Utaratibu Wa Kuabudu

11 Niigeni mimi, kama mimi ninavyomuiga Kristo. Ninawasifu kwa sababu mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kuwa mnashika mafundisho niliyowakabidhi. Lakini napenda muelewe kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo. Kwa hiyo mwanamume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anaaib isha kichwa chake. Na mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anaaibisha kichwa chake, ni sawa kama ame nyoa nywele zote kichwani. Kama mwanamke hataki kufunika kichwa chake, nywele zake zinyolewe; na kama ni aibu kwa mwanamke kunyoa kichwa chake, au kukata nywele zake, basi afunike kichwa chake. Mwanamume asifunike kichwa chake kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume. Kwa maana mwanamume hakuumbwa kutoka kwa mwanamke, bali mwanamke ame toka kwa mwanamume. Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwa namke, bali mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume. 10 Hii ndio sababu inampasa mwanamke afunike kichwa chake na kwa ajili ya malaika. 11 Lakini katika Bwana mwanamke hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamume, wala mwanamume hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamke. 12 Kwa maana kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanamume, vivyo hivyo sasa mwanamume anazaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vinatoka kwa Mungu.

13 Amueni wenyewe, je, ni sawa kwa mwanamke kumwomba Mungu akiwa hakufunika kichwa chake? 14 Je, maumbile ya asili hayatu fundishi kuwa ni aibu kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu? 15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni sifa kwake. Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu za kumfunika. 16 Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.

Chakula Cha Bwana

17 Kuhusu maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu kwa sababu mikutano yenu inaleta madhara zaidi kuliko mema. 18 Kwanza, mna pokutana kama kanisa nasikia kwamba kuna mgawanyiko kati yenu, na kwa kiasi fulani naamini ndivyo ilivyo. 19 Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili wale walio wa kweli waweze kuonekana.

20 Mnapokutana pamoja hamli chakula cha Bwana. 21 Kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anaendelea na chakula chake bila kun goja wengine, na mmoja anabaki na njaa wakati mwingine analewa. 22 Je, hamwezi mkala na kunywa kwenye nyumba zenu? Au mnadharau kanisa la Mungu na kuwafedhehesha wasio na kitu? Niwaambie nini?

Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, sitawasifu!

23 Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale maagizo niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate, 24 naye akiisha kushukuru , akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, ambao ni kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” 25 Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, “Hiki kikombe ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo kwa ukumbusho wangu.” 26 Maana kila mlapo mkate huu na kunywa katika kikombe hiki, mnatangaza kifo cha Bwana mpaka atakapokuja.

27 Kwa hiyo mtu ye yote anayekula mkate huo au kukinywea kikombe hicho isivyostahili, atakuwa na hatia juu ya mwili na damu ya Bwana. 28 Kila mtu ajichunguze mwenyewe, na ndipo aule mkate na kukinywea kikombe. 29 Kwa maana mtu ye yote alaye na kunywa pasipo kutambua mwili wa Bwana, anajiletea hukumu juu yake mwenyewe. 30 Na hii ndio sababu wengi wenu ni wagonjwa na dhaifu, na wengine wamekufa. 31 Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingalihukumiwa. 32 Tunapohukumiwa na Bwana, anaturudi ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu. 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana pamoja kula, ngojaneni. 34 Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani ili mnapokutana pamoja msije mkahukumiwa. Na nitakapokuja nitawapa maagizo zaidi.

11 Be ye followers of me, even as I also am of Christ.

Now I praise you, brethren, that ye remember me in all things, and keep the ordinances, as I delivered them to you.

But I would have you know, that the head of every man is Christ; and the head of the woman is the man; and the head of Christ is God.

Every man praying or prophesying, having his head covered, dishonoureth his head.

But every woman that prayeth or prophesieth with her head uncovered dishonoureth her head: for that is even all one as if she were shaven.

For if the woman be not covered, let her also be shorn: but if it be a shame for a woman to be shorn or shaven, let her be covered.

For a man indeed ought not to cover his head, forasmuch as he is the image and glory of God: but the woman is the glory of the man.

For the man is not of the woman: but the woman of the man.

Neither was the man created for the woman; but the woman for the man.

10 For this cause ought the woman to have power on her head because of the angels.

11 Nevertheless neither is the man without the woman, neither the woman without the man, in the Lord.

12 For as the woman is of the man, even so is the man also by the woman; but all things of God.

13 Judge in yourselves: is it comely that a woman pray unto God uncovered?

14 Doth not even nature itself teach you, that, if a man have long hair, it is a shame unto him?

15 But if a woman have long hair, it is a glory to her: for her hair is given her for a covering.

16 But if any man seem to be contentious, we have no such custom, neither the churches of God.

17 Now in this that I declare unto you I praise you not, that ye come together not for the better, but for the worse.

18 For first of all, when ye come together in the church, I hear that there be divisions among you; and I partly believe it.

19 For there must be also heresies among you, that they which are approved may be made manifest among you.

20 When ye come together therefore into one place, this is not to eat the Lord's supper.

21 For in eating every one taketh before other his own supper: and one is hungry, and another is drunken.

22 What? have ye not houses to eat and to drink in? or despise ye the church of God, and shame them that have not? what shall I say to you? shall I praise you in this? I praise you not.

23 For I have received of the Lord that which also I delivered unto you, that the Lord Jesus the same night in which he was betrayed took bread:

24 And when he had given thanks, he brake it, and said, Take, eat: this is my body, which is broken for you: this do in remembrance of me.

25 After the same manner also he took the cup, when he had supped, saying, this cup is the new testament in my blood: this do ye, as oft as ye drink it, in remembrance of me.

26 For as often as ye eat this bread, and drink this cup, ye do shew the Lord's death till he come.

27 Wherefore whosoever shall eat this bread, and drink this cup of the Lord, unworthily, shall be guilty of the body and blood of the Lord.

28 But let a man examine himself, and so let him eat of that bread, and drink of that cup.

29 For he that eateth and drinketh unworthily, eateth and drinketh damnation to himself, not discerning the Lord's body.

30 For this cause many are weak and sickly among you, and many sleep.

31 For if we would judge ourselves, we should not be judged.

32 But when we are judged, we are chastened of the Lord, that we should not be condemned with the world.

33 Wherefore, my brethren, when ye come together to eat, tarry one for another.

34 And if any man hunger, let him eat at home; that ye come not together unto condemnation. And the rest will I set in order when I come.