Watumwa

Watumwa wote wawahesabu mabwana zao kuwa wanastahili hesh ima zote, ili watu wasije wakalitukana jina la Mungu pamoja na mafundisho yetu. Watumwa ambao mabwana zao ni waamini, wasikose kuwaheshimu kwa kuwa ni ndugu; bali watumike kwa ubora zaidi kwa sababu wale wanaonufaika kwa huduma yao ni waamini na ni wapendwa.

Fundisha na kuhimiza mambo haya. Mtu ye yote akifundisha kinyume cha haya na asikubaliane na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo, na mafundisho yanayo ambatana na kumcha Mungu, huyo amejaa majivuno na wala hafahamu cho chote. Mtu kama huyo ana uchu wa ubishi na mashindano ya maneno ambayo huleta wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya, na ugomvi wa mara kwa mara kati ya watu wenye mawazo maovu, ambao hawanayo ile kweli, na ambao hudhani kwamba kumcha Mungu ni njia ya kuchuma fedha.

Bali kumcha Mungu na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu cho chote hapa duniani, wala hatuwezi kutoka na kitu. Lakini kama tuna chakula na mavazi, basi tutaridhika. Watu wanaotamani kuwa matajiri huanguka katika majaribu na mtego na katika tamaa nyingi mbaya na za kijinga, ambazo huwato komeza wanadamu katika upotevu na maangamizi. 10 Maana kupenda fedha ni chanzo cha uovu wote. Tamaa ya fedha imewafanya wengine watangetange mbali na imani na kuteseka kwa huzuni nyingi.

Mawaidha Ya Paulo Kwa Timotheo

11 Lakini wewe mtu wa Mungu, epuka haya yote. Tafuta kupata haki, utauwa, imani, upendo, subira na upole. 12 Pigana ile vita njema ya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa ulipokiri lile ungamo lako jema mbele ya mashahidi wengi.

13 Mbele ya Mungu ambaye amevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Kristo Yesu ambaye kwa ushuhuda wake mbele ya Pontio Pilato alikiri lile ungamo jema, 14 ninakuamuru utunze amri hii bila doa wala lawama mpaka Bwana wetu Yesu Kristo atakapokuja. 15 Jambo hili Mungu atalitimiza kwa wakati wake mwenyewe, Mungu Mbarikiwa ambaye peke yake ndiye Atawalaye, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. 16 Yeye peke yake ndiye asiyekufa, na ndiye aishiye katika nuru isiyoweza kukaribiwa; hakuna mwanadamu ali yepata kumwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.

17 Uwaagize matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke matumaini yao katika mali ambayo haina hakika. Bali wam tumaini Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifu rahie. 18 Waambie watende wema, wawe matajiri katika matendo mema, wawe wakarimu na tayari kushiriki mali zao na wengine. 19 Kwa njia hii watajiwekea msingi imara kwa wakati ujao na hivyo watajipatia uzima ambao ni uzima kweli.

20 Timotheo, tunza vema yote uliyokabidhiwa. Epuka majadil iano yasiyo ya Mungu na mabishano ambayo kwa makosa huitwa elimu.

Maagizo maalumu kwa Watumwa

Wote ambao ni watumwa waoneshe heshima kubwa kwa mabwana zao. Ndipo jina la Mungu na mafundisho yetu hayatakosolewa. Baadhi ya watumwa wanao mabwana ambao ni waamini, hivyo hao ni ndugu. Je, inamaanisha wasiwaheshimu mabwana zao? Hapana, watawatumikia hata kwa uzuri zaidi, kwa sababu wanawasaidia waaminio, watu wawapende.

Haya ni mambo ambayo lazima uyafundishe na kumwambia kila mtu kufanya.

