Mashahidi Wawili

11 Ndipo nikapewa kipimo kama fimbo, nikaambiwa, “Nenda kapime Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu na uwahesabu watu waabuduo humo. Lakini usipime uwanja wa nje ya Hekalu, uache, kwa sababu uwanja huo wamepewa mataifa wasiomjua Mungu. Wao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili. Nami nitawapa uwezo mashahidi wangu wawili watoe unabii kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini na mbili, wakiwa wamevaa magunia.”

Manabii hao wawili ni ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana na mbele ya nchi yote. Na mtu akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Na hivyo ndivyo atakavyokufa mtu ye yote atakayetaka kuwad huru. Watu hawa wanayo mamlaka ya kuyafunga mawingu ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Watakuwa na mamlaka juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuleta maafa ya kila aina ulimwenguni, kama wapendavyo. Lakini wakishamaliza kutoa unabii huo, yule mnyama atokaye katika shimo la kuzimu ata wapiga vita na kuwashinda na kuwaua. Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkuu ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo Bwana wao alisulubiwa. Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, lugha, taifa na rangi wataziangalia maiti zao, na hawataruhusu wazikwe. 10 Watu waishio duniani watafura hia kifo cha manabii hao wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu manabii hao waliwatesa watu waishio ulimwenguni.

11 Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu iliwaingia, nao wakasimama; wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu. 12 Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati maadui zao wakiwatazama. 13 Wakati huo huo, kukatokea tetemeko kuu la nchi, na sehemu moja ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo na waliosalimika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.

14 Maafa ya pili yamekwisha kupita. Lakini maafa ya tatu yanakuja upesi.

Tarumbeta Ya Saba

15 Kisha malaika wa saba akapiga tarumbeta yake. Na sauti kuu zikasikika mbinguni zikisema, “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” 16 Na wale wazee ishirini na wanne waketio mbele za Mungu katika viti vyao vya enzi wakaanguka kifudifudi wakamwabudu Mungu, 17 wakisema, “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi uli yeko na uliyekuwako; kwa kuwa umeuchukua uweza wako mkuu na ukaanza kutawala. 18 Watu wa mataifa walikasirika kwa kuwa wakati wa ghadhabu yako umefika. Wakati umefika wa kuwahukumu wafu na kuwapa tuzo watumishi wako manabii na watakatifu walioli tukuza jina lako, wakubwa kwa wadogo; na wakati umefika wa kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”

19 Kisha Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa na sanduku la agano lake likaonekana Hekaluni mwake. Kukatokea umeme, sauti, ngurumo na tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.

The Two Witnesses

11 I was given a reed like a measuring rod(A) and was told, “Go and measure the temple of God and the altar, with its worshipers. But exclude the outer court;(B) do not measure it, because it has been given to the Gentiles.(C) They will trample on the holy city(D) for 42 months.(E) And I will appoint my two witnesses,(F) and they will prophesy for 1,260 days,(G) clothed in sackcloth.”(H) They are “the two olive trees”(I) and the two lampstands, and “they stand before the Lord of the earth.”[a](J) If anyone tries to harm them, fire comes from their mouths and devours their enemies.(K) This is how anyone who wants to harm them must die.(L) They have power to shut up the heavens(M) so that it will not rain during the time they are prophesying;(N) and they have power to turn the waters into blood(O) and to strike the earth with every kind of plague as often as they want.

Now when they have finished their testimony, the beast(P) that comes up from the Abyss(Q) will attack them,(R) and overpower and kill them. Their bodies will lie in the public square of the great city(S)—which is figuratively called Sodom(T) and Egypt—where also their Lord was crucified.(U) For three and a half days some from every people, tribe, language and nation(V) will gaze on their bodies and refuse them burial.(W) 10 The inhabitants of the earth(X) will gloat over them and will celebrate by sending each other gifts,(Y) because these two prophets had tormented those who live on the earth.

11 But after the three and a half days(Z) the breath[b] of life from God entered them,(AA) and they stood on their feet, and terror struck those who saw them. 12 Then they heard a loud voice from heaven saying to them, “Come up here.”(AB) And they went up to heaven in a cloud,(AC) while their enemies looked on.

13 At that very hour there was a severe earthquake(AD) and a tenth of the city collapsed. Seven thousand people were killed in the earthquake, and the survivors were terrified and gave glory(AE) to the God of heaven.(AF)

14 The second woe has passed; the third woe is coming soon.(AG)

The Seventh Trumpet

15 The seventh angel sounded his trumpet,(AH) and there were loud voices(AI) in heaven, which said:

“The kingdom of the world has become
    the kingdom of our Lord and of his Messiah,(AJ)
    and he will reign for ever and ever.”(AK)

16 And the twenty-four elders,(AL) who were seated on their thrones before God, fell on their faces(AM) and worshiped God, 17 saying:

“We give thanks(AN) to you, Lord God Almighty,(AO)
    the One who is and who was,(AP)
because you have taken your great power
    and have begun to reign.(AQ)
18 The nations were angry,(AR)
    and your wrath has come.
The time has come for judging the dead,(AS)
    and for rewarding your servants the prophets(AT)
and your people who revere your name,
    both great and small(AU)
and for destroying those who destroy the earth.”

19 Then God’s temple(AV) in heaven was opened, and within his temple was seen the ark of his covenant.(AW) And there came flashes of lightning, rumblings, peals of thunder,(AX) an earthquake and a severe hailstorm.(AY)

Footnotes

  1. Revelation 11:4 See Zech. 4:3,11,14.
  2. Revelation 11:11 Or Spirit (see Ezek. 37:5,14)