Bwana Atakuja Ghafla

Basi, ndugu wapendwa, hatuna haja ya kuwaandikieni kuhusu nyakati na tarehe atakayokuja Bwana, kwa maana mnajua wazi kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi anavyokuja usiku. Wakati watu bado wanasema, “Kuna amani na usalama’

Bali ninyi, ndugu wapendwa, hamko gizani kuhusu mambo haya hata siku ile iwashtue kama mwizi. Ninyi nyote ni wana wa nuru, wana wa mchana. Sisi sio watu wa giza au wa usiku. Kwa hiyo basi, tusiwe kama baadhi ya watu wengine, waliolala, bali tukeshe na kuwa na kiasi. Maana wale wanaolala hulala usiku, na wale wanaolewa hulewa usiku. Lakini kwa kuwa sisi ni watu wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukivaa imani na upendo kama kinga ya kifuani na kuvaa tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma. Maana Mungu hakutuchagua ili tupate ghadhabu yake bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. 10 Yeye alitufia ili kama tuko hai au hata kama tumekufa, tuishi pamoja naye. 11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana kama mnavyofanya sasa.

Maagizo Ya Mwisho Na Salamu

12 Sasa tunawaomba, ndugu wapendwa, muwaheshimu wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu; ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya. 13 Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa ajili ya kazi yao. Ishini kwa amani kati yenu. 14 Na tunawasihi, ndugu wapendwa, muwaonye wale walio wavivu, watieni moyo walio waoga, wasaidieni walio dhaifu na muwe na subira na kila mtu. 15 Hakikisheni kuwa mtu hamlipi mwenzake ovu kwa ovu bali daima jitahidini kutendeana wema ninyi kwa ninyi na watu wengine wote.

16 Furahini wakati wote, 17 ombeni pasipo kukoma, 18 shu kuruni katika kila hali; kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu mkiwa ndani ya Kristo Yesu. 19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu; 20 msidharau unabii. 21 Pimeni kila kitu. Yash ikeni kwa makini yaliyo mema. 22 Epukeni uovu wa kila namna.

23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase kabisa. Roho zenu, nafsi zenu na miili yenu na ihifadhiwe bila kuwa na lawama kwa wakati atakapokuja Bwana wetu Yesu Kristo. 24 Yeye aliyew aita ni mwaminifu naye atafanya haya.

25 Ndugu wapendwa, tuombeeni. 26 Wasalimieni ndugu wote kwa busu takatifu. 27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.

Uwe tayari kwa ujio wa Bwana

Na sasa ndugu zangu, hatuna haja ya kuwaandikia juu ya nyakati na tarehe. Ninyi mnafahamu vizuri kuwa siku ambayo Bwana atakuja itakuwa ya kushitukiza, kama mwizi anavyokuja usiku. Watu watasema, “tuna amani na tuko salama.” Wakati huo ndipo uharibifu utakapowajia haraka, kama maumivu anayoyapata mwanamke anapojifungua. Na watu hao hawataweza kukwepa.

Lakini ninyi ndugu zangu, hamuishi katika giza. Na hivyo ile siku haitawashangaza kama mwivi. Nyote ni watu wa nuru. Ni watu wa mchana. Hatuko katika usiku wala giza. Hivyo tusiwe kama watu wengine. Tusiwe wasinziao. Tuwe macho na wenye kiasi. Watu walalao, hulala usiku. Watu wanywao kupita kiasi, hunywa usiku. Bali sisi ni watu wa mchana, hivyo tujitawale wenyewe. Tuvae imani na upendo vitulinde. Na tumaini la wokovu liwe kwetu kama kofia ya vita.

Mungu hakutuchagua tuangamie katika hasira yake. Mungu alituchagua tuwe na wokovu katika Bwana wetu Yesu Kristo. 10 Yesu alikufa kwa ajili yetu ili tuishi pamoja nae. Haijalishi kama tu hai au wafu atakapokuja. 11 Hivyo farijianeni ninyi kwa ninyi na msaidiane kukua imara katika imani, kama mnavyofanya sasa.

Maagizo ya Mwisho na Salamu

12 Tunawaomba mwatambue wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao, kama wafuasi wa Bwana, wanatumika kama viongozi wenu na kuwafundisha namna ya kuishi. 13 Wapeni heshima ya hali ya juu na upendo kwa sababu ya kazi wanayofanya.

