Kristo alituweka sisi huru ili tuwe na uhuru. Kwa hiyo simameni imara wala msikubali tena kulemewa na minyororo ya utumwa. Sikilizeni! Mimi Paulo nawaambieni kwamba kama mkiku bali kutahiriwa, basi Kristo hatawafaidia cho chote. Tena, napenda kumshuhudia kila mmoja wenu anayekubali kutahiriwa kwamba inampasa kushika sheria zote. Ninyi mnaotafuta kuhesabiwa haki kwa njia ya sheria fahamuni kwamba mmetengwa na Kristo, mko mbali na neema ya Mungu. Kwa maana, kwa msaada wa Roho wa Mungu, sisi tunangojea kwa matumaini kupata haki kwa njia ya imani. Kwa maana tukiwa ndani ya Kristo, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuleti faida yo yote, bali jambo la msingi ni kuwa na imani inayofanya kazi kwa upendo.

Mlikuwa mkienenda vizuri, sasa ni nani aliyewazuia msiitii kweli? Kushawishiwa huku hakutokani na yule anayewaita. Hamira kidogo sana inaweza kuchachusha donge zima. 10 Nina hakika katika Bwana kwamba mtakubaliana na msimamo wangu. Huyo anayewasumbueni atapata hukumu anayostahili hata akiwa nani. 11 Lakini ndugu zangu, kama mimi ninahubiri kwamba kutahiriwa ni lazima, kwa nini bado nateswa? Ingekuwa hivyo, mahubiri yangu juu ya msalaba wa Kristo yasingekuwa kikwazo tena. 12 Laiti hao wanaowavurugeni wangejikatakata wenyewe!

13 Ndugu zangu, ninyi mliitwa ili muwe watu huru. Hata hivyo msitumie uhuru wenu kuendelea kufuata tamaa za mwili, bali tumi kianeni ninyi kwa ninyi kwa upendo. 14 Kwa maana sheria yote hukamilika katika amri moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” 15 Lakini ikiwa mtaumana na kutafunana, basi jihadhar ini, msije mkaangamizana wenyewe kwa wenyewe.

Maisha Ya Kiroho

16 Kwa hiyo nasema, mruhusuni Roho atawale maisha yenu na msitafute kutimiza tamaa za mwili. 17 Kwa maana tamaa za mwili hushindana na Roho; na Roho hushindana na tamaa za mwili. Roho na mwili hupingana, na kwa sababu hiyo ninyi hamwezi kufanya yale mnayotaka. 18 Lakini kama mkiongozwa na Roho, hamko tena chini ya sheria.

19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri nayo ni haya: uasherati, uchafu, ufisadi, 20 kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, mafarakano, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine yanayofanana na hayo. Nawaonya, kama nilivyokwisha waonya kabla, kwamba watu watendao mambo kama haya, hawataurithi Ufalme wa Mungu. 22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumili vu, wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi. Hakuna sheria inayopinga mambo kama haya.

24 Wote walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na tamaa zake. 25 Kwa kuwa tunaishi kwa kuongozwa na Roho wa Mungu, basi tufuate uongozi wake. 26 Tusiwe watu wenye maji vuno, tusichokozane na wala tusioneane wivu. Kuchukuliana Mizigo

Freedom in Christ

It is for freedom that Christ has set us free.(A) Stand firm,(B) then, and do not let yourselves be burdened again by a yoke of slavery.(C)

Mark my words! I, Paul, tell you that if you let yourselves be circumcised,(D) Christ will be of no value to you at all. Again I declare to every man who lets himself be circumcised that he is obligated to obey the whole law.(E) You who are trying to be justified by the law(F) have been alienated from Christ; you have fallen away from grace.(G) For through the Spirit we eagerly await by faith the righteousness for which we hope.(H) For in Christ Jesus(I) neither circumcision nor uncircumcision has any value.(J) The only thing that counts is faith expressing itself through love.(K)

You were running a good race.(L) Who cut in on you(M) to keep you from obeying the truth? That kind of persuasion does not come from the one who calls you.(N) “A little yeast works through the whole batch of dough.”(O) 10 I am confident(P) in the Lord that you will take no other view.(Q) The one who is throwing you into confusion,(R) whoever that may be, will have to pay the penalty. 11 Brothers and sisters, if I am still preaching circumcision, why am I still being persecuted?(S) In that case the offense(T) of the cross has been abolished. 12 As for those agitators,(U) I wish they would go the whole way and emasculate themselves!

Life by the Spirit

13 You, my brothers and sisters, were called to be free.(V) But do not use your freedom to indulge the flesh[a];(W) rather, serve one another(X) humbly in love. 14 For the entire law is fulfilled in keeping this one command: “Love your neighbor as yourself.”[b](Y) 15 If you bite and devour each other, watch out or you will be destroyed by each other.

16 So I say, walk by the Spirit,(Z) and you will not gratify the desires of the flesh.(AA) 17 For the flesh desires what is contrary to the Spirit, and the Spirit what is contrary to the flesh.(AB) They are in conflict with each other, so that you are not to do whatever[c] you want.(AC) 18 But if you are led by the Spirit,(AD) you are not under the law.(AE)

19 The acts of the flesh are obvious: sexual immorality,(AF) impurity and debauchery; 20 idolatry and witchcraft; hatred, discord, jealousy, fits of rage, selfish ambition, dissensions, factions 21 and envy; drunkenness, orgies, and the like.(AG) I warn you, as I did before, that those who live like this will not inherit the kingdom of God.(AH)

22 But the fruit(AI) of the Spirit is love,(AJ) joy, peace,(AK) forbearance, kindness, goodness, faithfulness, 23 gentleness and self-control.(AL) Against such things there is no law.(AM) 24 Those who belong to Christ Jesus have crucified the flesh(AN) with its passions and desires.(AO) 25 Since we live by the Spirit,(AP) let us keep in step with the Spirit. 26 Let us not become conceited,(AQ) provoking and envying each other.

Footnotes

  1. Galatians 5:13 In contexts like this, the Greek word for flesh (sarx) refers to the sinful state of human beings, often presented as a power in opposition to the Spirit; also in verses 16, 17, 19 and 24; and in 6:8.
  2. Galatians 5:14 Lev. 19:18
  3. Galatians 5:17 Or you do not do what