Timotheo Atumwa Kwenda Thesalonike

Hatimaye tuliposhindwa kuvumilia zaidi, tuliona afadhali tubaki Athene peke yetu. Tukamtuma Timotheo ambaye ni ndugu yetu na mtumishi wa Mungu katika kuieneza Habari Njema ya Kristo, aje kuwaimarisha na kuwatia moyo ili asije mtu akababaishwa na mateso haya. Kama mjuavyo, tumepangiwa mateso. Hata tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaambia mara kwa mara kwamba tutateswa, na kama mjuavyo ndivyo ilivyokuwa. Ndio maana niliposhindwa kuvumilia nilituma mtu ili nifahamu msimamo wenu katika imani. Niliogopa kuwa pengine yule mjaribu shetani alikuwa amewajaribu na kwamba pengine juhudi yetu kwenu ingekuwa ni bure.

Taarifa Ya Timotheo

Lakini sasa Timotheo amekwisha rejea kutoka kwenu na ameleta taarifa nzuri kuhusu imani yenu na upendo wenu. Ametuam bia kwamba mnatukumbuka kwa wema na kwamba mna hamu siku zote kutuona kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaona. Kwa sababu hiyo ndugu zetu, katika dhiki na mateso yetu yote tumefarijika kwa ajili yenu, kutokana na imani yenu. Maana sasa hakika tunaishi kwa kuwa ninyi mmesimama imara katika Bwana. Tutawezaje kumshu kuru Mungu kiasi cha kutosha kwa ajili yenu, kutokana na furaha tuliyo nayo mbele za Mungu wetu kwa sababu yenu? 10 Usiku na mchana tunaomba kwa bidii ili tuwezeshwe kuwaona tena na kuwapa tieni kile ambacho bado kinapungua katika imani yenu.

11 Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu. 12 Bwana na awawezeshe ninyi kupendana zaidi na zaidi na kuwapenda watu wote kama sisi tunav yowapenda ninyi. 13 Tunamwomba awaimarisheni mioyo ili msiwe na lawama bali muwe watakatifu mbele za Mungu Baba yetu, wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na watakatifu wake wote.

1-2 Nisingeweza kuja kwenu, ila ilikuwa vigumu kuendelea kusubiri zaidi. Hivyo tuliamua kumtuma Timotheo kwenu na tukabaki Athene peke yetu. Timotheo ni ndugu yetu. Ni mtenda kazi pamoja nasi kwa ajili ya Mungu katika kuwahubiri watu Habari Njema kuhusu Kristo. Nilimtuma Timotheo kuwaimarisha na kuwafariji katika imani yenu. Tulimtuma ili asiwepo kati yenu atakayebugudhiwa na mateso tuliyo nayo sasa. Ninyi wenyewe mnatambua kuwa ni lazima tupatwe na mateso haya. Hata pale tulipokuwa pamoja nanyi, tuliendelea kuwaeleza mapema ya kuwa sote tutapata matatizo. Na mnafahamu kuwa ilitokea kama tulivyowaambia. Hii ndiyo sababu nilimtuma Timotheo kwenu, ili nipate kujua juu ya uaminifu wenu. Nilimtuma kwenu nilipokuwa siwezi kuendelea kusubiri zaidi. Nilihofu kuwa Shetani angeweza kuwashinda kwa majaribu yake. Kisha kazi yetu iliyokuwa ngumu ingepotea bure.

Bali sasa Timotheo amerudi kutoka kwenu na kutueleza juu ya uaminifu wenu na upendo wenu. Ametueleza kuwa mmeendelea kuwa na kumbukumbu njema juu yetu kama mfano kwenu. Na amesema kuwa mnatamani sana kutuona tena. Hivyo ndivyo ilivyo kwetu pia tunatamani sana kuwaona ninyi. Kwa hiyo, ndugu zangu, tunatiwa moyo sana kwa ajili ya uaminifu wenu. Tunapata mateso na masumbufu mengi, lakini bado tunatiwa moyo nanyi. Kwa kuwa sasa tuna maisha mapya tunapata utimilifu ikiwa imani yenu katika Bwana inaendelea kuwa imara. Tuna furaha tele mbele za Mungu wetu kwa ajili yenu! Lakini hatuwezi kumshukuru Mungu inavyopasa kwa furaha ile yote tuliyo nayo. 10 Usiku na mchana tuliendelea kuomba kwa mioyo yetu yote kwamba tuweze kuja huko na tuwaone tena. Tunataka kuwapa kila mnachohitaji ili imani yenu iwe timilifu.

11 Tunaomba kwamba Mungu wetu aliye Baba yetu, na Bwana Yesu wataiongoza njia yetu kuja kwenu. 12 Tunaomba kuwa Bwana ataufanya upendo wenu uendelee kukua. Tunaomba kuwa atawapa kupendana zaidi na zaidi miongoni mwenu na kwa watu wote. Tunaomba kuwa mtampenda kila mmoja kwa namna ile ile ambayo sisi tuliwapenda ninyi. 13 Hii itaongeza hamu yenu ya kutenda yaliyo haki, na mtakuwa watakatifu msio na kosa mbele za Mungu wetu na baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapo kuja na watakatifu[a] wake wote.

Footnotes

  1. 3:13 watakatifu Au “malaika watakatifu”.