Upendo Na Utii

Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini kama mtu ye yote akitenda dhambi, tunaye mtetezi wetu kwa Baba, yaani Yesu Kristo mwenye haki. Kristo ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya dhambi zetu, na wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.

Na tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua Kristo ikiwa tunatii amri zake. Mtu ye yote akisema, “Ninamjua’ Lakini mtu ye yote anayetii neno lake, huyo ndiye ambaye upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kwa kweli. Hivi ndivyo tunavy ojua kuwa tumo ndani ya Kristo. Mtu anayesema anadumu ndani ya Kristo anapaswa kuishi kama Yesu Kristo mwenyewe alivyoishi.

Wapendwa, siwaandikii amri mpya bali amri ile ambayo mme kuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilok wisha kusikia. Lakini hata hivyo amri hii ninayowaandikieni ni mpya; ambayo ukweli wake unaonekana kwake na kwenu, kwa sababu giza linatoweka na nuru ya kweli imekwishaanza kuangaza. Mtu anayesema kwamba anaishi nuruni, naye anamchukia ndugu yake, bado yumo gizani. 10 Anayempenda ndugu yake anaishi katika nuru na wala hana kitu cha kumfanya ajikwae. 11 Lakini anayemchukia ndugu yake anaishi gizani na anatembea gizani, wala hajui aen dako, kwa sababu giza limempofusha macho.

Kwa Watoto, Baba Na Vijana

12 Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Ninawaandikieni ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliyekuwapo tangu mwanzo. Ninawaandikieni ninyi vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Ninawandikieni ninyi watoto, kwa kuwa mmemjua Baba. 14 Ninawaan dikieni ninyi akina baba, kwa kuwa mmemjua yeye aliyekuwapo tangu mwanzo. Ninawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Msipende Dunia

15 Msiipende dunia wala mambo yaliyomo duniani. Kama mtu akiipenda dunia, hawezi kumpenda Baba. 16 Maana vitu vyote vil ivyomo duniani, yaani, tamaa za mwili, tamaa ya vitu vinavyoone kana kwa macho, na kiburi kiletwacho na mali, vyote hivi havitoki kwa Baba bali hutoka ulimwenguni. 17 Nayo dunia inapita na tamaa zake zote zinapita, lakini mtu anayetimiza mapenzi ya Mungu huishi milele.

Onyo Kuhusu Adui Wa Kristo

18 Watoto wapendwa, huu ni wakati wa mwisho. Na kama mlivy okwisha kusikia kwamba yule mpinga-Kristo anakuja, hata sasa wapinga-Kristo wengi wamekwisha kuja. Kwa hiyo tunajua kuwa huu ni wakati wa mwisho. 19 Watu hao walitoka kati yetu, lakini hawakuwa wa kundi letu. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangeende lea kuishi pamoja nasi; lakini waliondoka ili iwe wazi kuwa hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kundi letu.

20 Lakini ninyi mmemiminiwa Roho Mtakatifu na nyote mnaijua kweli. 21 Siwaandikii hivi kwa kuwa hamuijui kweli bali kwa sababu mnaijua na kwa kuwa hakuna uongo utokao katika kweli. 22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni yule anayekana kwamba Yesu si Kristo. Mtu huyo ndiye mpinga-Kristo, anayemkana Baba na Mwana. 23 Mtu anayemkana Mwana hawezi kumjua Baba; mtu anayemkiri Mwana anamjua na Baba pia.

24 Hakikisheni kwamba ujumbe mliosikia tangu mwanzo unadumu mioyoni mwenu. Ujumbe huo ukikaa mioyoni mwenu, ninyi pia mtadumu ndani ya Mwana na ndani ya Baba. 25 Na yeye ametuahidi uzima wa milele.

26 Ninawaandikia mambo haya kuhusu wale wanaojaribu kuwapo tosha. 27 Lakini yule Roho Mtakatifu mliyempokea anakaa ndani yenu wala hamhitaji mtu kuwafundisha. Lakini kama vile huyo Roho Mtakatifu anavyowafundisha mambo yote, naye ni wa kweli wala si wa uongo; kama alivyowafundisha, dumuni ndani yake.

Watoto Wa Mungu

28 Na sasa, wanangu, kaeni siku zote ndani yake, kusudi ata kapotokea tuwe na ujasiri na wala tusijitenge naye kwa kuona aibu atakapokuja.

29 Kama mnajua kwamba yeye ni wa haki, basi mnajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.