Mgawanyiko Katika Kanisa

Lakini ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwili, na kama watoto wachanga katika Kristo. Niliwalisha maziwa, sio chakula kigumu; kwa kuwa mli kuwa hamjawa tayari kukipokea. Kwa maana ninyi bado mnatawaliwa na mambo ya mwili. Je, wakati kuna wivu na kugombana kati yenu, ninyi si watu wa mwili wenye tabia kama za watu wa kawaida? Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo” hamfanyi kama watu wa kawaida?

Hata hivyo, Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Sisi ni watum ishi tu ambao kama Bwana alivyotupangia kila mmoja kazi yake, mliamini kwa msaada wetu. Mimi nilipanda mbegu, na Apolo akaimwagilia maji, lakini ni Mungu aliyefanya mbegu iote. Kwa hiyo anayepanda mbegu na anayemwagilia maji si kitu, bali Mungu pekee ndiye aliyefanya mbegu iote. Anayepanda mbegu ni sawa na yule anayemwagilia maji. Kila mmoja wao atapokea malipo yake kulingana na kazi yake. Sisi ni wafanyakazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu; ninyi ni jengo la Mungu.

10 Kwa neema niliyopewa na Mungu nilijenga msingi kama mjenzi hodari, na mtu mwingine ana jenga juu ya msingi huo. Lakini kila mmoja awe mwangalifu anavyojenga juu yake. 11 Kwa maana hakuna mtu anayeweza kuweka msingi mwingine isipokuwa ule uliokwisha jengwa, ambao ni Yesu Kristo. 12 Kama mtu ye yote atajenga juu ya msingi huu akitumia dhahabu, fedha, mawe ya tha mani, mbao, majani au nyasi, 13 kazi yake itaonekana; kwa kuwa ile siku itaidhihirisha kazi yake. Itadhihirishwa kwa moto, na moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu. 14 Kama alichojenga hakitaharibiwa kwa moto, atapokea tuzo. 15 Kama kazi ya mtu itateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini kama mtu aliyenusurika kwenye moto.

16 Je, hamjui kwamba ninyi ni Hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu ye yote akiliharibu Hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa sababu Hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ni Hekalu hilo. 18 Mtu asijidanganye mwenyewe. Kama kuna mtu miongoni mwenu anadhani kuwa yeye ana hekima kwa kipimo cha nyakati hizi, basi afadhali awe mjinga ili apate kuwa na hekima ya kweli. 19 Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuuzi mbele za Mungu. Kama Maandiko yasemavyo, “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao.’ ’ 20 Na tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni bure.”

21 Kwa hiyo mtu asijivune kwa sababu ya watu. Kwa kuwa vitu vyote ni vyenu, 22 kama ni Paulo au Apolo au Petro au dunia au maisha au kifo, au wakati uliopo au wakati unaokuja, haya yote ni yenu; 23 na ninyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu.

And I, brethren, could not speak unto you as unto spiritual, but as unto carnal, even as unto babes in Christ.

I have fed you with milk, and not with meat: for hitherto ye were not able to bear it, neither yet now are ye able.

For ye are yet carnal: for whereas there is among you envying, and strife, and divisions, are ye not carnal, and walk as men?

For while one saith, I am of Paul; and another, I am of Apollos; are ye not carnal?

Who then is Paul, and who is Apollos, but ministers by whom ye believed, even as the Lord gave to every man?

I have planted, Apollos watered; but God gave the increase.

So then neither is he that planteth any thing, neither he that watereth; but God that giveth the increase.

Now he that planteth and he that watereth are one: and every man shall receive his own reward according to his own labour.

For we are labourers together with God: ye are God's husbandry, ye are God's building.

10 According to the grace of God which is given unto me, as a wise masterbuilder, I have laid the foundation, and another buildeth thereon. But let every man take heed how he buildeth thereupon.

11 For other foundation can no man lay than that is laid, which is Jesus Christ.

12 Now if any man build upon this foundation gold, silver, precious stones, wood, hay, stubble;

13 Every man's work shall be made manifest: for the day shall declare it, because it shall be revealed by fire; and the fire shall try every man's work of what sort it is.

14 If any man's work abide which he hath built thereupon, he shall receive a reward.

15 If any man's work shall be burned, he shall suffer loss: but he himself shall be saved; yet so as by fire.

16 Know ye not that ye are the temple of God, and that the Spirit of God dwelleth in you?

17 If any man defile the temple of God, him shall God destroy; for the temple of God is holy, which temple ye are.

18 Let no man deceive himself. If any man among you seemeth to be wise in this world, let him become a fool, that he may be wise.

19 For the wisdom of this world is foolishness with God. For it is written, He taketh the wise in their own craftiness.

20 And again, The Lord knoweth the thoughts of the wise, that they are vain.

21 Therefore let no man glory in men. For all things are your's;

22 Whether Paul, or Apollos, or Cephas, or the world, or life, or death, or things present, or things to come; all are your's;

23 And ye are Christ's; and Christ is God's.