Utaratibu Wa Kuabudu

11 Niigeni mimi, kama mimi ninavyomuiga Kristo. Ninawasifu kwa sababu mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kuwa mnashika mafundisho niliyowakabidhi. Lakini napenda muelewe kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo. Kwa hiyo mwanamume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anaaib isha kichwa chake. Na mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anaaibisha kichwa chake, ni sawa kama ame nyoa nywele zote kichwani. Kama mwanamke hataki kufunika kichwa chake, nywele zake zinyolewe; na kama ni aibu kwa mwanamke kunyoa kichwa chake, au kukata nywele zake, basi afunike kichwa chake. Mwanamume asifunike kichwa chake kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume. Kwa maana mwanamume hakuumbwa kutoka kwa mwanamke, bali mwanamke ame toka kwa mwanamume. Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwa namke, bali mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume. 10 Hii ndio sababu inampasa mwanamke afunike kichwa chake na kwa ajili ya malaika. 11 Lakini katika Bwana mwanamke hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamume, wala mwanamume hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamke. 12 Kwa maana kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanamume, vivyo hivyo sasa mwanamume anazaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vinatoka kwa Mungu.

13 Amueni wenyewe, je, ni sawa kwa mwanamke kumwomba Mungu akiwa hakufunika kichwa chake? 14 Je, maumbile ya asili hayatu fundishi kuwa ni aibu kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu? 15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni sifa kwake. Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu za kumfunika. 16 Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.

Chakula Cha Bwana

17 Kuhusu maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu kwa sababu mikutano yenu inaleta madhara zaidi kuliko mema. 18 Kwanza, mna pokutana kama kanisa nasikia kwamba kuna mgawanyiko kati yenu, na kwa kiasi fulani naamini ndivyo ilivyo. 19 Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili wale walio wa kweli waweze kuonekana.

20 Mnapokutana pamoja hamli chakula cha Bwana. 21 Kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anaendelea na chakula chake bila kun goja wengine, na mmoja anabaki na njaa wakati mwingine analewa. 22 Je, hamwezi mkala na kunywa kwenye nyumba zenu? Au mnadharau kanisa la Mungu na kuwafedhehesha wasio na kitu? Niwaambie nini?

Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, sitawasifu!

23 Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale maagizo niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate, 24 naye akiisha kushukuru , akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, ambao ni kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” 25 Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, “Hiki kikombe ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo kwa ukumbusho wangu.” 26 Maana kila mlapo mkate huu na kunywa katika kikombe hiki, mnatangaza kifo cha Bwana mpaka atakapokuja.

27 Kwa hiyo mtu ye yote anayekula mkate huo au kukinywea kikombe hicho isivyostahili, atakuwa na hatia juu ya mwili na damu ya Bwana. 28 Kila mtu ajichunguze mwenyewe, na ndipo aule mkate na kukinywea kikombe. 29 Kwa maana mtu ye yote alaye na kunywa pasipo kutambua mwili wa Bwana, anajiletea hukumu juu yake mwenyewe. 30 Na hii ndio sababu wengi wenu ni wagonjwa na dhaifu, na wengine wamekufa. 31 Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingalihukumiwa. 32 Tunapohukumiwa na Bwana, anaturudi ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu. 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana pamoja kula, ngojaneni. 34 Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani ili mnapokutana pamoja msije mkahukumiwa. Na nitakapokuja nitawapa maagizo zaidi.

11 Fuateni mfano wangu, kama ninavyoufuata mfano wa Kristo.

Kanuni kwa Ajili ya Mikutano Yenu

Nawasifu kwa sababu daima mnanikumbuka mimi na kuyafuata mafundisho niliyowapa. Lakini ninataka mwelewe kuwa kichwa cha kila mwanaume ni Kristo. Na Kichwa cha mwanamke ni mwanaume.[a] Na Kichwa cha Kristo ni Mungu.

Kila mwanaume anayeomba au kutabiri akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake. Lakini kila mwanamke anayeomba au kutabiri pasipo kufunika kichwa chake anakiaibisha kichwa chake. Kwa jinsi hiyo anakuwa sawa na mwanamke yule aliyenyoa nywele zake. Ikiwa mwanamke hatafunika kichwa chake, basi na azinyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukata nywele zake au kuzinyoa kichwani mwake. Hivyo anapaswa kufunika kichwa chake.

