Sifa Za Kuhani Mkuu

Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa watu huteuliwa kumtumikia Mungu kwa niaba yao, kutoa sadaka na dhabihu kwa ajili ya dhambi zao. Anaweza kuwaonea huruma wale wasioel ewa na wanaopotoka kwa sababu yeye mwenyewe anasumbuliwa na udhaifu kama wao . Kwa sababu hii, anawajibika kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi za hao watu.

Hakuna mtu anayejichagulia heshima hii ya kuwa kuhani mkuu. Kila mmoja huitwa na Mungu kama vile Haruni alivyoitwa.

Kristo hakujichagulia mwenyewe utukufu wa kuwa kuhani mkuu. Bali aliteuliwa na Mungu ambaye alimwambia, “Wewe ni mwanangu, leo hii nimekuzaa;” na tena kama asemavyo mahali pengine, “Wewe ni kuhani milele, katika ngazi ile ya ukuhani ya Mel kizedeki. Yesu alipokuwa akiishi duniani, alitoa dua na maombi kwa kilio kikuu na machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa na kumtoa katika kifo, naye Mungu alimsikia kwa sababu alikuwa mnyenyekevu na mtiifu. Ingawa alikuwa Mwana wa Mungu, aliji funza utii kutokana na mateso aliyopata; na baada ya kufanywa mkamilifu, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii, 10 akateuliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu wa ngazi ile ile ya

Onyo Kuhusu Kuanguka

11 Kuhusu ukuhani huu, tunayo mengi ya kusema ambayo ni mag umu kuyaeleza, kwa maana ninyi si wepesi wa kuelewa. 12 Ingawa kwa wakati huu mngalipaswa kuwa walimu, lakini bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za kwanza za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana anayeishi kwa maziwa peke yake bado ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafund isho kuhusu neno la haki. 14 Bali chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, watu ambao wamekomaa akili kutokana na mafunzo ya mazoezi ya kupambanua kati ya mema na mabaya.