Karama Za Roho Mtakatifu

12 Sasa kuhusu karama za Roho Mtakatifu ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu. Mnajua kwamba mlipokuwa hamumjui Mungu mlivutwa na kupotoshwa na sanamu bubu.

Kwa hiyo napenda mfahamu ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kukiri, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu. Basi kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni mmoja. Pia kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni mmoja. Kisha kuna aina tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule anayeongoza kazi zote kwa kila mtu. Roho Mtakatifu hudhi hirishwa kwa kila mtu kwa faida ya wote.

Maana mtu mmoja hupewa neno la hekima na huyo Roho, na mwingine hupewa neno la ufahamu kutoka kwa Roho huyo huyo. Mtu mwingine hupewa imani na huyo Roho na mwingine karama za kuponya. 10 Huyo huyo Roho humpa mwingine uwezo wa kufanya miujiza, mwin gine unabii, mwingine uwezo wa kutofautisha kati ya roho mbalim bali, mwingine aina za lugha na mwingine uwezo wa kutafsiri lugha. 11 Lakini ni Roho huyo huyo mmoja anayefanya haya yote, naye hugawa karama kwa kila mtu, kama yeye mwenyewe apendavyo.

Mwili Mmoja, Viungo Vingi

12 Kama vile mwili ulivyo mmoja lakini una viungo vingi, na viungo vyote ingawa ni vingi vinafanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo na Kristo. 13 Kwa maana tumebatizwa na Roho mmoja katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wagiriki, kama ni watumwa au watu huru; nasi tumepewa tunywe, huyo Roho mmoja.

14 Mwili si kiungo kimoja, bali una viungo vingi. 15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si sehemu ya mwili.” Hiyo isingefanya huo mkono usiwe sehemu ya mwili. 16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si sehemu ya mwili.” Hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili. 17 Kama mwili mzima ungelikuwa jicho, ungelisikiaje? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, ungelinusa namna gani? 18 Lakini kama mwili ulivyo, Mungu alipanga viungo vyote katika mwili, kimoja kimoja, kama alivyopenda. 19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja mwili ungekuwa wapi? 20 Kama mwili ulivyo, kuna viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.

21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sikuhitaji!” Na kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sikuhitaji!” 22 Kinyume chake, vile viungo vya mwili ambavyo vinaonekana kuwa dhaifu ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana. 23 Na vile viungo vya mwili ambavyo tunav iona havina heshima ndivyo tunavipa heshima ya pekee. Na vile viungo vya mwili ambavyo hatuwezi kuvionyesha, tunavitunza kwa adabu 24 ambayo vile viungo vyenye uzuri wa kuonekana havihi taji. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile visivyokuwa na heshima, 25 ili pasiwe na mga wanyiko katika mwili, bali viungo vyote visaidiane kwa usawa. 26 Kama kiungo kimoja cha mwili kikiteseka, viungo vyote vinateseka pamoja; kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote vinafurahi pamoja.

27 Basi ninyi ni mwili wa Kristo, na kila mmoja wenu ni kiungo cha huo mwili. 28 Na Mungu ameteua katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, kisha waponyaji, wasaidizi, watawala, wasemaji wa lugha mbalimbali. 29 Je, wote ni mitume? Au wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote wanafanya miujiza? 30 Je, wote wana karama ya kuponya? Wote wanasema kwa lugha ngeni? Wote wanatafsiri lugha? 31 Basi takeni kwa moyo karama zilizo bora. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora kupita zote.

Concerning Spiritual Gifts

12 Now about the gifts of the Spirit,(A) brothers and sisters, I do not want you to be uninformed.(B) You know that when you were pagans,(C) somehow or other you were influenced and led astray to mute idols.(D) Therefore I want you to know that no one who is speaking by the Spirit of God says, “Jesus be cursed,”(E) and no one can say, “Jesus is Lord,”(F) except by the Holy Spirit.(G)

There are different kinds of gifts, but the same Spirit(H) distributes them. There are different kinds of service, but the same Lord. There are different kinds of working, but in all of them and in everyone(I) it is the same God(J) at work.

Now to each one the manifestation of the Spirit is given for the common good.(K) To one there is given through the Spirit a message of wisdom,(L) to another a message of knowledge(M) by means of the same Spirit, to another faith(N) by the same Spirit, to another gifts of healing(O) by that one Spirit, 10 to another miraculous powers,(P) to another prophecy,(Q) to another distinguishing between spirits,(R) to another speaking in different kinds of tongues,[a](S) and to still another the interpretation of tongues.[b] 11 All these are the work of one and the same Spirit,(T) and he distributes them to each one, just as he determines.

Unity and Diversity in the Body

12 Just as a body, though one, has many parts, but all its many parts form one body,(U) so it is with Christ.(V) 13 For we were all baptized(W) by[c] one Spirit(X) so as to form one body—whether Jews or Gentiles, slave or free(Y)—and we were all given the one Spirit to drink.(Z) 14 Even so the body is not made up of one part but of many.(AA)

15 Now if the foot should say, “Because I am not a hand, I do not belong to the body,” it would not for that reason stop being part of the body. 16 And if the ear should say, “Because I am not an eye, I do not belong to the body,” it would not for that reason stop being part of the body. 17 If the whole body were an eye, where would the sense of hearing be? If the whole body were an ear, where would the sense of smell be? 18 But in fact God has placed(AB) the parts in the body, every one of them, just as he wanted them to be.(AC) 19 If they were all one part, where would the body be? 20 As it is, there are many parts, but one body.(AD)

21 The eye cannot say to the hand, “I don’t need you!” And the head cannot say to the feet, “I don’t need you!” 22 On the contrary, those parts of the body that seem to be weaker are indispensable, 23 and the parts that we think are less honorable we treat with special honor. And the parts that are unpresentable are treated with special modesty, 24 while our presentable parts need no special treatment. But God has put the body together, giving greater honor to the parts that lacked it, 25 so that there should be no division in the body, but that its parts should have equal concern for each other. 26 If one part suffers, every part suffers with it; if one part is honored, every part rejoices with it.

27 Now you are the body of Christ,(AE) and each one of you is a part of it.(AF) 28 And God has placed in the church(AG) first of all apostles,(AH) second prophets,(AI) third teachers, then miracles, then gifts of healing,(AJ) of helping, of guidance,(AK) and of different kinds of tongues.(AL) 29 Are all apostles? Are all prophets? Are all teachers? Do all work miracles? 30 Do all have gifts of healing? Do all speak in tongues[d]?(AM) Do all interpret? 31 Now eagerly desire(AN) the greater gifts.

Love Is Indispensable

And yet I will show you the most excellent way.

Footnotes

  1. 1 Corinthians 12:10 Or languages; also in verse 28
  2. 1 Corinthians 12:10 Or languages; also in verse 28
  3. 1 Corinthians 12:13 Or with; or in
  4. 1 Corinthians 12:30 Or other languages