Lakini mwanaume hapaswi kufunika kichwa chake, kwa sababu ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume. Mwanaume hakutoka kwa mwanamke bali mwanamke ndiye aliyetoka kwa mwanaume. Na mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke lakini mwanamke ndiye aliumbwa kwa ajili ya mwanaume. 10 Hivyo, kutokana na nilivyosema, mwanamke anapaswa kukitawala kichwa chake kwa kukifunika anapoomba au anapotabiri. Pia, anapaswa kufanya hivi kwa sababu ya malaika.[b]

11 Lakini katika Bwana mwanamke anamhitaji mwanaume, na mwanaume anamhitaji mwanamke. 12 Hii ni kweli kwa sababu mwanamke alitoka kwa mwanaume, lakini pia mwanaume anazaliwa na mwanamke. Hakika, kila kitu kinatoka kwa Mungu.

13 Amueni hili ninyi wenyewe: Je, ni sahihi mwanamke kumwomba Mungu akiwa hajafunika kichwa chake? 14 Je, si hata hali ya asili inatufundisha kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu? 15 Lakini kuwa na nywele ndefu ni heshima kwa mwanamke. Mwanamke amepewa nywele ndefu ili kufunika kichwa chake. 16 Baadhi ya watu wanaweza kuanzisha mabishano kuhusiana na yale niliyosema. Lakini desturi ambayo sisi na makanisa ya Mungu yanafuata ni hii: ya kwamba wanawake wanaweza kuomba na kutabiri ujumbe kutoka kwa Mungu, vichwa vyao vikiwa vimefunikwa.

Chakula cha Bwana

17 Siwasifu kwa mambo ninayowaambia sasa. Mikutano yenu inawaumiza kuliko inavyowasaidia. 18 Kwanza, nimesikia kuwa mnapokutana kama kanisa mmegawanyika. Hili si gumu kuliamini 19 kwa sababu ya fikra zenu kwamba imewapasa kuwa na makundi tofauti ili kuonesha ni akina nani walio waamini wa kweli!

20 Mnapokusanyika, hakika hamli chakula cha Bwana.[c] 21 Ninasema hivi kwa sababu mnapokula, kila mmoja anakula na kumaliza chakula chake pasipo kula na wengine. Baadhi ya watu hawapati chakula cha kutosha, ama kinywaji cha kutosha na hivyo kubaki na njaa na kiu, ambapo wengine wanakula na kunywa zaidi hata kulewa.[d] 22 Mnaweza kula na kunywa katika nyumba zenu. Inaonekana kuwa mnadhani kanisa la Mungu si muhimu. Mnawatahayarisha wasio na kitu. Niseme nini? Je, niwasifu? Hapana, siwezi kuwasifu katika hili.

23 Mafundisho niliyowafundisha ni yale yale niliyopokea kutoka kwa Bwana, ya kwamba usiku ule ambao Bwana Yesu alikamatwa, aliuchukua mkate 24 na akashukuru. Kisha akaumega na kusema, “Huu ni mwili wangu; ni kwa ajili yenu. Uleni mkate huu kwa ajili ya kunikumbuka mimi.” 25 Kwa namna hiyo hiyo, baada ya wote kula, Yesu alichukua kikombe cha divai na akasema, “Divai hii inawakilisha agano jipya ambalo Mungu anafanya na watu wake, linaloanza kwa sadaka ya damu yangu. Kila mnywapo divai hii, fanyeni hivi kwa ajili ya kunikumbuka mimi.” 26 Hii inamaanisha kuwa kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mnawaambia wengine kuhusu kifo cha Bwana mpaka atakaporudi.

27 Hivyo, ukiula mkate na kukinywea kikombe cha Bwana isivyostahili, unautendea dhambi mwili na damu ya Bwana. 28 Unapaswa kujichunguza mwenendo wako kabla ya kula mkate na kunywa kikombe. 29 Ukila na kunywa bila kuwajali wale ambao ndiyo mwili wa Bwana, kula na kunywa kwako kutasababisha uhukumiwe kuwa mwenye hatia. 30 Ndiyo sababu watu wengi katika kanisa lenu ni wagonjwa na dhaifu, na wengi wameshakufa. 31 Lakini ikiwa tungejichunguza kwa usahihi, Mungu asingetuhukumu. 32 Lakini Bwana anapotuhukumu, anatuadhibu ili kutuonesha njia sahihi. Hufanya hivi ili tusishutumiwe kuwa wakosa na tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.

33 Hivyo ndugu zangu, mnapokusanyika pamoja ili mle, subirianeni na mkaribishane kwa moyo wa upendo. 34 Ikiwa mtu yeyote anawaza kuhusu njaa yake mwenyewe, basi akae nyumbani kwake na ale huko! Fanyeni hivi ili kukutanika kwenu kusilete hukumu ya Mungu juu yenu. Nitakapokuja nitawaambia nini cha kufanya kuhusu masuala mengine.

