Yesu Na Mwanamke Msamaria

Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kuba tiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana. Lakini kwa hakika Yesu hakubatiza, wanafunzi wake ndio waliokuwa wakibatiza watu. Bwana alipopata habari hizi aliondoka Yudea akarudi Galilaya. Katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.

Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu. Kisima cha Yakobo kilikuwa hapo na kwa kuwa Yesu alikuwa amechoka kutokana na safari, aliketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.

Mama mmoja Msamaria akaja kuteka maji na Yesu akamwambia, “Naomba maji ya kunywa.” Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula. Yule mama akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” -Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria. 10 Yesu akamjibu, “Kama ungelifahamu Mungu anataka kukupa nini, na mimi ninayekuomba maji ya kunywa ni nani, ungeliniomba nikupe maji ya uzima.”

11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kuchotea maji na kisima hiki ni kirefu . Hayo maji ya uzima utay apata wapi? 12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”

13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena. 14 Lakini ye yote atakayekunywa maji nitakay ompa mimi, hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa kama chemchemi itakayobubujika maji yenye uhai na kumpa uzima wa milele.”

15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuchota maji!”

16 Yesu akamjibu, “Nenda kamwite mumeo, kisha uje naye hapa.” 17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwam bia, “Umesema kweli kuwa huna mume. 18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanamume unayeishi naye sasa si mume wako!”

19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii. 20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu lakini ninyi Way ahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”

21 Yesu akamjibu, “Mama, niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu. 22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwab udu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi. 23 Lakini wakati unakuja, tena umekwisha timia, ambapo wale wanaoabudu inavyostahili watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu kwa njia hii ndio anaowataka Baba. 24 Mungu ni roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.” 25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masihi, aitwaye Kristo, anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”

26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye Masihi.”

Masihi.”

27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kum wona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemwuliza, “Unataka nini kwake?” au “Kwa nini unazungumza naye?”

28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaam bia watu, 29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote nili yowahi kufanya! Je, yawezekana huyu ndiye Masihi?”

30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.

31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau cho chote.”

32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”

33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?” 34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma, na kuikamilisha kazi yake. 35 Si mnao msemo kwamba, ‘Bado miezi minne tutavuna’? Hebu yaangalieni mashamba, jinsi mazao yalivyoiva tayari kuvunwa! 36 Mvunaji hupokea ujira wake, naye hukusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele. Kwa hiyo aliyepanda mbegu na anayevuna, wata furahi pamoja. 37 Ule msemo wa zamani kwamba , ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa. 38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi hiyo; ninyi mmefaidika kutokana na jasho lao!”

39 Wasamaria wengi walimwamini kutokana na ushuhuda wa yule mama alipowaambia kwamba, “Ameniambia mambo yote niliyowahi kutenda.” 40 Kwa hiyo wale Wasamaria walipokuja, walimsihi akae kwao, naye akakaa kwa siku mbili. 41 Watu wengi zaidi wakamwa mini kutokana na ujumbe wake. 42 Wakamwambia yule mama, sasa hatuamini tu kwa sababu ya yale uliyotuambia bali kwa kuwa tumem sikia sisi wenyewe, na tunajua hakika kwamba yeye ni Mwokozi wa ulimwengu.”

Yesu Amponya Mtoto Wa Afisa

43 Zile siku mbili zilipokwisha, Yesu aliondoka kwenda Gali laya. 44 Yesu mwenyewe alikwisha sema kwamba nabii haheshimiki nchini kwake. 45 Lakini alipofika, Wagalilaya walimpokea vizuri baada ya kuona mambo aliyofanya huko Yerusalemu wakati wa siku kuu, maana na wao walihudhuria.

46 Alikwenda tena mjini Kana katika Galilaya, kule alipo geuza maji kuwa divai. Na huko Kapernaumu alikuwapo afisa mmoja ambaye mtoto wake alikuwa mgonjwa. 47 Huyo afisa alipopata habari kuwa Yesu alikuwa amefika Galilaya kutoka Yudea, alikwenda akamwomba aje kumponya mwanae ambaye alikuwa mgonjwa karibu ya kufa.

48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu hamwezi kuamini pasipo kuona ishara na miujiza?”

49 Yule afisa akajibu, “Bwana, tafadhali njoo kabla mwa nangu hajafa.” 50 Yesu akamwambia, “Nenda nyumbani, mwanao ataishi.” Yule afisa akaamini maneno ya Yesu, akaondoka kurudi nyumbani. 51 Alipokuwa bado yuko njiani, alikutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanae alikuwa mzima. 52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.” 53 Yule baba akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao ataishi.” Kwa hiyo yeye, pamoja na jamaa yake yote wakamwamini Yesu.

54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Yudea.

Jesus Talks With a Samaritan Woman

Now Jesus learned that the Pharisees had heard that he was gaining and baptizing more disciples than John(A) although in fact it was not Jesus who baptized, but his disciples. So he left Judea(B) and went back once more to Galilee.

Now he had to go through Samaria.(C) So he came to a town in Samaria called Sychar, near the plot of ground Jacob had given to his son Joseph.(D) Jacob’s well was there, and Jesus, tired as he was from the journey, sat down by the well. It was about noon.

