Haki Za Mtume

Je, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana? Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni uthibitisho wa utume wangu katika Bwana. Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu. Je? hatuna haki ya kupewa chakula na cha kunywa? Je, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana na Kefa? Au ni Barnaba na mimi tu ambao tunal azimika kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu?

Ni askari yupi anayelipa gharama zake mwenyewe akiwa kam bini? Ni mkulima gani anayepanda mizabibu na hali matunda yake? Ni mfugaji yupi asiyekunywa maziwa ya kundi la wanyama wake? Mnadhani nasema haya kwa kutumia mifano ya kila siku tu? Je, sheria haisemi vivyo hivyo? Kwa maana sheria ya Musa inasema, “Usimfunge ng’ombe kinywa wakati anapopura nafaka.” Je? Mnad hani ni ng’ombe ambaye Mungu anamfikiria? 10 Je, Mungu hasemi haya hasa kwa ajili yetu? Kwa kweli haya yalisemwa kwa ajili yetu kwa sababu mtu anapolima na mwingine akapura nafaka, wote wana paswa kufanya hivyo wakiwa na matumaini ya kupata sehemu ya mavuno. 11 Je, ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, itakuwa ni kitu kikubwa sana iwapo tutavuna mahitaji ya mwili kutoka kwenu? 12 Kama wengine wana haki ya kupata msaada kutoka kwenu, sisi je, isingepasa tuwe na haki hiyo hata zaidi? Lakini sisi hatukupenda kutumia haki hii, bali tunavumilia kila kitu ili tusije tukaweka kizuizi kwenye Injili ya Kristo.

13 Hamjui kwamba, watu walioajiriwa kazi Hekaluni wanapata chak ula chao hekaluni, na wale wanaohudumu madhabahuni wanapata sehemu ya sadaka zinazotolewa? 14 Vivyo hivyo, Bwana aliagiza kwamba wale wanaohubiri Injili watapata chakula chao kutokana na Injili. 15 Lakini mimi sikutumia haki hizi, na wala siandiki haya ili kudai haki zangu. Ni afadhali nife, kuliko mtu aniondolee haki hii ya kujisifu. 16 Ninapohubiri Injili, siwezi kujisifu kwa sababu ninalazimika kuhubiri. Ole wangu nisipohubiri Injili! 17 Nikihubiri kwa hiari ningetegemea kupata tuzo; lakini ikiwa nalazimika kufanya hivyo, basi ninachofanya ni kutekeleza wajibu wangu. 18 Kwa hali hii tuzo yangu ni nini? Tuzo yangu ni hii, kwamba katika kuhubiri kwangu, nitangaze Injili pasipo kudai cho chote na hivyo nisitumie haki zangu katika kuhubiri Injili.

19 Ingawa mimi ni huru, na si mtumwa wa mtu ye yote, nimeji fanya kuwa mtumwa wa wote, ili niweze kuwavuta wengi iwezeka navyo. 20 Kwa Wayahudi, nilikuwa kama Myahudi ili niweze kuwa vuta Wayahudi. Kwa watu wanaotawaliwa na sheria, nilikuwa kama niliye chini ya sheria, ingawa mimi siko chini ya sheria, ili niweze kuwavuta walio chini ya sheria. 21 Kwa watu wasioijua sheria nilikuwa kama nisiye na sheria, ingawa hii haina maana kwamba sizishiki amri za Mungu, bali niko chini ya sheria ya Kristo, ili niweze kuwavuta wasio na sheria. 22 Kwa wadhaifu nilikuwa mdhaifu ili niweze kuwavuta wadhaifu. Nimekuwa mdhaifu ili niweze kuwavuta wadhaifu. Nimekuwa mtu wa hali zote kwa watu wote ili kwa njia zote nipate kuwaokoa baadhi yao. 23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nishiriki baraka zake.

24 Mnajua kwamba katika mashindano ya riadha wote wanao shindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu anayepata tuzo. Kwa hiyo kimbieni katika mashindano kwa njia itakayowapatia tuzo. 25 Kila mwana-riadha anayeshiriki katika michezo ya mashindano hufanya mazoezi makali. Wanafanya hivyo ili kupokea tuzo ambayo haidumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata tuzo isiyohari bika kamwe. 26 Mimi sikimbii pasipo kuwa na lengo. Sipigani kama mtu anayepiga hewa; 27 lakini nauimarisha mwili wangu na kuutawala, ili baada ya kuwahubiria wengine, mimi mwenyewe nisije nikakataliwa.

Haki Ambazo Paulo Hajazitumia

Mnajua kuwa mimi ni mtu niliye huru. Mnajua kuwa mimi ni mtume na kwamba nilimwona Yesu Bwana wetu. Na ninyi ni kielelezo cha kazi yangu katika Bwana. Wengine wanaweza wasikubali kuwa mimi ni mtume, lakini hakika ninyi mnakubali. Ninyi ni uthibitisho kuwa mimi ni mtume wa Bwana.

