Mungu Ajibu Sala Ya Kornelio

10 Katika mji wa Kaisaria aliishi afisa mmoja wa jeshi ambaye alikuwa kamanda wa kikosi cha Italia, jina lake Kornelio. Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na jamii yake yote. Alitoa msaada kwa ukarimu kwa watu na kumwomba Mungu mara kwa mara.

Alasiri moja, mnamo saa tisa, malaika wa Mungu alimjia katika ndoto na kumwita, “Kornelio!” Kornelio akamtazama yule malaika kwa hofu akasema, “Ni nini Bwana?” Malaika akasema, “Sala zako na sadaka ulizotoa kwa maskini zimefika mbinguni, na Mungu amezikumbuka. Sasa tuma watu Jopa wakamlete Simoni ait waye Petro. Yeye hivi sasa anaishi na Simoni mtengenezaji ngozi kando ya bahari.” Yule malaika aliyekuwa akizungumza naye ali poondoka, Kornelio aliwaita watumishi wake wawili na mlinzi wake mmoja aliyekuwa mcha Mungu, na baada ya kuwasimulia mambo yote yaliyotokea, akawatuma waende Jopa.

Kesho yake, walipokuwa wanaukaribia mji, Petro alipanda juu ghorofani kuomba mnamo saa sita. 10 Alipokuwa akisali aliona njaa akatamani kupata chakula. Lakini wakati kilipokuwa kinaan daliwa, alisinzia akaota ndoto. 11 Akaona katika ndoto mbingu zimefunguka na kitu kama shuka kubwa ikishushwa kwa ncha zake nne. 12 Ndani ya ile shuka walikuwemo aina zote za wanyama na nyoka na ndege. 13 Kisha sauti ikamwambia Petro, “Inuka, uchinje na ule mnyama ye yote umpendaye kati ya hawa.” 14 Petro akajibu, “La Bwana! Sijawahi kula cho chote ambacho kimetajwa na sheria zetu za Kiyahudi kuwa ni kichafu.” 15 Ile sauti ikarudia kusema naye mara ya pili, “Usiite cho chote alichokitakasa Bwana kuwa ni kichafu.” 16 Hii ilitokea mara tatu, ndipo ile shuka ikarudishwa mbinguni.

17 Petro alikuwa bado akijiuliza maana ya mambo haya aliyoy aona, wakati wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio walipofika kwenye nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi. 18 Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.

19 Wakati huo Petro alikuwa akifikiria juu ya ile ndoto, Roho Mtakatifu akamwambia, “Wako watu watatu wamekuja kukuta futa. 20 Shuka chini ukaonane nao na usione shaka kwenda nao kwa kuwa nimewatuma kwako.” 21 Petro akashuka, akawaendea wale watu akawaambia, “Mimi ndiye mnayemtafuta. Mnataka nini?” 22 Wao wakamjibu, “Tumetumwa na Kamanda Kornelio ambaye ni mtu mwema anayemcha Mungu na kusifiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagi zwa na malaika wa Mungu akukaribishe nyumbani kwake, ili asiki lize maneno utakayomwambia.” 23 Petro aliwakaribisha walale kwake. Kulipokucha akaandamana nao pamoja na baadhi ya ndugu waamini wa pale Jopa.

Petro Nyumbani Kwa Kornelio

24 Kesho yake wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwan goja pamoja na ndugu zake na marafiki wa karibu ambao alikuwa amewaalika. 25 Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akapiga magoti. 26 Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama! Mimi ni mwanadamu tu.” 27 Petro alipokuwa akizungumza naye aliingia ndani ambapo alikuta watu wengi wamekusanyika. 28 Petro akawaambia, “Mnajua kwamba sheria ya Wayahudi hairu husu Myahudi kuwatembelea au kuchangamana na watu wa mataifa men gine kama hivi nifanyavyo. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwone mtu ye yote kuwa mchafu au asiyefaa. 29 Ndiyo sababu ulipotuma nije sikusita. Kwa hiyo naomba unieleze kwa nini ume niita.” 30 Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa mchana. Mara akatokea mtu aliyevaa nguo za kung’ara akasimama mbele yangu. 31 Akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na Mungu, naye amekumbuka msaada wako kwa maskini. 32 Basi tuma watu waende Jopa wakamwite Simoni aitwaye Petro. Yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi ambaye nyumba yake iko sehemu za pwani.’ 33 Ndio sababu nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vizuri kuja. Basi sasa tuko hapa wote mbele ya Mungu kuyasikiliza yote ambayo Mungu amekuamuru kutuambia.”

