Mfano Wa Wafanyakazi Katika Shamba La Mizabibu

20 “Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mtu mwenye shamba la mizabibu aliyeondoka alfajiri kwenda kutafuta vibarua wa kufanya kazi shambani kwake. Wakapatana kuwa atawalipa msha hara wa kutwa, yaani dinari moja, akawapeleka shambani.

“Mnamo saa tatu akaondoka tena akawakuta watu wengine wamesimama sokoni bila kazi. Akawaambia, ‘Ninyi pia nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu na nitawalipa haki yenu.’ Kwa hiyo wakaenda. Mnamo saa sita na pia saa tisa alion doka tena akafanya hivyo hivyo. Mnamo saa kumi na moja akaon doka tena akawakuta watu wengine bado wanazurura. Akawauliza, ‘Kwa nini mmesimama hapa kutwa nzima pasipo kufanya kazi?’ Wakamjibu, ‘Ni kwa kuwa hakuna aliyetuajiri.’ Akawaambia, ‘Ninyi pia nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la miza bibu.’

“Ilipofika jioni, yule mwenye shamba akamwita msimamizi wa vibarua akamwambia, ‘Waite wafanyakazi uwalipe ujira wao, ukian zia na wale walioajiriwa mwisho na kuishia na wale walioajiriwa kwanza.’ Wale vibarua walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakaja na kila mmoja wao akalipwa dinari moja. 10 Basi wale wal ioajiriwa kwanza walipofika, walidhani watalipwa zaidi. Lakini kila mmoja wao pia alipewa dinari moja. 11 Walipoipokea, wakaanza kumlalamikia yule mwenye shamba wakisema, 12 ‘Hawa watu walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu. Ime kuwaje wewe ukawalipa sawa na sisi ambao tumefanya kazi ngumu na kuchomwa na jua mchana kutwa?’

13 “Yule mwenye shamba akamjibu mmoja wao, ‘Rafiki, sija kudhulumu. Je, hatukupatana kwamba utafanya kazi kwa dinari moja? 14 Chukua haki yako uende. Mimi nimeamua kumlipa huyu mtu ali yeajiriwa mwisho sawa na wewe. 15 Je, siwezi kufanya nipendavyo na mali yangu? Au unaona wivu kwa kuwa nimekuwa mkarimu?’ 16 Hali kadhalika, wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”

Yesu Azungumza Tena Kuhusu Kifo Chake

17 Yesu alipokuwa akienda Yerusalemu aliwachukua kando wale wanafunzi wake kumi na wawili akawaambia, 18 “Sasa tunakwenda Yerusalemu na mimi Mwana wa Adamu nitatiwa mikononi mwa makuhani wakuu na walimu wa sheria nao watanihukumu adhabu ya kifo 19 na kunikabidhi kwa watu wa mataifa ambao watanizomea na kunipiga mijeledi na kunisulubisha; na siku ya tatu nitafufuliwa.”

Ombi La Mama Wa Wana Wa Zebedayo

20 Kisha mama yao wana wa Zebedayo akaja kwa Yesu akiwa na wanae, akapiga magoti akamwomba aseme neno.

21 Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Akajibu, “Tafadhali, ruhusu wanangu hawa, waketi mmoja upande wako wa kulia na mwin gine upande wako wa kushoto katika Ufalme wako.”

22 Yesu akawaambia, “Hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kuny wea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.’ ’

23 Akawaambia, “Kikombe changu mtakinywea. Lakini kuhusu kuketi kulia au kushoto kwangu, sina mamlaka ya kuwaruhusu. Nafasi hizo ni za wale ambao Baba yangu amewaandalia.”

24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya waliwakasi rikia hao ndugu wawili. 25 Lakini Yesu akawaita wote pamoja aka waambia, “Mnafahamu kuwa watawala wa mataifa hupenda kuheshi miwa, na wenye vyeo hupenda kuonyesha mamlaka yao. 26 Isiwe hivyo kwenu. Badala yake, anayetaka kuwa mkuu kati yenu hana budi kuwa mtumishi wenu. 27 Na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu ni lazima awe mtumishi wenu; 28 kama vile ambavyo mimi Mwana wa Adamu sikuja ili nitumikiwe bali kutumika na kutoa maisha yangu kuwa fidia kwa ajili ya watu wengi.”

Yesu Awaponya Vipofu Wawili

29 Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu, walimfuata. 30 Vipofu wawili waliokuwa wameketi kando ya barabara waliposikia kwamba ni Yesu aliyekuwa akipita, wakapiga kelele wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuonee huruma.” 31 Watu wakawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao walizidi kupiga kelele wakisema, “ Bwana, Mwana wa Daudi, tuonee huruma.” 32 Yesu akasimama na akawaita, akawau liza, “Mnataka niwafanyie nini?” 33 Wakamjibu, “Bwana tuna taka kuona.”

34 Yesu akawaonea huruma, akawagusa, na mara wakaweza kuona; wakamfuata.