Maisha Mapya

Basi kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, ninyi pia jiimarisheni kwa nia hiyo hiyo kwa maana mtu aliyekwisha kuteseka katika mwili hana uhusiano tena na dhambi. Matokeo yake ni kwamba, kwa muda wa maisha yake yaliyobakia hapa duniani, haishi tena kwa kufuata tamaa mbaya za mwili bali anaishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu. Maana mmekwisha kutumia muda wa kutosha katika maisha yenu yaliyopita mkifanya yale ambayo watu wasiomjua Mungu hupenda kutenda: uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulevi na ibada ovu za sanamu. Wanaona ajabu kwamba sasa hamshi riki tena pamoja nao katika ufisadi wao wa kinyama, nao huwatu kana. Lakini itawabidi kujieleza mbele zake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa. Kwa maana hii ndio sababu Injili ilihubiriwa hata kwa hao waliokufa: wahukumiwe kama wana damu wengine kuhusu maisha yao katika mwili, bali wapate kuishi katika roho kama Mungu aishivyo.

Kuja Kwa Kristo Kumekaribia

Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo muwe na akili timamu na wenye kiasi ili mweze kuomba. Zaidi ya yote, pen daneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi sana. Karibishaneni pasipo manung’uniko. 10 Kila mmoja na atumie kipawa alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu. 11 Mtu akisema kitu, basi na awe kama anayesema maneno halisi ya Mungu. Mtu anayetoa huduma na ahudumu kwa nguvu apewayo na Mungu; ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo. Yeye ni mwenye utukufu na uweza, milele na milele. Amina.

Kuteseka Kwa Mkristo

12 Wapendwa, msishangae kwa ajili ya mateso makali yanayowa pata kana kwamba ni kitu kigeni kinawatokea. 13 Bali furahini kwamba mnashiriki katika mateso ya Kristo, ili mpate kufurahi na kushangilia wakati utukufu wake utakapofunuliwa. 14 Kama mkilau miwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa Utukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yenu. 15 Lakini asiwepo mtu ye yote kati yenu ambaye atateswa kwa kuwa ni mwuaji, au mwizi, au mhalifu au anayejiingiza katika mambo ya watu wengine. 16 Lakini kama mtu akiteseka kwa kuwa ni mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu kwa jina hilo. 17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya watu wa Mungu; na kama itaanza na sisi, mwisho wa hao ambao hawatii Injili ya Mungu utakuwaje? 18 Na, “Kama ni vigumu kwa mtu wa haki kuokolewa, itakuwaje kwa mtu asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?” 19 Basi wale wanaoteswa kufuatana na mapenzi ya Mungu, wajikabidhi kwa Muumba wao aliye mwaminifu.

Maisha Mapya

Kristo aliteseka alipokuwa katika mwili wake. Hivyo mjitayarishe kwa fikra ile ile aliyokuwa nayo Kristo. Yeyote anayekubali kuteseka katika maisha haya hakika ameamua kuacha kutenda dhambi. Jiimarishe wenyewe ili mweze kuishi maisha yenu yaliyosalia hapa duniani kwa kutenda yale anayotaka Mungu, siyo maovu ambayo watu wanataka kufanya. Huko nyuma mmepoteza muda mwingi mkitenda yale ambayo wasiyomjua Mungu wanapenda kutenda. Mliishi kwa kutojali maadili, mkitenda maovu mliyotaka kutenda. Daima mlikuwa mnalewa, mlifanya sherehe mbaya za ulevi, na mlitenda mambo ya aibu katika ibada zenu za sanamu.

Na sasa “marafiki” zenu wa zamani wanaona ni ajabu kwamba ninyi hamshirikiani nao katika njia za maisha zilizo mbaya na zisizofaa wanazozifuata. Na hivyo wanasema mabaya juu yenu. Lakini itawalazimu kukutana na Mungu na kutoa maelezo juu ya yale waliyoyatenda. Yeye ndiye atakaye hukumu watu wote muda si mrefu, walio hai sasa na wale waliokwisha kufa. Walikosolewa na wengine katika maisha yao hapa duniani. Lakini ulikuwa mpango wa Mungu kwamba wasikie Habari Njema kabla hawajafa ili wawe na maisha mapya katika Roho.

Vitumieni vizuri vipawa vya Mungu

Wakati wa kila kitu kufikia mwisho wake umekaribia. Hivyo iweni waangalifu katika akili zenu na mjizuie kwa kila jambo. Hii itawasaidia katika maombi yenu. Jambo lililo muhimu kuliko yote, daima mpendane ninyi kwa ninyi kikamilifu, kwa sababu upendo huwawezesha kusamehe dhambi. Mkaribishane ninyi kwa ninyi katika nyumba zenu na kushiriki chakula kwa pamoja pasipo manunguniko. 10 Mungu amewapa neema yake kwa namna nyingi mbalimbali. Hivyo muwe watumishi wema na kila mmoja wenu atumie kipawa chochote alichopewa kwa njia iliyo bora katika kuhudumiana ninyi kwa ninyi. 11 Ikiwa kipawa chako ni kuhubiri, maneno yako yawe kama yanayotoka kwa Mungu. Ikiwa kipawa chako ni kuhudumu, unatakiwa kuhudumu kwa nguvu anazokupa Mungu. Ndipo Mungu atakaposifiwa kwa kila jambo katika Yesu Kristo. Uwezo na utukufu ni wake milele na milele. Amina.

Kuteseka kama mfuasi wa Kristo

12 Rafiki zangu, msishangae kwa sababu ya mateso mnayoyapata sasa, mateso hayo yanaijaribu imani yenu. Msidhani kuwa linalotokea kwenu ni jambo la ajabu. 13 Lakini mnapaswa kufurahi kwa kuwa mnayashiriki mateso ya Kristo. Mtafurahi na kujawa na raha wakati uweza wake mkuu utapodhihirishwa kwa ulimwengu. 14 Mhesabu kuwa ni heshima watu wanapowanenea mabaya kwa sababu mnamwakilisha Kristo. Linapotokea hilo inaonesha kuwa Roho wa Mungu, aliye Roho wa utukufu, yupo pamoja nanyi. 15 Mnaweza kupata mateso; lakini msiteseke kwa sababu mmeua, mmeiba, mmesababisha ghasia, au mmejaribu kutawala maisha ya watu wengine. 16 Lakini endapo utateswa kwa kuwa ni “Mkristo” basi usione haya. Bali umshukuru Mungu kwa kuwa unalibeba jina hilo. 17 Wakati wa kuanza hukumu umewadia. Hukumu hiyo itaanza na familia ya Mungu. Ikiwa itaanzia kwetu, nini kitawatokea wale wasioikubali Habari Njema ya Mungu?

18 “Iwapo ni vigumu hata kwa mtu mwema kuokolewa,
    nini kitatokea kwa yule aliye kinyume na Mungu na amejaa dhambi?”(A)

19 Hivyo kama mnateseka kwa sababu ya kutii mapenzi ya Mungu, yakabidhini maisha yenu kwake maana Yeye ndiye aliyewaumba, na hivyo mnapaswa kumwamini. Na anastahili kuthaminiwa na kuaminiwa.