Kutoka kwa Paulo, Silvano na Timotheo. Kwa kanisa la Wath esalonike mlio wa Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo. Tuna watakieni neema na amani.

Shukrani Kwa Imani Ya Wathesalonike

Tunamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu wote na kuwaom bea pasipo kukoma. Tunakumbuka daima mbele za Mungu Baba yetu, kazi yenu inayotokana na imani, juhudi yenu kubwa katika upendo, na uvumilivu wenu unaotokana na tumaini mlilonalo kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Ndugu zetu mnaopendwa na Mungu, tunafahamu kwamba Mungu amewachagua kwa maana Injili yetu haikuwajia kwa maneno matupu bali ilidhihirishwa kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, mkawa na uhakika kamili. Ninyi mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi kwa faida yenu. Nanyi mkatuiga sisi, mkamuiga na Bwana; kwa maana mlilipokea neno kwa furaha mliyopewa na Roho Mtakatifu ingawa mlipata mateso makali. Kwa hiyo mkawa kielelezo kwa waamini wote wa Makedonia na Akaya.

Maana neno la Mungu limeenea kutoka kwenu, sio mpaka Make donia na Akaya tu, bali imani yenu kwa Mungu imejulika na mahali pote. Kwa hiyo hatuhitaji kusema lo lote kuhusu imani yenu; kwa maana wao wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea. Wanasimulia jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha ibada za sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli; 10 na kumngoja Mwanae kutoka mbin guni, ambaye alimfufua kutoka kwa wafu, yaani Yesu. Yeye anatu komboa kutoka katika ghadhabu ijayo.

Paul, and Silvanus, and Timotheus, unto the church of the Thessalonians which is in God the Father and in the Lord Jesus Christ: Grace be unto you, and peace, from God our Father, and the Lord Jesus Christ.

We give thanks to God always for you all, making mention of you in our prayers;

Remembering without ceasing your work of faith, and labour of love, and patience of hope in our Lord Jesus Christ, in the sight of God and our Father;

Knowing, brethren beloved, your election of God.

For our gospel came not unto you in word only, but also in power, and in the Holy Ghost, and in much assurance; as ye know what manner of men we were among you for your sake.

And ye became followers of us, and of the Lord, having received the word in much affliction, with joy of the Holy Ghost.

So that ye were ensamples to all that believe in Macedonia and Achaia.

For from you sounded out the word of the Lord not only in Macedonia and Achaia, but also in every place your faith to God-ward is spread abroad; so that we need not to speak any thing.

For they themselves shew of us what manner of entering in we had unto you, and how ye turned to God from idols to serve the living and true God;

10 And to wait for his Son from heaven, whom he raised from the dead, even Jesus, which delivered us from the wrath to come.