When a Samaritan woman came to draw water, Jesus said to her, “Will you give me a drink?”(E) (His disciples had gone into the town(F) to buy food.)

The Samaritan woman said to him, “You are a Jew and I am a Samaritan(G) woman. How can you ask me for a drink?” (For Jews do not associate with Samaritans.[a])

10 Jesus answered her, “If you knew the gift of God and who it is that asks you for a drink, you would have asked him and he would have given you living water.”(H)

11 “Sir,” the woman said, “you have nothing to draw with and the well is deep. Where can you get this living water? 12 Are you greater than our father Jacob, who gave us the well(I) and drank from it himself, as did also his sons and his livestock?”

13 Jesus answered, “Everyone who drinks this water will be thirsty again, 14 but whoever drinks the water I give them will never thirst.(J) Indeed, the water I give them will become in them a spring of water(K) welling up to eternal life.”(L)

15 The woman said to him, “Sir, give me this water so that I won’t get thirsty(M) and have to keep coming here to draw water.”

16 He told her, “Go, call your husband and come back.”

17 “I have no husband,” she replied.

Jesus said to her, “You are right when you say you have no husband. 18 The fact is, you have had five husbands, and the man you now have is not your husband. What you have just said is quite true.”

19 “Sir,” the woman said, “I can see that you are a prophet.(N) 20 Our ancestors worshiped on this mountain,(O) but you Jews claim that the place where we must worship is in Jerusalem.”(P)

21 “Woman,” Jesus replied, “believe me, a time is coming(Q) when you will worship the Father neither on this mountain nor in Jerusalem.(R) 22 You Samaritans worship what you do not know;(S) we worship what we do know, for salvation is from the Jews.(T) 23 Yet a time is coming and has now come(U) when the true worshipers will worship the Father in the Spirit(V) and in truth, for they are the kind of worshipers the Father seeks. 24 God is spirit,(W) and his worshipers must worship in the Spirit and in truth.”

25 The woman said, “I know that Messiah” (called Christ)(X) “is coming. When he comes, he will explain everything to us.”

26 Then Jesus declared, “I, the one speaking to you—I am he.”(Y)

The Disciples Rejoin Jesus

27 Just then his disciples returned(Z) and were surprised to find him talking with a woman. But no one asked, “What do you want?” or “Why are you talking with her?”

28 Then, leaving her water jar, the woman went back to the town and said to the people, 29 “Come, see a man who told me everything I ever did.(AA) Could this be the Messiah?”(AB) 30 They came out of the town and made their way toward him.

31 Meanwhile his disciples urged him, “Rabbi,(AC) eat something.”

32 But he said to them, “I have food to eat(AD) that you know nothing about.”

33 Then his disciples said to each other, “Could someone have brought him food?”

34 “My food,” said Jesus, “is to do the will(AE) of him who sent me and to finish his work.(AF) 35 Don’t you have a saying, ‘It’s still four months until harvest’? I tell you, open your eyes and look at the fields! They are ripe for harvest.(AG) 36 Even now the one who reaps draws a wage and harvests(AH) a crop for eternal life,(AI) so that the sower and the reaper may be glad together. 37 Thus the saying ‘One sows and another reaps’(AJ) is true. 38 I sent you to reap what you have not worked for. Others have done the hard work, and you have reaped the benefits of their labor.”

Many Samaritans Believe

39 Many of the Samaritans from that town(AK) believed in him because of the woman’s testimony, “He told me everything I ever did.”(AL) 40 So when the Samaritans came to him, they urged him to stay with them, and he stayed two days. 41 And because of his words many more became believers.

42 They said to the woman, “We no longer believe just because of what you said; now we have heard for ourselves, and we know that this man really is the Savior of the world.”(AM)

Jesus Heals an Official’s Son

43 After the two days(AN) he left for Galilee. 44 (Now Jesus himself had pointed out that a prophet has no honor in his own country.)(AO) 45 When he arrived in Galilee, the Galileans welcomed him. They had seen all that he had done in Jerusalem at the Passover Festival,(AP) for they also had been there.

46 Once more he visited Cana in Galilee, where he had turned the water into wine.(AQ) And there was a certain royal official whose son lay sick at Capernaum. 47 When this man heard that Jesus had arrived in Galilee from Judea,(AR) he went to him and begged him to come and heal his son, who was close to death.

48 “Unless you people see signs and wonders,”(AS) Jesus told him, “you will never believe.”

49 The royal official said, “Sir, come down before my child dies.”

50 “Go,” Jesus replied, “your son will live.”

The man took Jesus at his word and departed. 51 While he was still on the way, his servants met him with the news that his boy was living. 52 When he inquired as to the time when his son got better, they said to him, “Yesterday, at one in the afternoon, the fever left him.”

53 Then the father realized that this was the exact time at which Jesus had said to him, “Your son will live.” So he and his whole household(AT) believed.

54 This was the second sign(AU) Jesus performed after coming from Judea to Galilee.

Footnotes

  1. John 4:9 Or do not use dishes Samaritans have used