Ishini kwa amani kila mmoja na mwenzake. 14 Tunawasihi, kuwaonya wale wanaokataa kuishi kwa kuwajibika.[a] Watieni moyo wanaoogopa. Wasaidieni walio dhaifu. Mvumilieni kila mmoja. 15 Asiwepo anae jaribu kulipiza baya kwa baya. Lakini kila mara mfanye lililo jema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.

16 Mwe na furaha daima. 17 Msiache kuomba. 18 Shukuruni kwa kila jambo. Hivi ndivyo Mungu anavyotutaka tuishi katika Kristo Yesu.

19 Msiizimishe kazi ya Roho Mtakatifu. 20 Msiuchukulie unabii kama kitu kisicho cha muhimu. 21 Lakini pimeni kila kitu. Lishikeni lililo jema, 22 na mkae mbali na kila aina ya ovu.

23 Tunaomba kwamba Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, atawafanya muwe watakatifu mkiwa wake. Tunaomba kwamba katika roho yote, nafsi yote, na mwili mzima mtahifadhiwa salama pasipo lawama Bwana wetu Yesu Kristo atakapokuja. 24 Yeye awaitae atawatendea haya. Mnaweza kumtumainia.

25 Kaka na dada zangu, tafadhali mtuombee. 26 Wasalimuni ndugu wote kwa salamu maalum ya watu wa Mungu.[b] 27 Ninawaagiza kwa mamlaka ya Bwana kuusoma walaka huu kwa waamini wote huko. 28 Neema ya Bwana wetu Yesu kristo iwe nanyi nyote.

Footnotes

  1. 5:14 kuwajibika Ikiwa na maana ya “kuishi kwa kufuata utaratibu unaofaa” Kuishi pasipo kuwajibika ni kutofanya kazi.
  2. 5:26 salamu maalum ya watu wa Mungu Kwa maana ya kawaida, “busu takatifu”.

The Day of the Lord

Now, brothers and sisters, about times and dates(A) we do not need to write to you,(B) for you know very well that the day of the Lord(C) will come like a thief in the night.(D) While people are saying, “Peace and safety,”(E) destruction will come on them suddenly,(F) as labor pains on a pregnant woman, and they will not escape.(G)

But you, brothers and sisters, are not in darkness(H) so that this day should surprise you like a thief.(I) You are all children of the light(J) and children of the day. We do not belong to the night or to the darkness. So then, let us not be like others, who are asleep,(K) but let us be awake(L) and sober.(M) For those who sleep, sleep at night, and those who get drunk, get drunk at night.(N) But since we belong to the day,(O) let us be sober, putting on faith and love as a breastplate,(P) and the hope of salvation(Q) as a helmet.(R) For God did not appoint us to suffer wrath(S) but to receive salvation through our Lord Jesus Christ.(T) 10 He died for us so that, whether we are awake or asleep, we may live together with him.(U) 11 Therefore encourage one another(V) and build each other up,(W) just as in fact you are doing.

Final Instructions

12 Now we ask you, brothers and sisters, to acknowledge those who work hard(X) among you, who care for you in the Lord(Y) and who admonish you. 13 Hold them in the highest regard in love because of their work. Live in peace with each other.(Z) 14 And we urge you, brothers and sisters, warn those who are idle(AA) and disruptive, encourage the disheartened, help the weak,(AB) be patient with everyone. 15 Make sure that nobody pays back wrong for wrong,(AC) but always strive to do what is good for each other(AD) and for everyone else.

16 Rejoice always,(AE) 17 pray continually,(AF) 18 give thanks in all circumstances;(AG) for this is God’s will for you in Christ Jesus.

19 Do not quench the Spirit.(AH) 20 Do not treat prophecies(AI) with contempt 21 but test them all;(AJ) hold on to what is good,(AK) 22 reject every kind of evil.

23 May God himself, the God of peace,(AL) sanctify you through and through. May your whole spirit, soul(AM) and body be kept blameless(AN) at the coming of our Lord Jesus Christ.(AO) 24 The one who calls(AP) you is faithful,(AQ) and he will do it.(AR)

25 Brothers and sisters, pray for us.(AS) 26 Greet all God’s people with a holy kiss.(AT) 27 I charge you before the Lord to have this letter read to all the brothers and sisters.(AU)

28 The grace of our Lord Jesus Christ be with you.(AV)