Njia Ya Kweli Ya Wokovu

Hatimaye ndugu zangu, furahini katika Bwana. Mimi sichoki kuwaandikieni mambo yale yale niliyokwisha waandikia kwa maana najua kwamba yatakuwa ni kinga kwenu. Jihadharini na watenda maovu, hao mbwa, na wale wanaokaza mafundisho ya kutahiriwa. Sisi tumepokea tohara ya kweli, kwa maana tunamwabudu Mungu katika Roho. Sisi tunaona fahari kwa ajili ya maisha yetu ndani ya Kristo Yesu. Hatuweki matumaini yetu katika mambo ya mwili, ijapokuwa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuweka matumaini katika mambo hayo. Kama mtu mwingine ye yote anadhani kuwa anazo sababu za kuweka matumaini yake katika mambo ya mwili, basi mimi ninazo sababu zaidi. Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwis raeli wa kabila la Benjamini; Mwebrania halisi. Kuhusu mambo ya kushika sheria, mimi nilikuwa Mfarisayo; na kwa upande wa juhudi, mimi nilikuwa na bidii katika kutesa kanisa; na kuhusu haki ipatikanayo kwa kutii sheria, mimi nilikuwa sina hatia.

Lakini mambo hayo niliyoyaona mwanzo kuwa ni faida kwangu, sasa nayaona kuwa ni hasara kwa ajili ya Kristo. Zaidi ya hayo, nahesabu mambo yote kuwa hasara tupu yakilinganishwa na faida kubwa ninayopata kwa kumjua Kristo Yesu aliye Bwana wangu. Kwa ajili yake nilikubali kupoteza kila kitu na kuona mambo hayo yote kuwa ni takataka ili nipate faida ya kuwa na Kristo; na nikiwa kwake nisionekane kama mtu mwenye haki yake mwenyewe, inayotokana na kushika sheria, bali niwe na ile haki inayotokana na kumwamini Kristo, ambaye yeye ni haki itokayo kwa Mungu inayopatikana kwa imani. 10 Nataka nimjue Kristo na nguvu ya ufufuo wake na nishi riki mateso yake, niwe kama yeye katika kifo chake; 11 na hivyo, kama ikiwezekana, niufikie ufufuo kutoka kwa wafu.

12 Sisemi kwamba nimekwisha kupokea haya yote, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha; bali nazidi kukaza mwendo ili nipate kile ambacho, kwa ajili yake, Kristo amenifanya niwe wake. 13 Ndugu zangu, bado sijihesabu kuwa nimekwisha pata ile zawadi. Lakini jambo moja ninalofanya ni kusahau mambo yote yali yopita, na kukaza mwendo kufikia yaliyo mbele yangu. 14 Nakaza na nifikie ushindi, ili nipate zawadi ambayo Mungu ameniitia mbinguni, nikiwa ndani ya Kristo Yesu.

15 Sisi tuliokomaa kiroho tuwe na msimamo kama huu. Lakini kama kuna mawazo tofauti kuhusu jambo lo lote, Mungu atawafunu lia. 16 Ila tushike sana yale tuliyokwisha kupokea.

17 Ndugu zangu, nawasihi mfuate mfano wangu, na muwatazame wale wanaofuata mfano tuliowapa. 18 Kwa maana, kama nilivyok wisha waambia kabla, na sasa nasema tena kwa machozi, wako watu wengi miongoni mwenu ambao maisha yao yanaonyesha kuwa wao ni adui wa msalaba wa Kristo. 19 Mwisho wa watu hao ni kuangamia, na Mungu wao ni tumbo; kwa sababu wao huyaonea fahari mambo ya aibu na mawazo yao yametawaliwa na mambo ya dunia. 20 Lakini uraia wetu uko mbinguni. Nasi tunangoja kwa hamu Mwokozi kutoka huko, yaani Bwana wetu Yesu Kristo, 21 ambaye, kwa uwezo unaomwezesha kutawala kila kitu, atabadilisha miili yetu midhaifu ili iwe na utukufu kama alionao yeye.