Ninataka kuwajibu baadhi ya watu wanaotaka kunichunguza. Je, hatuna haki ya kula na kunywa? Je, hatuna haki ya kusafiri pamoja na mke aliye mwamini? Mitume wengine wote, wadogo zake Bwana na Petro hufanya hivi. Na je, ni mimi na Barnaba tu ndiyo ambao ni lazima tufanya kazi ili tupate kipato cha kutuwezesha kuishi? Ni askari gani aendaye vitani kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Au ni nani achungaye kundi la kondoo na hanywi maziwa?

Lakini nina mifano mingi kutoka katika maisha ya kila siku inayosisitiza hoja yangu. Sheria ya Mungu inasema vivyo hivyo pia. Ndiyo, imeandikwa katika Sheria ya Musa kuwa; “Mnyama wa kazi anapotumika kupura nafaka, usimzuie kula nafaka.”(A) Je, Mungu aliposema hivi, alikuwa anawawazia wanyama pekee? Hapana. 10 Hakika Mungu alizungumza kuhusu sisi. Ndiyo, iliandikwa kwa ajili yetu. Wote wawili, anayelima na anayepura nafaka, wana haki ya kupata nafaka kutokana na kazi yao. 11 Ikiwa tulipanda mbegu ya kiroho mioyoni mwenu, je, hatustahili kupata vitu kwa ajili ya maisha haya kutoka kwenu? 12 Ikiwa wengine wana haki ya kupata vitu kutoka kwenu, hakika hata sisi tuna haki pia. Lakini hatuitumii haki hii. Tunavumilia katika hali zote ili tusimfanye mtu yeyote akaacha kuitii Habari Njema ya Kristo. 13 Hakika mnajua ya kuwa wanaotumika Hekaluni hula chakula kutoka Hekaluni. Na wale wanaotumika madhabahuni hupata sehemu ya yale yanayotolewa madhabahuni. 14 Vivyo hivyo kwa wale wenye kazi ya kuhubiri Injili. Bwana ameamuru kuwa nao wataishi kutokana na kazi hiyo.

15 Lakini sijatumia haki hizi, na si kwamba ninataka kitu chochote kutoka kwenu. Ijapokuwa ninaandika hivi hilo si lengo langu. Ni bora nife kuliko mtu yeyote kuchukua kutoka kwangu kitu ninachojivunia. 16 Sijivuni kwa sababu ya kazi yangu ya kuhubiri Habari Njema kwa sababu ni wajibu wangu ambao ni lazima nifanye; ole wangu nisipowahubiri watu Habari Njema. 17 Ikiwa ningehubiri kwa sababu ya utashi kwangu, ningestahili kulipwa. Lakini sikuchagua kufanya kazi hii. Ni lazima nihubiri Habari Njema. Hivyo ninafanya kazi niliyokabidhiwa. 18 Sasa, kwa kufanya kazi hii ninapata nini? Thawabu yangu, ni kuwa ninapowahubiri watu Habari Njema, ninawapa bure na sizitumii haki zinazoambatana na kufanya kazi hii.

19 Niko huru. Similikiwi na mtu yeyote, lakini ninakuwa mtumwa ili watu wengi waokoke. 20 Kwa Wayahudi nilienenda kama Myahudi ili nisaidie Wayahudi wengi waokolewe. Sitawaliwi na sheria, lakini kwa wanaotawaliwa na sheria nilikuwa kama ninayetawaliwa na sheria. Nilifanya hivi kuwasaidia wanaotawaliwa na sheria, ili waokoke. 21 Kwa wasio na sheria nilikuwa kama nisiye na sheria, ili niwasaidie wasio na sheria kuokoka. Mimi si kama mtu asiye na Sheria ya Mungu, ninatawaliwa na sheria ya Kristo. 22 Kwa waliodhaifu, nilikuwa dhaifu ili niwasaidie kuokoka. Nilifanyika kila kitu kwa watu wote ili nifanye kila kinachowezekana niweze kuwasaidia watu waokolewe. 23 Ninafanya kila ninachoweza ili Habari Njema ijulikane na niweze kushiriki katika Habari zake.

24 Mnajua kuwa katika riadha, wanariadha wengi hukimbia, lakini mmoja tu hupata zawadi. Hivyo kimbieni hivyo. Kimbieni ili mshinde! 25 Wote wanaoshiriki katika mchezo hufanya mazoezi kwa bidii ili waweze kushinda na kupata zawadi. Lakini zawadi wanazopata hazidumu milele. Lakini zawadi yetu ni ile inayodumu milele. 26 Hivyo ninakimbia kama mtu mwenye malengo. Ninapigana ngumi kama mpiganaji anayepiga kitu, si kama anayepiga hewa. 27 Ninaudhibiti mwili wangu kikamilifu na kuufanya unitiii kwa kila jambo ninalotaka kutenda. Ninafanya hivi ili mimi binafsi nisiikose thawabu baada ya kuwahubiri wengine Habari Njema.