Mafundisho ya Uongo na Utajiri wa Kweli

Watu wengine wanafundisha uongo na hawakubaliani na mafundisho ya kweli ambayo yanatoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Hawakubali mafundisho ambayo yanatuongoza kumheshimu na kumpendeza Mungu. Wanajivunia wanayoyafahamu, lakini hawaelewi chochote. Wamepagawa na wana ugonjwa wa kupenda mabishano na mapigano ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, ugomvi, matusi, na uovu wa kutoaminiana. Daima wanaleta shida, kwa sababu ni watu ambao kufikiri kwao kumeharibiwa. Wamepoteza ufahamu wao wa ukweli. Wanafikiri kwamba kujifanya wanamheshimu Mungu ni njia ya kupata utajiri.

Kuishi kwa kumheshimu Mungu, hakika, ni njia ambayo watu hutajirika sana, kwa sababu inamaanisha wanaridhika na walivyo navyo. Tulipokuja ulimwenguni, tulikuja bila kitu, na tutakapokufa hatutachukua chochote. Hivyo, kama tukiwa na chakula na nguo, tutaridhika navyo. Watu ambao wanatamani kuwa matajiri wanajiletea majaribu wenyewe. Wananasa katika mtego. Wanaanza kutaka vitu vingi vya kijinga ambavyo vitawaumiza na kuwaharibu. 10 Kupenda fedha kunasababisha aina zote za uovu. Watu wengine wamegeuka kutoka kwenye imani yetu kwa sababu wanataka kupata fedha nyingi zaidi. Lakini wamejisababishia wenyewe maumivu mengi na huzuni.

Baadhi ya mambo ya Kukumbuka

11 Lakini wewe ni mali ya Mungu. Hivyo kaa mbali na mambo hayo yote, daima jaribu kutenda mema ili umheshimu Mungu na uwe na imani, upendo, uvumilivu, na upole. 12 Tunatakiwa tupigane kutunza imani yetu. Jaribu kwa bidii kadri unavyoweza kushinda vita vya thawabu. Tunza uzima wa milele. Ni uzima mliyouchagua kuupata mlipoikiri imani yenu katika Yesu; huo ukweli wa ajabu mliousema waziwazi kwa wote kuusikia. 13 Mbele ya Mungu na Kristo Yesu nakupa amri. Yesu ni yule aliyeshuhudia ukweli aliposimama mbele ya Pontio Pilato. Mungu ndiye anayetoa uhai kwa kila kitu. Nakuambia haya sasa: 14 Tenda niliyokuamuru kufanya bila dosari au kulaumu mpaka muda atakapo rudi. 15 Mungu atafanya hayo yatokee wakati utakapotimia. Yeye ni mwenye utukufu zaidi na mtawala pekee, mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. 16 Mungu pekee hafi, anaishi katika nuru angavu sana ambayo watu hawawezi kusogea karibu. Hakuna mtu aliyemwona Mungu; wala anayeweza kumuona. Heshima na nguvu ni zake milele. Amina.

17 Wape amri hii wale ambao ni matajiri wa vitu vya ulimwengu huu. Waambie wasiwe na majivuno, bali wamtumaini Mungu wala si katika fedha zao. Fedha haziwezi kuaminiwa, lakini Mungu anatuhudumia kwa ukarimu mkubwa na anatupa vitu vyote ili tufurahi. 18 Waambie wale ambao ni matajiri watende mema. Wawe matajiri katika kuzifanya kazi njema. Na uwambie wawe tayari kutoa na kuwapa wengine vitu. 19 Kwa kufanya hivi, watajiwekea hazina kwa ajili yao wenyewe. Na hazina hiyo itakuwa ni msingi imara huo utakuwa msingi imara ambao maisha yao ya siku zijazo yatajengwa. Wataweza kuwa na maisha yaliyo ya kweli kabisa.

20 Timotheo, Mungu ameweka vitu vingi kwako uvitunze. Uvitunze vyema. Jitenge na watu wanaosema mambo yasiyofaa ambayo hayatoki kwa Mungu na wale wanaokupinga na “elimu” ambayo siyo “elimu” kabisa. 21 Watu wengine wanaodai kuwa na “elimu” wamepotea mbali kabisa kutokana na wanachoamini.

Ninaomba neema ya Mungu iwe kwenu nyote.