Tarumbeta Ya Tano

Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake, nikaona nyota iliyokuwa imeanguka kutoka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ili pewa ufunguo wa shimo la kuzimu. Alipolifungua hilo shimo, moshi ulitoka ndani yake kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vilitiwa giza kwa ajili ya ule moshi uliotoka katika shimo hilo. Kisha, katika ule moshi wakatoka nzige wakatua ardhini. Nao wakapewa nguvu kama nguvu ya nge wa duniani. Waliambiwa wasidhuru nyasi za nchi, wala majani, wala mmea au mti wo wote. Bali wawadhuru wale watu wasiokuwa na muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao. Waliruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano lakini wasiwaue. Na uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama uchungu wa mtu anapoumwa na nge. Katika siku hizo watu watata futa kifo lakini hawatakiona; watatamani kufa, lakini kifo kita wakimbia.

Wale nzige walionekana kama farasi waliotayarishwa kwa vita; vichwani mwao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu; na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu. Manyoya yao yalifanana kama nywele za wanawake; na meno yao yalikuwa kama meno ya simba. Walikuwa na magamba yaliyofanana na ngao za chuma; na kelele za mabawa yao zilikuwa kama kelele za magari ya farasi yenye farasi wanaokimbia kwenda vitani. 10 Walikuwa na mikia ya kuuma kama nge; nguvu yao ya kutesa watu kwa muda wa miezi mitano ilikuwa katika mikia yao. 11 Walikuwa na mfalme wa kuwatawala, naye ni malaika wa shimo la kuzimu ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Aba doni na kwa Kigiriki ni Apolioni.

12 Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanakuja.

Tarumbeta Ya Sita

13 Malaika wa sita akapiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe nne za madhabahu iliyoko mbele ya Mungu. 14 Sauti hiyo ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tar umbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa wa Efrati.” 15 Basi wakafunguliwa wale malaika wanne waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo na mwezi huo na mwaka huo, wawaue theluthi moja ya wanadamu. 16 Idadi ya majeshi wapandao farasi ilikuwa milioni mia mbili. 17 Na hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: wapanda farasi walivaa ngao vifuani zenye rangi ya moto na samawati na kiberiti. Na vichwa vya farasi hao vilikuwa kama vichwa vya simba; na moto, moshi na kiberiti vili kuwa vinatoka vinywani mwao. 18 Theluthi moja ya wanadamu waliu awa kwa maafa hayo matatu, yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliy otoka vinywani mwa hao farasi. 19 Nguvu ya hao farasi ilikuwa vinywani mwao na mikiani mwao; kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka wenye vichwa ambavyo vilitumika kuwadhuru watu.

20 Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika maafa hayo, bado walikataa kutubu na kuacha kuabudu vitu walivyotengeneza kwa mikono yao wenyewe. Waliendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu na za fedha na za shaba na za mawe na za miti, sanamu zisizoweza kuona, kusikia wala kutembea. 21 Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati na wizi.

The fifth angel sounded his trumpet, and I saw a star that had fallen from the sky to the earth.(A) The star was given the key(B) to the shaft of the Abyss.(C) When he opened the Abyss, smoke rose from it like the smoke from a gigantic furnace.(D) The sun and sky were darkened(E) by the smoke from the Abyss.(F) And out of the smoke locusts(G) came down on the earth and were given power like that of scorpions(H) of the earth. They were told not to harm(I) the grass of the earth or any plant or tree,(J) but only those people who did not have the seal of God on their foreheads.(K) They were not allowed to kill them but only to torture them for five months.(L) And the agony they suffered was like that of the sting of a scorpion(M) when it strikes. During those days people will seek death but will not find it; they will long to die, but death will elude them.(N)

The locusts looked like horses prepared for battle.(O) On their heads they wore something like crowns of gold, and their faces resembled human faces.(P) Their hair was like women’s hair, and their teeth were like lions’ teeth.(Q) They had breastplates like breastplates of iron, and the sound of their wings was like the thundering of many horses and chariots rushing into battle.(R) 10 They had tails with stingers, like scorpions, and in their tails they had power to torment people for five months.(S) 11 They had as king over them the angel of the Abyss,(T) whose name in Hebrew(U) is Abaddon(V) and in Greek is Apollyon (that is, Destroyer).

12 The first woe is past; two other woes are yet to come.(W)

13 The sixth angel sounded his trumpet, and I heard a voice coming from the four horns(X) of the golden altar that is before God.(Y) 14 It said to the sixth angel who had the trumpet, “Release the four angels(Z) who are bound at the great river Euphrates.”(AA) 15 And the four angels who had been kept ready for this very hour and day and month and year were released(AB) to kill a third(AC) of mankind.(AD) 16 The number of the mounted troops was twice ten thousand times ten thousand. I heard their number.(AE)

17 The horses and riders I saw in my vision looked like this: Their breastplates were fiery red, dark blue, and yellow as sulfur. The heads of the horses resembled the heads of lions, and out of their mouths(AF) came fire, smoke and sulfur.(AG) 18 A third(AH) of mankind was killed(AI) by the three plagues of fire, smoke and sulfur(AJ) that came out of their mouths. 19 The power of the horses was in their mouths and in their tails; for their tails were like snakes, having heads with which they inflict injury.

20 The rest of mankind who were not killed by these plagues still did not repent(AK) of the work of their hands;(AL) they did not stop worshiping demons,(AM) and idols of gold, silver, bronze, stone and wood—idols that cannot see or hear or walk.(AN) 21 Nor did they repent(AO) of their murders, their magic arts,(AP) their sexual immorality(AQ) or their thefts.