Matoleo Kwa Ajili Ya Waamini

16 Na sasa kuhusu matoleo kwa ajili ya kuwasaidia watu wa Mungu. Kama nilivyoagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo. Siku ya kwanza ya juma kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake, na fedha hiyo aiweke ili nitaka pokuja pasiwepo na haja ya kufanya mchango. Nikishafika nita wapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili waweze kupeleka zawadi yenu Yerusalemu. Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.

Mipango Ya Paulo

Baada ya kupitia Makedonia, nitakuja kwenu; maana natazamia kupitia Makedonia. Pengine nitakaa nanyi kwa muda, au hata nitakaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili muweze kunisaidia katika safari zangu, po pote niendapo. Kwa maana sipendi niwaone sasa nikiwa napita; natarajia kuwa na muda wa kutosha wa kukaa nanyi, kama Bwana akiruhusu. Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste. Kwa maana mlango umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, na huko kuna wapinzani wengi . 10 Ikiwa Timotheo atakuja kwenu mkaribisheni asiwe na woga wo wote akiwa nanyi kwa sababu anaendeleza kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo. 11 Basi asiwepo mtu atakayemdharau. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunirudia. Namtegemea yeye pamoja na hao ndugu.

12 Na sasa, kuhusu ndugu yetu Apolo. Nilimsihi sana awa tembelee pamoja na wale ndugu wengine, lakini haikuwa mapenzi yake kuja huko wakati huu. Atakuja apatapo nafasi.

Maneno Ya Mwisho

13 Kesheni; simameni imara katika imani, muwe shujaa na hodari. 14 Fanyeni kila kitu katika upendo. 15 Sasa ndugu zangu, mnafahamu kwamba watu wa nyumbani kwa Stefana walikuwa waamini wa kwanza katika Akaya, nao wamejitoa kuwasaidia watu wa Mungu. 16 Nawasihi mnyenyekee na kufuata uongozi wa watu kama hawa, na wa kila mtendakazi mwenzenu na kila anayejibidisha katika kazi. 17 Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa maana hawa wamenisaidia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu. 18 Wao wameburudisha roho yangu na yenu pia. Watu kama hawa, wanastahili kutambuliwa. 19 Makanisa ya Asia wanawas alimu. Akila na Priska, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu katika Bwana. 20 Pia ndugu wote wanawasalimu. Sali mianeni kwa busu takatifu. 21 Mimi Paulo, kwa mkono wangu mwe nyewe, naandika salamu hii. 22 Kama mtu ye yote hampendi Bwana, na alaaniwe. ‘Maranatha.’ Bwana wetu, njoo! 23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.

Makusanyo kwa Ajili ya Waamini Katika Uyahudi

16 Sasa, kuhusu mchango wa pesa kwa ajili ya watu wa Mungu: Fanyeni kama nilivyoyaambia makanisa ya Galatia kufanya. Siku ya kwanza ya kila wiki, kila mmoja wenu achukue kiasi cha pesa kutoka kwenye pesa zake na azitenge. Akusanye kiasi anachoweza kutokana na anavyobarikiwa. Na hivyo hamtahitaji kukusanya nitakapokuja. Nitakapofika, nitatuma baadhi ya watu wapeleke sadaka yenu Yerusalemu. Hawa watakuwa wale ambao ninyi mtakubali kuwa waende. Nitawatuma na barua ya utambulisho. Ikiwa itakuwa vizuri kwangu kwenda pia, basi tutasafiri pamoja.

Mipango ya Paulo

Nimepanga kupitia Makedonia, hivyo nitakuja kwenu baada ya hapo. Pengine nitakaa kwenu kwa muda. Pengine nitakaa kwenu majira yote ya baridi. Hivyo mtaweza kunisaidia katika safari yangu, kila ninapokwenda. Sitaki kuja kuwaona sasa, kwa sababu nitaweza tu kukaa nanyi kwa muda mfupi, kabla haijanilazimu kwenda mahali pengine. Ninategemea kukaa pamoja nanyi kwa muda mrefu, ikiwa Bwana ataruhusu. Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste. Nitakaa hapa, kwa sababu sasa nimepewa fursa nzuri kwa kazi kubwa na inayokua. Na kuna watu wengi wanaopinga.

10 Timotheo atakapokuja kwenu, mjitahidi akae kwa raha na amani akiwa kwenu. Anafanya kazi kwa ajili ya Bwana kama mimi. 11 Hivyo yeyote miongoni mwenu asikatae kumpokea Timotheo. Msaidieni aendelee katika safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu. Ninategemea atakuja kwangu pamoja na ndugu wengine.

12 Na sasa kuhusu Apolo: Ninamsihi sana aje na ndugu wengine kuwatembelea ninyi huko Korintho. Hajataka kuja sasa, lakini atakuja kwenu atakapopata nafasi.

Paulo Amalizia Barua Yake

13 Iweni waangalifu. Simameni imara katika imani yenu. Mwe jasiri na wenye nguvu. 14 Fanyeni kila kitu katika upendo.

15 Mnajua kuwa Stefana na familia yake walikuwa waamini wa kwanza katika Akaya. Wamejitia katika kazi ya kuwahudumia watu wa Mungu. Ndugu zangu, ninawaomba, 16 mjiweke chini ya uongozi wa watu kama hawa na wengine wanaofanya kazi kwa bidii na kutumika pamoja nao.

17 Ninafurahi kwa sababu Stefana, Fortunato na Akaiko wamekuja. Hamko hapa pamoja nami lakini wamejaza nafasi yenu. 18 Wamekuwa faraja kuu kwangu na kwenu pia. Basi, mnapaswa kuitambua thamani ya watu kama hawa.

19 Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Priska wanawasalimu katika Bwana. Na kanisa linalokutana nyumbani mwao linawasalimu pia. 20 Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kila mmoja wenu kwa salamu maalum ya watu wa Mungu.[a]

21 Hii ni salamu yangu kwa mkono wangu mwenyewe: Paulo.

22 Ikiwa mtu yeyote hampendi Bwana, mwacheni mtu huyo abaki chini ya laana ya Mungu.

Njoo, Ewe Bwana![b]

23 Neema ya Bwana Yesu iwe pamoja nanyi.

24 Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu.

Footnotes

  1. 16:20 salamu maalum ya watu wa Mungu Kwa maana ya kawaida, “busu takatifu”.
  2. 16:22 Njoo, Ewe Bwana Hii ni tafsiri ya Kiaramu marana tha.