Hotuba Ya Petro

34 “Ndipo Petro alianza kwa kusema, “Sasa naamini ya kuwa Mungu hana upendeleo. 35 Yeye huwakubali watu wa kila taifa wam chao na kutenda haki. 36 Huu ndio ujumbe ambao Mungu aliwapele kea watu wa Israeli, kuhusu Habari Njema za amani kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye ni Bwana wa wote. 37 Ninyi bila shaka mnafa hamu mambo yaliyotokea sehemu zote za Yudea, kuanzia Galilaya tangu wakati wa mahubiri ya Yohana Mbatizaji. 38 Mnafahamu jinsi Mungu alivyompa Yesu wa Nazareti Roho Mtakatifu na uwezo, na jinsi alivyozunguka kila mahali akifanya mema na kuponya wote waliokuwa wakiteswa na nguvu za shetani, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye. 39 Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyofanya katika nchi ya Wayahudi na Yerusalemu. Walimwua kwa kumtundika msalabani. 40 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamwezesha kuonekana na watu. 41 Hakuonekana kwa watu wote, lakini alionekana kwa mashahidi ambao Mungu aliwachagua, yaani sisi ambao tulikula na kunywa naye baada ya kufufuka kwake. 42 Naye alituamuru kuhubiri kwa watu wote, na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyechaguliwa na Mungu kuwahukumu walio hai na wafu. 43 Manabii wote walishuhudia juu yake, kwamba kila mtu amwami niye atasamehewa dhambi katika jina lake.”

Mataifa Wapokea Roho Mtakatifu

44 Petro alipokuwa akisema maneno hayo, Roho Mtakatifu ali washukia wote waliokuwa wakisikiliza. 45 Wale Wayahudi waamini waliokuwa wamekuja na Petro walishangaa sana kuona kuwa Mungu aliwapa watu wa mataifa kipawa cha Roho Mtakatifu. 46 Kwa kuwa waliwasikia wakisema kwa lugha mpya na kumtukuza Mungu kwa ukuu wake. Ndipo Petro akasema, 47 “Je, kuna mtu anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea.” 48 Kwa hiyo akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Wakamsihi Petro akae nao kwa siku chache.

Cornelius Calls for Peter

10 At Caesarea(A) there was a man named Cornelius, a centurion in what was known as the Italian Regiment. He and all his family were devout and God-fearing;(B) he gave generously to those in need and prayed to God regularly. One day at about three in the afternoon(C) he had a vision.(D) He distinctly saw an angel(E) of God, who came to him and said, “Cornelius!”

Cornelius stared at him in fear. “What is it, Lord?” he asked.

The angel answered, “Your prayers and gifts to the poor have come up as a memorial offering(F) before God.(G) Now send men to Joppa(H) to bring back a man named Simon who is called Peter. He is staying with Simon the tanner,(I) whose house is by the sea.”

When the angel who spoke to him had gone, Cornelius called two of his servants and a devout soldier who was one of his attendants. He told them everything that had happened and sent them to Joppa.(J)

Peter’s Vision(K)

About noon the following day as they were on their journey and approaching the city, Peter went up on the roof(L) to pray. 10 He became hungry and wanted something to eat, and while the meal was being prepared, he fell into a trance.(M) 11 He saw heaven opened(N) and something like a large sheet being let down to earth by its four corners. 12 It contained all kinds of four-footed animals, as well as reptiles and birds. 13 Then a voice told him, “Get up, Peter. Kill and eat.”

