa katika hatari za watu wanaojifanya kuwa waamini lakini siyo waamini.

27 Nimefanya kazi ngumu na za kuchosha, na mara nyingi sikuweza kulala usingizi. Nimekuwa mwenye njaa na kiu. Mara nyingi nimekosa kula chakula. Nimekuwa katika hali ya baridi na kutokuwa na nguo za kujifunika. 28 Na kuna matatizo mengine mengi zaidi. Mojawapo ya hayo ni mzigo nilio nao kila siku wa majukumu yangu: Ninawaza juu ya makanisa yote. 29 Ninajisikia kuwa mdhaifu kila mara mtu mwingine anapokuwa dhaifu. Ninapata hasira sana pale mtu yeyote anapoingizwa dhambini.

30 Ikiwa ni lazima nisifu, nitajisifu katika vitu vinavyonidhihirisha kuwa mimi ni dhaifu. 31 Mungu ajua kuwa sisemi uongo. Yeye ni Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na anapaswa kutukuzwa milele. 32 Nilipo kuwa Dameski, gavana wa mfalme Areta alitaka kunikamata, hivyo aliweka walinzi nje ya malango ya jiji. 33 Lakini baadhi ya marafiki wakaniweka ndani ya kikapu. Kisha wakaniteremsha chini kupitia dirisha lililokuwa kwenye katika ukuta wa mji. Hivyo nikamtoroka gavana.

Footnotes

  1. 11:2 bibi harusi Kwa maana ya kawaida, “bikira au mwanamwali”.
  2. 11:14 malaika wa nuru Mtumishi au tarishi wa Mungu. Shetani anawadanganya watu waone kuwa ametumwa na Mungu.