Footnotes

  1. 11:3 mwanaume Au “Mume wake”.
  2. 11:10 sababu ya malaika Au “anapoomba au kuhubiri”. Inamwonyesha kila mtu wakiwemo na malaika kuwa anayo mamlaka kufanya hivi.
  3. 11:20 chakula cha Bwana Au “Mlo au Meza ya Bwana”. Mlo maalum ambao Yesu aliwaagiza wafuasi wake wale kwa ajili ya kumkumbuka. Tazama Lk 22:14-20.
  4. 11:21 wanakula … hata kulewa In maana, wengine wanabaki na njaa na kuwa na kiu, na wengine wanakula na kunywa zaidi hata kulewa.

11 Follow my example,(A) as I follow the example of Christ.(B)

On Covering the Head in Worship

I praise you(C) for remembering me in everything(D) and for holding to the traditions just as I passed them on to you.(E) But I want you to realize that the head of every man is Christ,(F) and the head of the woman is man,[a](G) and the head of Christ is God.(H) Every man who prays or prophesies(I) with his head covered dishonors his head. But every woman who prays or prophesies(J) with her head uncovered dishonors her head—it is the same as having her head shaved.(K) For if a woman does not cover her head, she might as well have her hair cut off; but if it is a disgrace for a woman to have her hair cut off or her head shaved, then she should cover her head.

A man ought not to cover his head,[b] since he is the image(L) and glory of God; but woman is the glory of man. For man did not come from woman, but woman from man;(M) neither was man created for woman, but woman for man.(N) 10 It is for this reason that a woman ought to have authority over her own[c] head, because of the angels. 11 Nevertheless, in the Lord woman is not independent of man, nor is man independent of woman. 12 For as woman came from man, so also man is born of woman. But everything comes from God.(O)

13 Judge for yourselves: Is it proper for a woman to pray to God with her head uncovered? 14 Does not the very nature of things teach you that if a man has long hair, it is a disgrace to him, 15 but that if a woman has long hair, it is her glory? For long hair is given to her as a covering. 16 If anyone wants to be contentious about this, we have no other practice—nor do the churches of God.(P)

Correcting an Abuse of the Lord’s Supper(Q)

17 In the following directives I have no praise for you,(R) for your meetings do more harm than good. 18 In the first place, I hear that when you come together as a church, there are divisions(S) among you, and to some extent I believe it. 19 No doubt there have to be differences among you to show which of you have God’s approval.(T) 20 So then, when you come together, it is not the Lord’s Supper you eat, 21 for when you are eating, some of you go ahead with your own private suppers.(U) As a result, one person remains hungry and another gets drunk. 22 Don’t you have homes to eat and drink in? Or do you despise the church of God(V) by humiliating those who have nothing?(W) What shall I say to you? Shall I praise you?(X) Certainly not in this matter!

23 For I received from the Lord(Y) what I also passed on to you:(Z) The Lord Jesus, on the night he was betrayed, took bread, 24 and when he had given thanks, he broke it and said, “This is my body,(AA) which is for you; do this in remembrance of me.” 25 In the same way, after supper he took the cup, saying, “This cup is the new covenant(AB) in my blood;(AC) do this, whenever you drink it, in remembrance of me.” 26 For whenever you eat this bread and drink this cup, you proclaim the Lord’s death until he comes.(AD)

27 So then, whoever eats the bread or drinks the cup of the Lord in an unworthy manner will be guilty of sinning against the body and blood of the Lord.(AE) 28 Everyone ought to examine themselves(AF) before they eat of the bread and drink from the cup. 29 For those who eat and drink without discerning the body of Christ eat and drink judgment on themselves. 30 That is why many among you are weak and sick, and a number of you have fallen asleep.(AG) 31 But if we were more discerning with regard to ourselves, we would not come under such judgment.(AH) 32 Nevertheless, when we are judged in this way by the Lord, we are being disciplined(AI) so that we will not be finally condemned with the world.(AJ)

33 So then, my brothers and sisters, when you gather to eat, you should all eat together. 34 Anyone who is hungry(AK) should eat something at home,(AL) so that when you meet together it may not result in judgment.

And when I come(AM) I will give further directions.

Footnotes

  1. 1 Corinthians 11:3 Or of the wife is her husband
  2. 1 Corinthians 11:7 Or Every man who prays or prophesies with long hair dishonors his head. But every woman who prays or prophesies with no covering of hair dishonors her head—she is just like one of the “shorn women.” If a woman has no covering, let her be for now with short hair; but since it is a disgrace for a woman to have her hair shorn or shaved, she should grow it again. A man ought not to have long hair
  3. 1 Corinthians 11:10 Or have a sign of authority on her