14 “Surely not, Lord!”(O) Peter replied. “I have never eaten anything impure or unclean.”(P)

15 The voice spoke to him a second time, “Do not call anything impure that God has made clean.”(Q)

16 This happened three times, and immediately the sheet was taken back to heaven.

17 While Peter was wondering about the meaning of the vision,(R) the men sent by Cornelius(S) found out where Simon’s house was and stopped at the gate. 18 They called out, asking if Simon who was known as Peter was staying there.

19 While Peter was still thinking about the vision,(T) the Spirit said(U) to him, “Simon, three[a] men are looking for you. 20 So get up and go downstairs. Do not hesitate to go with them, for I have sent them.”(V)

21 Peter went down and said to the men, “I’m the one you’re looking for. Why have you come?”

22 The men replied, “We have come from Cornelius the centurion. He is a righteous and God-fearing man,(W) who is respected by all the Jewish people. A holy angel told him to ask you to come to his house so that he could hear what you have to say.”(X) 23 Then Peter invited the men into the house to be his guests.

Peter at Cornelius’s House

The next day Peter started out with them, and some of the believers(Y) from Joppa went along.(Z) 24 The following day he arrived in Caesarea.(AA) Cornelius was expecting them and had called together his relatives and close friends. 25 As Peter entered the house, Cornelius met him and fell at his feet in reverence. 26 But Peter made him get up. “Stand up,” he said, “I am only a man myself.”(AB)

27 While talking with him, Peter went inside and found a large gathering of people.(AC) 28 He said to them: “You are well aware that it is against our law for a Jew to associate with or visit a Gentile.(AD) But God has shown me that I should not call anyone impure or unclean.(AE) 29 So when I was sent for, I came without raising any objection. May I ask why you sent for me?”

30 Cornelius answered: “Three days ago I was in my house praying at this hour, at three in the afternoon. Suddenly a man in shining clothes(AF) stood before me 31 and said, ‘Cornelius, God has heard your prayer and remembered your gifts to the poor. 32 Send to Joppa for Simon who is called Peter. He is a guest in the home of Simon the tanner, who lives by the sea.’ 33 So I sent for you immediately, and it was good of you to come. Now we are all here in the presence of God to listen to everything the Lord has commanded you to tell us.”

34 Then Peter began to speak: “I now realize how true it is that God does not show favoritism(AG) 35 but accepts from every nation the one who fears him and does what is right.(AH) 36 You know the message(AI) God sent to the people of Israel, announcing the good news(AJ) of peace(AK) through Jesus Christ, who is Lord of all.(AL) 37 You know what has happened throughout the province of Judea, beginning in Galilee after the baptism that John preached— 38 how God anointed(AM) Jesus of Nazareth with the Holy Spirit and power, and how he went around doing good and healing(AN) all who were under the power of the devil, because God was with him.(AO)

39 “We are witnesses(AP) of everything he did in the country of the Jews and in Jerusalem. They killed him by hanging him on a cross,(AQ) 40 but God raised him from the dead(AR) on the third day and caused him to be seen. 41 He was not seen by all the people,(AS) but by witnesses whom God had already chosen—by us who ate(AT) and drank with him after he rose from the dead. 42 He commanded us to preach to the people(AU) and to testify that he is the one whom God appointed as judge of the living and the dead.(AV) 43 All the prophets testify about him(AW) that everyone(AX) who believes(AY) in him receives forgiveness of sins through his name.”(AZ)

44 While Peter was still speaking these words, the Holy Spirit came on(BA) all who heard the message. 45 The circumcised believers who had come with Peter(BB) were astonished that the gift of the Holy Spirit had been poured out(BC) even on Gentiles.(BD) 46 For they heard them speaking in tongues[b](BE) and praising God.

Then Peter said, 47 “Surely no one can stand in the way of their being baptized with water.(BF) They have received the Holy Spirit just as we have.”(BG) 48 So he ordered that they be baptized in the name of Jesus Christ.(BH) Then they asked Peter to stay with them for a few days.

Footnotes

  1. Acts 10:19 One early manuscript two; other manuscripts do not have the number.
  2. Acts 10:46 Or other languages